SoC02 Tusiache nyuma afya ya akili. Hatua za haraka zinahitajika

SoC02 Tusiache nyuma afya ya akili. Hatua za haraka zinahitajika

Stories of Change - 2022 Competition

Chachasteven

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2014
Posts
1,941
Reaction score
2,044
Asubuhi moja ya Oktoba 2021, Kijana wa umri wa miaka 18 aitwaye Michael, mkazi wa Tabora, alikutwa chumbani kwake akiwa kajinyonga kwa kutumia shuka. Kwanini ajinyonge? Jibu lilikuwa pembeni ya mwili wake. Alikuwa ameacha ujumbe kwenye karatasi. Ujumbe mfupi tu. Haukuwa unazidi hata maneno kumi. Ujumbe ulikuwa ni maneno tisa; “Mama naomba unisamehe ni maisha tu yamenifanya nijiue mnizike.”

Inasikitisha!

Kwenye tukio lingine, miaka kadhaa iliyopita nikiwa napitia nyuzi humu JF, kuna bwana mmoja alitoa malalamiko kwamba baada ya mdogo wake kufeli mtihani wa kidato cha nne alianza kuonesha dalili za kuchanganyikiwa - Alikuwa anaongea maneno yasiyoeleweka na kufanya vitendo vya ajabu ambavyo mtu wa kawaida hawezi kufanya – Jambo moja aliloonyesha ilikuwa ni kuvutiwa na wanawake kupita kiasi na hofu ya mleta uzi ilikuwa ni kwamba siku moja angeweza kuwabaka dada zake na wanawake waliopo hapo nyumbani au hata kuwadhuru. Nilipopitia maoni nilisikitika. “Karogwa” ndiyo yalikuwa majibu ya watu! Ila ukweli ni kwamba “mdogo wa mleta uzi ule” hakuwa amerogwa. Ilikuwa ni Skizofrenia. Au kwa lugha rahisi moja ya magonjwa mengi ya afya ya akili!

Michael na “mdogo wa mleta uzi ule” ni mfano wa watu wengi ambao wanapitia changamoto ya afya ya akili.

Utauliza afya ya akili ni nini?Afya ya binadamu inamaanisha afya ya kimwili, kiakili na kisaikolojia kwa ujumla. Mazingira anayokaa mtu yanaathiri sana afya yake kwa nafasi kubwa. Mara nyingi watu hulalamika kuhusu afya ya kimwili tu na wanasahau afya ya akili na kisaikolojia. Ni rahisi kutambua mabadiliko ya mwili kwa dalili kama mafua, joto la mwili, maumivu ya kichwa au UVIKO-19. Lakini si watu wengi sana wanajua kufuatilia afya zao za akili.

Hivyo kukosa elimu ya afya ya akili na imani za kishirikina zinawaacha watu wengi kwenye mateso na maumivu ya ndani kwa ndani. Afya ya akili inahusisha kuanzia namna unavyofikiria, unavyohisi, pamoja na matendo yako. Hii inamaanisha maisha yako yanaathiriwa na afya ya akili kuanzia kijamii, kikazi na maisha binafsi. Afya ya akili ikiathirika inakuwa ni hatari kubwa sana kwa mhusika!

Baadhi ya sababu za watu kupatwa na tatizo la afya ya akili.

Mazingira: Kuishi kwenye mazingira magumu inaweza kusababisha mtu apate tatizo la afya ya akili. Mazingira kama umaskini au kuwa na familia ambayo inakunyanyapaa na kukudharau.
images.jpeg


Malezi na mikasa aliyopitia mhusika kipindi cha utoto: Hata kama ukiwa haupo kwenyemazingira magumu, mikasa uliyopitia utotoni inaweza kukusababishia tatizo la afya ya akili.

images (1).jpeg


Matukio ya kuhuzunisha: Matukio kama kupoteza umpendaye, au kutokufanikiwa mipango yako ni moja ya sababu za kupata tatizo la afya ya akili.

images (2).jpeg


Matumizi ya pombe na madawa ya kulevya: Hii ni sababu ya vijana wengi kujikuta tayari wana matatizo ya afya ya akili, na mara nyingi husababisha ugumu kupona.

images (3).jpeg


Watu wengi wenye matatizo ya afya ya akili hawajui namna nzuri ya kushughulikia matatizo yao ya afya ya akili, hivyo wanatumia njia ambazo zinaongeza hatari zaidi. Matokeo yake wanaishia kwenye matumizi ya dawa za kulevya, pombe au kujiua wakidhani hizi ni njia sahihi. Ila ukweli ni kinyume chake.

