Tusichoke Kuyajadili Matatizo Ya Simba

Baba Kiki

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2012
Posts
1,544
Reaction score
943
Baada ya klabu ya Simba kuwa na mwenendo usiovutia kwa karibu msimu wa tatu mfululizo, yametolewa maoni mbalimbali na sababu lukuki kuhusiana na nini hasa kiini cha kuvurunda huku. Mojawapo kati ya sababu kubwa ambazo nimezisikia kwa muda mrefu ni kutokuwa fit kimwili kwa wachezaji wa Simba kiasi cha kupelekea kuchoka kadri muda unavyoendelea na kushindwa kuhimili mapambano ua muda mrefu.

Mmojawapo wa watoa hoja hiyo ni Mtemi Ramadhani kiungo nguli wa Simba wa miaka ya nyuma ambaye nimesikia mara nyingi akilirudia sababu hii na pia baadhi ya makocha na wachambuzi mbalimbali. Mimi pia naunga mkono hoja hii lakini pia naona kuwa haya ni matokeo zaidi ya matatizo ya ndani ya Simba ambayo naweza kudiriki kusema ni ya kujitakia.

Kwa uchunguzi wangu, Simba bado ni moja kati ya timu nzuri zilizoko katika ligi hii ya VPL lakini inakabiliwa na matatizo makubwa mawili ambayo ni ya kujitakia na hivyo yako ndani ya uwezo wao kuyasahihisha na tatizo moja dogo kama nitakavyoeleza hapa chini.

1. Kukosa mwendelezo (lacking consistence)
Imeshazungumzwa sana na hadi sasa inachosha kusema kuwa kikosi cha Simba hakina uzoefu wa kutosha kwa kuwa kinatumia wachezaji wengi vijana, lakini pia kikosi hakijazoeana tangu wachezaji hadi benchi la ufundi. Kutokana na matatizo haya yote, Simba, kwa misimu mitatu mfululizo haiianzii pale ilipoishia; ila kila msimu na kwa hakika ni kila nusu msimu (kila raundi) Simba ni kama huwa inaanza upya!!!

Kutokana na hali hii, timu haijengwi vizuri kwa maana ya kujengwa juu ya msingi hatua kwa hatua hadi kufikia ubora wa juu wa kikosi. Ndio maana Simba kupoteza wachezaji mihimili ktk kila idara ni kitu cha kawaida na hakishtui. Rejea Musoti, Tambwe, Kiemba, Chanongo, na Owino ambaye inasemekana yuko mguu ndani mguu nje. Mlundikano wa kukosa uzoefu kutokuzoena na benchi jipya kila baada ya miezi mitano ndio tatizo kubwa na la ndani kabisa la Simba
Hata matokeo ya kuchoka mapema inaweza kuwa ni matokeo ya mwalimu mpya kutohusika na maandalizi ya mwanzo wa msimu, kwa hiyo hii sio sababu ila ni matokeo.

2. Kukosa Mshikamano ndani ya Klabu na Timu
Taarifa za kutiliana mashaka baina ya mashabiki na mashabiki, mashabiki na watendaji na watendaji kwa watendaji, kushikana uchawi, kuhujumiana, n.k ni vitu vya kila siku ndani ya Simba kwa zaidi ya miaka 5 sasa. Madhara ya hali hii yako kisaikolojia zaii kwa kuwa watu na hasa wachezaji wanakuwa katika pressure kubwa muda wote na kadiri mechi inavyokuwa ngumu ndani ya uwanja ndio pressure huzidi na kivyo kuathiri performance ya wachezaji. Kila mtu ni shahidi Simba inapokuwa na umoja kama ambavyo hutokea umoja wa kinafiki wakati wa mechi za Yanga jinsi inavyokuwa hatari zaidi. Kwa lugha nyingine mapungufu mengine ktk kikosi yangeweza kuzibwa na umoja tu ndani na baina ya timu kwa kuongeza ari ya kupambana

3. Ligi ni Ngumu na Haitabiriki
Hiki ni kitu ambacho watu wengi na hususani mashabiki hawataki kukikubali kwa kuwa tunaishi katika kwa mazoea sana. Ugumu wa ligi hii hauko katika ubora wa kiwango cha uchezaji ila katika saikolojia ya kila timu kutokukubali kufungwa. Timu ziko tayari kukabana hadi shingo, kupiga viatu, kukamiana, kupoteza muda na kufanya kila lililo ndani ya uwezo kuhakikiksha inapata matokeo bila kujali ugumu wa mechi. Ni timu zinazoweza kuhimili pressure kwa ukomavu kama Yanga na Azam ndizo zinaweza kupata matokeo hata katika mazingira magumu wakati mwingine bila kujali zinachezaje. Simba si mojawapo ya timu hizo. Bado Simba inacheza mpira wake laini, pasi nyingi (sexy football) lakini inakosa plan B mambo yanapokuwa magumu.

