Tusijipunje kwa kutoshiriki sensa

Tusijipunje kwa kutoshiriki sensa

Rashda Zunde

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2022
Posts
204
Reaction score
231
Ni vyema kutambua kuwa suala la sensa ya watu na makazi halifanyiki kwa manufaa na maslahi ya chama, dini wala kabila bali linafanyika kuisaidia serikali kupanga mipango yenye tija kwa kila Mtanzania.

Ukirejea umuhimu wa sensa ya watu na makazi, sioni kama kuna sababu yoyote ya msingi itakayomfanya mtu asiweze kushiriki ama asiwe tayari kutoa taarifa zake na kama yupo basi huyo ni msaliti naye anapaswa kutafakari maamuzi yake kwa maslahi yake binafsi na ya nchi.

Ni lazima tujiweke tayari kuhesabiwa na ili tufanikishe hili ni vyema tukemee, tukatae na kukanusha taarifa zenye kutia doa na kizuizi ushiriki wetu katika sensa kwani kutoshiriki sensa ni mithili ya usaliti.

Hata Rais Samia Suluhu wakati akizindua rasmi nembo ya sensa ya mwaka 2022 aliwaomba Watanzania wote kujizatiti na kujiweka tayari kushiriki sensa.
 
... hivi siku ya sensa (23.08.2022) ni siku ya mapumziko kitaifa? Ili wananchi wengi kadiri inavyowezekana wabaki majumbani mwao kutoa taarifa zao na za familia zao?
 
Hapana sio siku ya mapumziko. Utahesabiwa pale ulipo.
... makarani wa sensa watatembelea maofisini, mashambani, viwandani, migodini, n.k? If so, good! Inabidi vituo vya sensa viwekwe barabara kuu na magari yasimamishwe abiria wahesabiwe; vivyo airports, n.k.
 
... makarani wa sensa watatembelea maofisini, mashambani, viwandani, migodini, n.k? If so, good! Inabidi vituo vya sensa viwekwe barabara kuu na magari yasimamishwe abiria wahesabiwe; vivyo airports, n.k.
Yeah. Makarani watatembea kila sehemu. Kwahiyo hata ofisini watafika
 
Mimi Niko tiyari kuhesabiwa, ila ole wenu mtumie no yangu kutengeneza data za huongo katika uchaguzi wa 2025 , msije sema sikutoa angalizo,
Ila tofauti na hilo Sina pingamizi .
 
Mimi Niko tiyari kuhesabiwa, ila ole wenu mtumie no yangu kutengeneza data za huongo katika uchaguzi wa 2025 , msije sema sikutoa angalizo,
Ila tofauti na hilo Sina pingamizi .
Hili haliwezi kufanyika. Usiwe na wasi wasi
 
Anwani za Makazi zenyewe nyumbani kwangu hata hawakupita,sidhani kama Sensa watakuja
 
Niliona kwenye TBC live kiongozi mmoja katumia zaidi ya lisaa kujiandikisha, nikapata wasi wasi na hiyo spidi
 
Back
Top Bottom