Ingawa kila mtu ana haki ya afya bora bila kujali hali yake ya kiuchumi na kijamii, ni watu wachache sana wanaoweza kupata elimu ya afya ya akili. Hivyo kuna haja ya serikali na taasisi zisizo za kiserikali kuwekeza kwenye ukanda huu. Ziandaliwe semina, makala, vitabu na filamu ili jamii itambue umuhimu wa afya ya akili.

Kuwa na afya bora ndiyo njia pekee ya kuishi maisha yenye maana na yanayotakiwa. Kwa ulimwengu wa sasa ambao umejaa uongo wa mitandaoni na changamoto nyingi za kimaisha inakuwa ni rahisi sana afya za akili kuathirika haswa rika la vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa lolote lile. Tena kwa jamii hii ambayo inachukulia mambo kwa kawaida sana. Hatari inakuwa kubwa zaidi.

Ni wakati sote tubadili imani zetu kuhusu suala la afya. Tusiishie kuzingatia afya ya mwili tu. Inapaswa kuizingatia afya ya akili na kisaikolojia pia kama tunataka kuishi vyema. Hata hivyo kuna baadhi ya vitu vichache ambavyo ukivizingatia unakuwa na nafasi kubwa ya kuwa na afya njema kwa ujumla – Yaani kimwili, kiakili na kisaikolojia.

Fanya mazoezi mara kwa mara: Mazoezi ni sehemu muhimu sana ya afya ya binadamu na kuyafanya au kutoyafanya kunaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa hali ya afya ya mtu. Hivyo ni jambo muhimu sana na inashauriwa na madaktari.
images (4).jpeg


Kula vyakula sahihi: Kutumia chakula sahihi itakusaidia sana. Jaribu kuacha kutumia vyakula vya kufungasha. Vyakula vya mafuta na uongeze tabia ya kula matunda na mbogamboga. Pia kula chakula bora itakusaidia sana kuwa na afya imara.
images (5).jpeg


Kunywa maji ya kutosha: Sio kila mtu anafahamu umuhimu wa kunywa maji mengi. Moja ya faida ya maji itakusaidia kuweka uzito wako sawa. Pia maji yanasaidia sana mwili kukamilisha shughuli zake. Usitafute sababu ya kuacha kunywa maji. Hakikisha unatembea na kopo la maji kila unapoenda.
images (6).jpeg


Pumzisha mwili: Njia nyingine nzuri ya kuilinda afya yako ni pamoja na kulala usingizi wa kutosha. Jitahidi kulala mapema na kuamka mapema. Hakika utaona mabadiliko kwenye afya yako kama utajiwekea ratiba nzuri ya kupumzika.
images (7).jpeg


Fanya vipimo mara kwa mara: Jitahidi kupima afya yako kila wakati. Wengi wetu huwa tunasubiria mpaka hali iwe mbaya ndipo tupime, ila hili ni kosa. Kupima mara kwa mara kutakusaidia kujua na kuelewa afya yako mapema kabla haujazidiwa na magonjwa. Kinga ni bora kuliko tiba!
images (8).jpeg


Punguza mawazo: Mawazo ni ugonjwa mbaya sana!. Mawazo husababisha kula sana, kulala kupita kawaida na sonona ambayo itapelekea matatizo makubwa kwenye afya yako kiujumla na ndiyo maana baadhi wanaenda kujiua. Lakini ukishirikisha watu kwenye matatizo itapunguza uwezekano wa wewe kuathirika na afya yako.
images (9).jpeg


HITIMISHO: Serikali, taasisi zisizo za kiserikali na watu binafsi wafanye jitihada za kutoa elimu kwa jamii, haswa makundi yanayoathirika, kuhusu elimu ya afya ya akili. Hii itapunguza hatari zinazowakumba wahusika kama Michael na wengine wengi.
 