Kwa kuhitimisha, sababu ya kwanza na ya pili iko ndani ya uwezo wa Simba na ni sababu kubwa zaidi zinazopelekea timu kupepesuka. Aveva na kamati yake wanaweza kuimaliza kabisa ndani ya miezi michache ijayo. Hii sababu ya tatu ni nje ya uwezo na kwa kweli ni changamoto kwa Simba na timu nyingine zinazofanya vibaya kujipanga kivingine ili kubaki ktk ushindani wa kweli.
 
Timu zetu zinavyoendeshwa ni vigumu kufanya tathmini. Tuchukuwe mfano wa Liverpool yaani hata darasani mtu anaweza akafundishwa mchakato uliotumika kujinasua matatizoni.
 
Yani Simba inaacha wachezaji wazur wanasajili magarasa, hatuna watu kama wakina Boban, Kazimoto, kiungo mshambuliaji hatuna tunamawinga tu, namba tisa ndio hatuna kabisa, yani unamchukua Serenkuma unamwacha Tambwe na mpira anaocheza.

Okwi, Serenkuma wote ni sawa ilikuwa na haja gani kujaza mawinga na kumwacha goal poacher mzuri kama Tambwe, leo hii tunabaki kumutegemea Maguli ambaye kwangu naona hatusaidi kwenye mashambulizi zaidi ya kufunga magoli ya kubahatisha

Kiukweli Tambwe alikuwa msumbufu kwa mabeki tofauti na Maguli hata zile kosakosa tu hamna yani bora hata yule dogo Ibrahm ajibu, simba inabdi watafute watu wasumbufu kama namba 8 ya Coast
 
Nimetumia neno wadau nikimaanisha wadau wote wa soka, mwenzenu wiki hii nimechanganyikiwa sana na hii Simba

Nini Kifanyike Jamani, hali hii imekuwa mbaya sana mwaka huu, hatujawahi kufurahi walau mara mbili mfululizo, tukifurahi inafuta sare au kipigo

maoni ya kujenga jamani si ya kubeza, nisije geuka yule shabioki wa Kenya
 
Pole kaka kwanza tulisema ukawa tukaja kusema kabulu sasa cjui niseme aveva maana anatuzingua timu inafanya mazoezi kahama mechi shinyanga
 
Tatizo la simba ni jeuri,namuunga mkono mheshimiwa pinda kwamba WAPIGWE TU
 
Tatizo ni mfumo mzima, kuanzia uongozi mpaka baadhi ya matawi yanayojiona yana sauti.

Wachezaji nao wawajibike, huwezi cheza kama juzi alafu ukajiita na wewe ni mchezaji. juzi nimeangalia mpira nikawa nasikitika, yaani Simba inacheza hata timu ya daraja la nne haichezi vile.

Tatizo ni mfumo mzima!

Uongozi, baadhi ya wanachama na pia wachezaji wenyewe!
 
nguvu moja wanasimba, huenda tusitarajie BRN mwaka huu
 
Uongozi wa Simba ni tatizo.Kwa nini wasisamehe yote yaliyopita na kusamehe wanachama wote ili tuwe. kitu kimoja?Simba sio timu ya kucheza ndondo ili. ipate hela ya mafuta ya gari na kulipia hoteli.Huu ni upuuzi uliopitiliza.AVEVA na wenzio mnaiua simba.
 
ajiuzuru wawapishe watu wenye uwezo mashabiki wa simba nao ni wahovyohovyo tu bado wanakaa kimya ngoja washuke daraja tuu tumewachoka aveva,kaburu tukeni humu nyie ndo tatizoo
 
Timu inasafiri siku ya mechi umbali wa kilometer 100 kutoka kahama mpaka shinyanga mjini.Sababu kubwa eti walienda kucheza ndondo ili wapate hela ya mafuta ya basi.Upuuzi mtupu huu!
 
Pole kaka kwanza tulisema ukawa tukaja kusema kabulu sasa cjui niseme aveva maana anatuzingua timu inafanya mazoezi kahama mechi shinyanga

Huyo sio kaka ni dada,tena ni mpenzi wangu,tutake radhi tafadhari sana kabla sijakushtaki kwa mods
 
Huyo sio kaka ni dada,tena ni mpenzi wangu,tutake radhi tafadhari sana kabla sijakushtaki kwa mods

yahoo.............watu hunichanganya.......toa mawazp bhana ya kujenga simba ili ikuchape machi 8
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…