Tusaidiane; mwanamke mwenye vvu aweza kunyonyesha mtoto hadi mwaka mmoja na zaidi!?

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2011
Posts
1,684
Reaction score
2,156
Natumai mu wazima ndugu wana jamvi na mnaendelea kutafakari bajeti ya kwanza ya mh. SAADA MKUYA!

Pamoja na hayo naomba kufahamu hili jambo kama kweli kuna uwezekano wowote kwa mama kumnyonyesha mwanae hadi zaidi ya mwaka mmoja ikiwa ameshaathirika na ukimwi!

Je, kuna ushauri wanaopewa na wataalam au kuna dawa wanazopewa za kuwalinda watoto au hakuna uwezekano wowote wa jambo hilo na kama ikitokea mtoto huwa na hali gani!?

Naomba kuwasilisha.
 
Inawezekana kabisa mkuu..as long as mama yuko kwenye ARV's na anafuata ushauri atakaopewa clinic!
 
mkuu Mituni Twabona, nashukuru kwa mchango wako, na vipi kuhusu wale wanaokatazwa wao ARV wanakuwahawatumii!?
 
Hao wanaowakataza wanakosea sana kwani kwa mujibu wa muongozo wa WHO kuhusu unyonyeshaji kwa wamama wenye VVU inatakiwa wamama wote wenye VVU watumie dawa za kupunguza makali ya vvu maisha yao yote na wanyonyeshe watoto wao hadi umri usiopungua miaka 2 kwani hasara za kutonyonyesha ni kubwa kuliko za kunyonyesha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…