Upvote 10
Elimu ya kutosha itolewe ili watu wafahamu uhalisia wa hili tatizo. Pia imani za kishirikina zisiwekwe Kama kipaumbele. Tatu, watu wazungumze mara kwa mara wanapohisi wanapitia changamoto kwenye maisha. Hii itasaidia sana.
Mimi na wewe tufanye Nini kumaliza tatizo hili?
 
Me mpaka kazi naziona mzigo sababu ya schizophrenia Mungu anisaidie
 
Tatizo linachochewa sana na mitandao ya kijamii tena siku hizi ni watu wa rika zote.

Wape elimu wale wanao kuzunguka kuhusu mitandao na kama ni watoto basi uwadhibiti maana sio rahisi serikali iliyo shindwa kujenga madawati ikakumbuka swala lililo jificha kama hilo
 
Me mpaka kazi naziona mzigo sababu ya schizophrenia Mungu anisaidie
Pole sana, ndugu. Jaribu kuwaona wanasaikolojia uwaelezee hali unayopitia. Pia tumia muda mwingi kujichanganya na watu. Hii itakusaidia kupunguza mawazo. Usipende kukaa peke yako na jitahidi kuwa na mawazo chanya. Epuka mawazo hasi.
 
Tatizo linachochewa sana na mitandao ya kijamii tena siku hizi ni watu wa rika zote.

Wape elimu wale wanao kuzunguka kuhusu mitandao na kama ni watoto basi uwadhibiti maana sio rahisi serikali iliyo shindwa kujenga madawati ikakumbuka swala lililo jificha kama hilo
Umenikumbusha kauli fulani, mitandao ya kijamii ni shetani mbaya kuliko wote ulimwenguni. Na maisha tunayoona wengine wanayaishi mitandaoni yanatufanya tujichukulie duni. Hii inazaa msongo wa mawazo. Hata kama una maisha bora utatamani ya mitandaoni halafu yatakuharibu akili yako. So sad mitandao inatumika kwa njia ambayo si sahihi.

Ni muhimu vijana wafundishwe wanachokiona mitandaoni kisiingilie uhalisia wa maisha yao.
 
Nimepitia tatizo kubwa sana la afya ya akili miezi kadhaa iliyopita na nilifikia hatua ya kutaka kabisa kujiua na nilikua naiona ni njia sahihi na ni bora sana, yani niliiona ni njia bora sana, yani niliiona itakua ni kama ntakua nimeachiwa huru kutoka jela.

Baada ya watu wa karibu kufahamu ilo, walinijia kwa masikitiko na kushangazwa kua kwanini nataka kufanya hivi na walionyesha kuguswa sana na wakawa karibu sana kunilinda. Kitu ambacho kilirudisha akili yangu ya kawaida kwa haraka sana na kugundua kua nataka kufanya kitu cha kijinga sana.

Baada ya pale nikawa fresh ila kuna muda ile hali kama ikawa inarudi. Ikawa sasa akili yangu ikitulia nakua nawaza nifanye njia gani ile hali isinirudie. Uamuzi wa kwanza ukawa ni kuacha kabisa kuvuta bangi, nilikua navuta bangi kila siku na kiukweli ndio ilikua chanzo kikubwa sana cha hii hali.

Iko hivi. Kuna mipango yangu ya kimaisha ilikua imefeli, jambo ambalo ni la kawaida kabisa na lisingeweza kunipa hali hii kama nisingekua navuta bangi. Sasa bangi ilichokua inakifanya kwangu ni kama mnavyojua wavutaji wenzangu, mda mwingi ilikua ikitokea nikafkiria hali yangu naifkiria kwa undani sana na napata picha ya kujiona kama mtu niliefeli kabisa. Ni aina ya thinking niliyokua naipata pale nikivuta bangi tu.

