Uchaguzi 2020 Tusifanye ushabiki kwenye uchaguzi, ni hatma yetu

Uchaguzi 2020 Tusifanye ushabiki kwenye uchaguzi, ni hatma yetu

Sister Abigail

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2020
Posts
2,886
Reaction score
9,088
Tusilete ushabiki kama ule wa SIMBA na YANGA linapokuja suala la uchaguzi, tukiitana majina sijui nyumbu sijui mataga, hii ni hatma yetu ni maamuzi kwa faida yetu ya kesho. Likitokea baya tutalibeba wenyewe, na likitokea zuri tutafaidika nalo wenyewe kama Watanzania. Huu sio Mpira tuseme wamemaliza fulani kafungwa, fulani kashinda bhasi maisha yataendelea.

Hapana huu ni uchaguzi wa kuamua tunataka tuishije huko mbele miaka mitano ijayo, hatma yetu kama Watanzania.

Kuna maisha baada ya uchaguzi, na maisha tunayotaka yataamuliwa na sisi wananchi kupitia sanduku la kura.

Ombo langu tuache mihemko,tutumie akilii kujua ni mgombea yupo atakaetufaa.

Hebu fikiri A anamdiss B kwenye jukwaa, ohh yule ni kibaraka katumwa kuja kuvuruga amani, atawavuruga atawaacha peke yenu, ila cha kushangaza sasa yeye huyohuyo anaejitapa mzalendo MTU wa amani anamshambulia kwa mabomu yule anaemtaja kuwa kama mvuruga amani, inaingia akilini kweli?

Mtu anaonesha dhahiri kabisa ni muonevu wa kila aina,bado mnamshangilia hizi ni akili au mihemko? Kama ameweza kuwaonea hao atashindwa kukuonea wewe?

SERIKALI NI MFUMO WA WATU, ULIOUNDWA NA WATU KWA AJILI YA WATU

Na watu hao ni sisi wanachi, Watanzania Sisi ndo tunaowapa dhamana ya kutuongoza,na sisi ndo wa kuamua tuongozwe na MTU wa aina gani?

Maamuzi yapo kwetu. Na maisha yatayokuja chini ya huyo tuliemchagua ni yetu, kama mnyanyasaji tutanyanyasika sie, kama muonevu tutaonewa sie, kama ni muuwaji tutauliwa sie, kama ni mdhulumu tutadhulumiwa sie, vitisho sisi, kuburuzwa na kutupwa gerezani sisi, kufilisiwa Mali zetu sisi, kutekwa sisi, kunyimwa ajira sisi, kuuliwa biashara zetu kimabavu sisi, kukatwa kodi kandamizi sisi.

Wakulima wataoteseka ni Watanzania
Wafanyabiashara ni Watanzania
Walimu ni Watanzania
Wafanyakazi ni Watanzania
Wanafunzi ni Watanzania

Sio Kenya, Uganda wala Burundi. Ni Tanzanians!

Uchaguzi huu ni maamuzi ya kutaka tuishije tena awamu ijayo. Tusiwe wepesi kutumia AKILI.

Tuache MIHEMKO tutumie AKILI kuchagua kilicho bora kwa faida yetu wenyewe!

Mungu Ibariki Tanzania.

Abigail Nabal
 
Wamebandika msikivu, mnyenyekevu. Ukosefu wa aibu na kuleta mzaha na mambo ya msingi. Siku mtanzania akijua maana halisi ya maendeleo ataona kiasi gani tumepoteza muda na rasilimali kwenye michezo ya kijinga
 
Hii nchi ni tajiri sana sana.
Hebu fikiri wanyama waliojaa huko maporini wote ni hela. Wanyama wa porini ni wengi kuliko idaidi ya binadam.
Samaki ni wengi kuliko binadam, Mlima unaingiza na mabonde yanaingiza tu madola kupitia utalii bila gharama yoyote wanaonufaika ni watawala na mawaziri wao na baraza hilo zima.

Hebu tutafakari madini yaliyojaa kila mahali ni hela tu hizo.
Hebu tafakari Gesi iliyojaa kwa mtrilion ya ujazo huko ardhini . Vyote hivyo tumejaliwa na Muumba wetu ili kila mwanadam apate riziki yake bila mateso. Watu waishi kwenye ardhi hii kwa raha na kustarehe.
Setani aliona wivu mwanadam kufurahia utajiri wa Muumba kwa uhuru. Mbinu ya Shetani ikawa ni kumtumikisha binadam ili asifurahie utajiri aliopewa na Mungu. Shetani ameleta watawala waovu wengi Duniani ili wawatese wanadam mpaka wamkufuru Mungu na kuona kuwa kila kitu ni kigumu mpaka makaratasi yanayoitwa hela yanawapa watu maisha magumu.

Hebu Fikiri utajiri wote huo unaishia kwenye kuendesha maisha ya watawala na familia zao. Watu wasiozidi 5000 wa na huko utajiri wa watu wote. Ukiona majumba ya kifahari kule mijini na mahoteli ya kifahari na magari ya kifahari yote wamiliki wake kwa asilimia kubwa ni walioitawala au wanaoitawala nchi hii. Wao na familia zao jambo LA muhimu kwao ni maisha yao lakini kwa watanzania wanawadanganya kuwa nyie vumilieni shida zenu zitatatuliwa na wajukuu wenu tukishajenga madaraja na viwanja vya ndege.

Tuwakatae mana hakuna sababu Tanzania kuendelea kuwabembeleza watu walioshiba na kulewa madaraka kwa kodi zetu kwa nusu karne.
Hata kila mtanzania akipewa Mali yake bado tutakwenda mbele. Yaani huyu apewe kipande cha Tanzanite ,mwingine dhahabu, Almasi, Miti pori apasue mbao . Mwingine Tembo auze Pembe zake baada ya kufa. Mwngine samaki,mwingine Mlima n.k. Ni utajiri wa kumtosha kila mtanzania. Tatizo CCM wameamua kuchota Mali zote na kujimbikizia bila kujali kuwa wengine nao wanatamani maisha bora sio kuona madaraja na mavitu ya kifahari kwa watawala tu.

Zanzibar palikua na dira nzuri wakati wa ASP kwa ajili ya kuwalipa wazee mishahara .
Leo miaka 50 mbele CCM haiwezi hata kuwalipa wafanyakazi wa SMZ sh.40000./

CCM ni tatizo mana inaomba kura ili iendelee kuitumia katiba iliyopo kuwakandamiza Watu na kuwafanyia jeuri na udhalimu kwani wana uhakika kuwa mwenyekiti wao ana nguvu kuliko Sheria zote na ktiba yoto
 
Hasante sana kwa mada hii, ifike wakati tuwe wapenzi wa maendeleo na ustawi wetu. Tuwe serious na ustawi wetu na si vyama wala wagombea flani. Tanzania ina kila sababu ya kumkataa Magufuli kuendelea kuoiongoza!.
Asante kwa kuliona hilo..
 
Back
Top Bottom