Tushauriane juu ya Kilimo cha Almond (Lozi): Changamoto, faida na maeneo yanayofaa

Tushauriane juu ya Kilimo cha Almond (Lozi): Changamoto, faida na maeneo yanayofaa

Jojo123

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2013
Posts
432
Reaction score
703
Wanakilimo mliobobea naomba mwenye kujua hatua za kilimo hiki na masoko yake au tu anielekeze kinalimwa wapi nitaenda kufuatilia mwenyewe kwa wenyeji.

Aksante

Almond.jpg
almondsnutrition.jpg
Almond-Tree-Badam-Tree.jpg
 
Kina hela sana sijui kwanini watu hawa kiongelei.. Kilo 30,000/= mpka 40,000/= supermarkt na Kariakoo..
 
Nami naitaji ipo.siku nitanunua nizipande nijaribu kama zinaota si amtaki kutuambia
 
Hapa nchini kuna sehemu wanalima hizi almonds?
 
naona ni miti mikubwa tu kama mibuni, sasa sijui ka mbegu zake sa supermarket zinaweza ota manake tayari zishakaushwa na umeme
 
Kuna aina nyingine ya nuts pia ina soko zuri sana inaitwa macadamia, mbegu zake pale SUA morogoro wanazo, nilipita hapo mwaka jana mche walikua wanauza 2000
 
naona ni miti mikubwa tu kama mibuni, sasa sijui ka mbegu zake sa supermarket zinaweza ota manake tayari zishakaushwa na umeme
Ni mikubwa zaidi ya mibuni inakua na kuzidi hata mkorosho, ila inaonyesha inahitaji mtaji usio na mawazo ikiwa unataka kulima kibiashara kwani shughuli yake si ya kitoto...
 
Ni mikubwa zaidi ya mibuni inakua na kuzidi hata mkorosho, ila inaonyesha inahitaji mtaji usio na mawazo ikiwa unataka kulima kibiashara kwani shughuli yake si ya kitoto...
mie nataka kuwa mojawapo unaweza ukanipa mwanga, na wapi nipate mbegu bora za hii mimea, nitauza mifugo yangu huko kijijini niweze himili hiki kilimo na naona hakishambuliwi na magonjwa kwa sana
 
mie nataka kuwa mojawapo unaweza ukanipa mwanga, na wapi nipate mbegu bora za hii mimea, nitauza mifugo yangu huko kijijini niweze himili hiki kilimo na naona hakishambuliwi na magonjwa kwa sana
Mkuu sina uzoefu na hii kitu zaidi ya kusoma kwenye makala ila hilo suala la mbegu ngoja nitauliza kwa jamaa wa kilimo pale wizarani tuone kama kuna uwezekano wa miche kupatikana...
 
Mkuu sina uzoefu na hii kitu zaidi ya kusoma kwenye makala ila hilo suala la mbegu ngoja nitauliza kwa jamaa wa kilimo pale wizarani tuone kama kuna uwezekano wa miche kupatikana...
nitashukuru sana mkuu, tena nitafurahi sana,
 
Kilimo chan Almonds kipo ktk mkoa wa Morogoro. Ni mmea mwepesi sana kuota na kukua, unahimili vyema mabadiliko ya hali ya hewa. Unahitaji hali ya hewa yenye mvua za kati na zaidi.

Hukua kwa urefu sana, ila ktk ukulima wa kisasa ni muhimu kupunguza matawi.

Tuwasiliane kwa ushauri zaidi. 0713370555
 
Kilimo chan Almonds kipo ktk mkoa wa Morogoro. Ni mmea mwepesi sana kuota na kukua, unahimili vyema mabadiliko ya hali ya hewa. Unahitaji hali ya hewa yenye mvua za kati na zaidi.

Hukua kwa urefu sana, ila ktk ukulima wa kisasa ni muhimu kupunguza matawi.

Tuwasiliane kwa ushauri zaidi. 0713370555
Sio nia yangu kukupinga. Ni majadiliano. Israel ndio mlimaji mkubwa na mtumiaji wa almond hapa duniani. Ni maoni yangu kuwa Singida inaweza kuwa mwafaka kwa kilimo hiki kwa sababu. Kinahitaji mvua kidogo ili kupata matunda ambayo yanahitaji jua kukauka.
Mie sio mtaalam wa kilimo. Ni maoni tu.
 
Kilimo chan Almonds kipo ktk mkoa wa Morogoro. Ni mmea mwepesi sana kuota na kukua, unahimili vyema mabadiliko ya hali ya hewa. Unahitaji hali ya hewa yenye mvua za kati na zaidi.

Hukua kwa urefu sana, ila ktk ukulima wa kisasa ni muhimu kupunguza matawi.

Tuwasiliane kwa ushauri zaidi. 0713370555
Morogoro sehemu gani wanalima almond?
 
NoSio nia yangu kukupinga. Ni majadiliano. Israel ndio mlimaji mkubwa na mtumiaji wa almond hapa duniani. Ni maoni yangu kuwa Singida inaweza kuwa mwafaka kwa kilimo hiki kwa sababu. Kinahitaji mvua kidogo ili kupata matunda ambayo yanahitaji jua kukauka.
Mie sio mtaalam wa kilimo. Ni maoni tu.
Waweza weka source ya Takwimu zako mkuu kuhusu largest producer?
 

Attachments

  • Screenshot_20241230-005155.png
    Screenshot_20241230-005155.png
    102.1 KB · Views: 15
Back
Top Bottom