Kwaio ni kua bangi ilitaka kunipoteza kabisa na ndivyo hivyo inavyopoteza wengine kisaikolojia


Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kua, wakati ambao unakua na hali ngumu kimaisha ndio wakati ambao unatakiwa ujiepushe sana na vilevi ili kulinda afya yako ya akili. Badala yake fanya mazoezi na ujali mwili wako. Maisha yanabadilika muda wowote
 
Elimu ya kutosha itolewe ili watu wafahamu uhalisia wa hili tatizo. Pia imani za kishirikina zisiwekwe Kama kipaumbele. Tatu, watu wazungumze mara kwa mara wanapohisi wanapitia changamoto kwenye maisha. Hii itasaidia sana.
Tatizo ni unamweleza nani. Kuna watu unawaeleza badala ya kukushauri wanaanza kukushangaa
 
Umenikumbusha kauli fulani, mitandao ya kijamii ni shetani mbaya kuliko wote ulimwenguni. Na maisha tunayoona wengine wanayaishi mitandaoni yanatufanya tujichukulie duni. Hii inazaa msongo wa mawazo. Hata kama una maisha bora utatamani ya mitandaoni halafu yatakuharibu akili yako. So sad mitandao inatumika kwa njia ambayo si sahihi.

Ni muhimu vijana wafundishwe wanachokiona mitandaoni kisiingilie uhalisia wa maisha yao.
Inaweza kuwa ni asilimia 10 au chini ya hapo ndio watu wanao faidika na mitandao ya hii,

Lakini wengi wao wanapata tabu sana hususani kwenye saikolojia.
 
Nimepitia tatizo kubwa sana la afya ya akili miezi kadhaa iliyopita na nilifikia hatua ya kutaka kabisa kujiua na nilikua naiona ni njia sahihi na ni bora sana, yani niliiona ni njia bora sana, yani niliiona itakua ni kama ntakua nimeachiwa huru kutoka jela.

Baada ya watu wa karibu kufahamu ilo, walinijia kwa masikitiko na kushangazwa kua kwanini nataka kufanya hivi na walionyesha kuguswa sana na wakawa karibu sana kunilinda. Kitu ambacho kilirudisha akili yangu ya kawaida kwa haraka sana na kugundua kua nataka kufanya kitu cha kijinga sana.

Baada ya pale nikawa fresh ila kuna muda ile hali kama ikawa inarudi. Ikawa sasa akili yangu ikitulia nakua nawaza nifanye njia gani ile hali isinirudie. Uamuzi wa kwanza ukawa ni kuacha kabisa kuvuta bangi, nilikua navuta bangi kila siku na kiukweli ndio ilikua chanzo kikubwa sana cha hii hali.

Iko hivi. Kuna mipango yangu ya kimaisha ilikua imefeli, jambo ambalo ni la kawaida kabisa na lisingeweza kunipa hali hii kama nisingekua navuta bangi. Sasa bangi ilichokua inakifanya kwangu ni kama mnavyojua wavutaji wenzangu, mda mwingi ilikua ikitokea nikafkiria hali yangu naifkiria kwa undani sana na napata picha ya kujiona kama mtu niliefeli kabisa. Ni aina ya thinking niliyokua naipata pale nikivuta bangi tu.

Kwaio ni kua bangi ilitaka kunipoteza kabisa na ndivyo hivyo inavyopoteza wengine kisaikolojia


Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kua, wakati ambao unakua na hali ngumu kimaisha ndio wakati ambao unatakiwa ujiepushe sana na vilevi ili kulinda afya yako ya akili. Badala yake fanya mazoezi na ujali mwili wako. Maisha yanabadilika muda wowote
Pole sana, mkuu kwa changamoto uliyopitia. Umeandika vyema kabisa. Jambo la kwanza ni mtu kukubali ana tatizo fulani ndipo apate ufumbuzi wa shida yake. Wengi hawakubali matatizo waliyonayo ndiyo maana wanateseka. Pili, watu wa karibu ni Muhimu sana katika kumjenga mtu. Niwapongeze ndugu zako na wewe pia hongera kwa hatua ulizochukua kuacha uraibu wa madawa ya kulevya. Endelea kuwa balozi mzuri wa elimi hii.
 
Inaweza kuwa ni asilimia 10 au chini ya hapo ndio watu wanao faidika na mitandao ya hii,

Lakini wengi wao wanapata tabu sana hususani kwenye saikolojia.
Kweli, ndugu. Hali ni mbaya na inasikitisha sana. Watu wanataka kuishi maisha wanayoyaona mitandaoni - ikitokea wakashindwa basi wanaanza kuigiza. Tatizo tayari hilo - Ambalo baade mtu akiona ameshindwa kufikia maisha anayomuona yule anayemfuatilia anaishi, basi anakata tamaa kupelekea hatari kubwa zaidi. Kuna haja vijana waelimishwe kutofautisha maisha halisi na yale ya maigizo mitandaoni.
 
Tatizo ni unamweleza nani. Kuna watu unawaeleza badala ya kukushauri wanaanza kukushangaa
Elimu duni. Mimi naamini wenzetu wametupita vitu vingi kwa sababu hawachukulii mambo kawaida tu. Hata hivyo, hiyo haimaanishi utakosa mtu wa kumweleza kabisa namna unavyojihisi. Angalia watu wako wa karibu haswa wake unaowaamini na uwaeleze.

Wazungu Wana msemo wao ambao ukitafsiriwa kwa kiswahili utasimama Kama "kueleza tatizo lako ni nusu ya kulitatua."

Hivyo kushirikisha watu wako wa karibu kwenye matatizo kuna faida kubwa sana. Inaweza ikawa mke wako au yeyote unayemuamini.
 
Kiroho inaitwa kuuza nafsi yako kwa shetani. Yaani unakuwa na utupu au gap au uwazi kwenye akili kunakuwa na nafasi tupu itakiwayo kujazwa Ili akili ibalance thus watu ukimbilia kwenye ulevi, uzinzi, ulafi yaani uteja wa matendo yote ya mwili Ili kuijaza ile nafsi tupu Ili kuitafuta amani ya moyo kitendo hichi uitwa kuuza nafsi yako kwa shetani.
 
Asubuhi moja ya Oktoba 2021, Kijana wa umri wa miaka 18 aitwaye Michael, mkazi wa Tabora, alikutwa chumbani kwake akiwa kajinyonga kwa kutumia shuka. Kwanini ajinyonge? Jibu lilikuwa pembeni ya mwili wake. Alikuwa ameacha ujumbe kwenye karatasi. Ujumbe mfupi tu. Haukuwa unazidi hata maneno kumi. Ujumbe ulikuwa ni maneno tisa; “Mama naomba unisamehe ni maisha tu yamenifanya nijiue mnizike.”

Inasikitisha!

Kwenye tukio lingine, miaka kadhaa iliyopita nikiwa napitia nyuzi humu JF, kuna bwana mmoja alitoa malalamiko kwamba baada ya mdogo wake kufeli mtihani wa kidato cha nne alianza kuonesha dalili za kuchanganyikiwa - Alikuwa anaongea maneno yasiyoeleweka na kufanya vitendo vya ajabu ambavyo mtu wa kawaida hawezi kufanya – Jambo moja aliloonyesha ilikuwa ni kuvutiwa na wanawake kupita kiasi na hofu ya mleta uzi ilikuwa ni kwamba siku moja angeweza kuwabaka dada zake na wanawake waliopo hapo nyumbani au hata kuwadhuru. Nilipopitia maoni nilisikitika. “Karogwa” ndiyo yalikuwa majibu ya watu! Ila ukweli ni kwamba “mdogo wa mleta uzi ule” hakuwa amerogwa. Ilikuwa ni Skizofrenia. Au kwa lugha rahisi moja ya magonjwa mengi ya afya ya akili!

Michael na “mdogo wa mleta uzi ule” ni mfano wa watu wengi ambao wanapitia changamoto ya afya ya akili.

Utauliza afya ya akili ni nini?Afya ya binadamu inamaanisha afya ya kimwili, kiakili na kisaikolojia kwa ujumla. Mazingira anayokaa mtu yanaathiri sana afya yake kwa nafasi kubwa. Mara nyingi watu hulalamika kuhusu afya ya kimwili tu na wanasahau afya ya akili na kisaikolojia. Ni rahisi kutambua mabadiliko ya mwili kwa dalili kama mafua, joto la mwili, maumivu ya kichwa au UVIKO-19. Lakini si watu wengi sana wanajua kufuatilia afya zao za akili.

Hivyo kukosa elimu ya afya ya akili na imani za kishirikina zinawaacha watu wengi kwenye mateso na maumivu ya ndani kwa ndani. Afya ya akili inahusisha kuanzia namna unavyofikiria, unavyohisi, pamoja na matendo yako. Hii inamaanisha maisha yako yanaathiriwa na afya ya akili kuanzia kijamii, kikazi na maisha binafsi. Afya ya akili ikiathirika inakuwa ni hatari kubwa sana kwa mhusika!

Baadhi ya sababu za watu kupatwa na tatizo la afya ya akili.

Mazingira: Kuishi kwenye mazingira magumu inaweza kusababisha mtu apate tatizo la afya ya akili. Mazingira kama umaskini au kuwa na familia ambayo inakunyanyapaa na kukudharau.
View attachment 2306310

Malezi na mikasa aliyopitia mhusika kipindi cha utoto: Hata kama ukiwa haupo kwenyemazingira magumu, mikasa uliyopitia utotoni inaweza kukusababishia tatizo la afya ya akili.

View attachment 2306311

Matukio ya kuhuzunisha: Matukio kama kupoteza umpendaye, au kutokufanikiwa mipango yako ni moja ya sababu za kupata tatizo la afya ya akili.

View attachment 2306313

Matumizi ya pombe na madawa ya kulevya: Hii ni sababu ya vijana wengi kujikuta tayari wana matatizo ya afya ya akili, na mara nyingi husababisha ugumu kupona.

View attachment 2306314

Watu wengi wenye matatizo ya afya ya akili hawajui namna nzuri ya kushughulikia matatizo yao ya afya ya akili, hivyo wanatumia njia ambazo zinaongeza hatari zaidi. Matokeo yake wanaishia kwenye matumizi ya dawa za kulevya, pombe au kujiua wakidhani hizi ni njia sahihi. Ila ukweli ni kinyume chake.

Ingawa kila mtu ana haki ya afya bora bila kujali hali yake ya kiuchumi na kijamii, ni watu wachache sana wanaoweza kupata elimu ya afya ya akili. Hivyo kuna haja ya serikali na taasisi zisizo za kiserikali kuwekeza kwenye ukanda huu. Ziandaliwe semina, makala, vitabu na filamu ili jamii itambue umuhimu wa afya ya akili.

Kuwa na afya bora ndiyo njia pekee ya kuishi maisha yenye maana na yanayotakiwa. Kwa ulimwengu wa sasa ambao umejaa uongo wa mitandaoni na changamoto nyingi za kimaisha inakuwa ni rahisi sana afya za akili kuathirika haswa rika la vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa lolote lile. Tena kwa jamii hii ambayo inachukulia mambo kwa kawaida sana. Hatari inakuwa kubwa zaidi.

Ni wakati sote tubadili imani zetu kuhusu suala la afya. Tusiishie kuzingatia afya ya mwili tu. Inapaswa kuizingatia afya ya akili na kisaikolojia pia kama tunataka kuishi vyema. Hata hivyo kuna baadhi ya vitu vichache ambavyo ukivizingatia unakuwa na nafasi kubwa ya kuwa na afya njema kwa ujumla – Yaani kimwili, kiakili na kisaikolojia.

Fanya mazoezi mara kwa mara: Mazoezi ni sehemu muhimu sana ya afya ya binadamu na kuyafanya au kutoyafanya kunaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa hali ya afya ya mtu. Hivyo ni jambo muhimu sana na inashauriwa na madaktari.
View attachment 2306307

Kula vyakula sahihi: Kutumia chakula sahihi itakusaidia sana. Jaribu kuacha kutumia vyakula vya kufungasha. Vyakula vya mafuta na uongeze tabia ya kula matunda na mbogamboga. Pia kula chakula bora itakusaidia sana kuwa na afya imara.
View attachment 2306308

Kunywa maji ya kutosha: Sio kila mtu anafahamu umuhimu wa kunywa maji mengi. Moja ya faida ya maji itakusaidia kuweka uzito wako sawa. Pia maji yanasaidia sana mwili kukamilisha shughuli zake. Usitafute sababu ya kuacha kunywa maji. Hakikisha unatembea na kopo la maji kila unapoenda.
View attachment 2306302

Pumzisha mwili: Njia nyingine nzuri ya kuilinda afya yako ni pamoja na kulala usingizi wa kutosha. Jitahidi kulala mapema na kuamka mapema. Hakika utaona mabadiliko kwenye afya yako kama utajiwekea ratiba nzuri ya kupumzika.
View attachment 2306304

Fanya vipimo mara kwa mara: Jitahidi kupima afya yako kila wakati. Wengi wetu huwa tunasubiria mpaka hali iwe mbaya ndipo tupime, ila hili ni kosa. Kupima mara kwa mara kutakusaidia kujua na kuelewa afya yako mapema kabla haujazidiwa na magonjwa. Kinga ni bora kuliko tiba!
View attachment 2306305

Punguza mawazo: Mawazo ni ugonjwa mbaya sana!. Mawazo husababisha kula sana, kulala kupita kawaida na sonona ambayo itapelekea matatizo makubwa kwenye afya yako kiujumla na ndiyo maana baadhi wanaenda kujiua. Lakini ukishirikisha watu kwenye matatizo itapunguza uwezekano wa wewe kuathirika na afya yako.
View attachment 2306306

HITIMISHO: Serikali, taasisi zisizo za kiserikali na watu binafsi wafanye jitihada za kutoa elimu kwa jamii, haswa makundi yanayoathirika, kuhusu elimu ya afya ya akili. Hii itapunguza hatari zinazowakumba wahusika kama Michael na wengine wengi.
same story as always. Tukifanya tafiti tusikukute wewe mtoa mada una historia ya kutukana watu kwa namna yoyote ile ili kujifurahisha wewe mwenyewe na tukukute hujawahi kuyafanya maisha ya watu kuwa vituko sehemu yoyote. Otherwise na wewe una angukia kwenye sehemu ya watu wazima wenye afya ya akili lakini wenye matatizo makubwa na serious ya afya ya akili nadhani wewe una angukia kwenye kundi hili nilimention hapa, unaleta siasa kwenye saikolojia unajielewa wewe?
 
Pole sana, mkuu kwa changamoto uliyopitia. Umeandika vyema kabisa. Jambo la kwanza ni mtu kukubali ana tatizo fulani ndipo apate ufumbuzi wa shida yake. Wengi hawakubali matatizo waliyonayo ndiyo maana wanateseka. Pili, watu wa karibu ni Muhimu sana katika kumjenga mtu. Niwapongeze ndugu zako na wewe pia hongera kwa hatua ulizochukua kuacha uraibu wa madawa ya kulevya. Endelea kuwa balozi mzuri wa elimi hii.
Asante sana.
 
same story as always. Tukifanya tafiti tusikukute wewe mtoa mada una historia ya kutukana watu kwa namna yoyote ile ili kujifurahisha wewe mwenyewe na tukukute hujawahi kuyafanya maisha ya watu kuwa vituko sehemu yoyote. Otherwise na wewe una angukia kwenye sehemu ya watu wazima wenye afya ya akili lakini wenye matatizo makubwa na serious ya afya ya akili nadhani wewe una angukia kwenye kundi hili nilimention hapa, unaleta siasa kwenye saikolojia unajielewa wewe?
Nilikuwa na express ninachokifahamu, mkuu. Na Ndiyo maana nikasisitiza elimu itolewe ili tuwe na uelewa mpana kwenye tatizo hili. Asante, mkuu.
 
Back
Top Bottom