Tusimbebeshe sana lawama Gamond hata professor alifeli pamoja na uprofesa wake

changaule

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2020
Posts
6,039
Reaction score
10,151
Kuna mahali, Ihefu imeizidi Yanga hasa wanapocheza nao pale Highland estate.

Mechi ya jana ni kama marudio ya mechi ya msimu uliopita.

Tuliamini Nabi ni kocha bora, kocha mzuri sana aliyeifanya Yanga iwe unbeaten kwa michezo zaidi ya 40 lakini kaja kuumbuliwa na Ihefu na sherehe ya unbeaten ikaishia hapo.

Ukiangalia mechi ya msimu uliopita na msimu huu haijatofautiana matukio.


1) Nabi na Gamond wote walifelishwa kutokana uchaguzi wa wchezaji na bahati mbaya wote wawili wamewatumia Moloko, Mauya na Sureboy kwenye kikosi kinachoanza. Sijui ni mazingira gani yanayowasukuma kuwa kigugumizi cha kushindwa kujua mapungufu ya hao watu kwenye mechi ngumu ya away.
Gamond hakuwahi kumpa Mauya zaidi ya dakika 20 uwanjani na mara zote alikuwa ana muingiza dakika za lala salama, lakini jana anakuja kuingia mtego kwa kumuanini mchezaji ambaye haaminiki. Mbaya zaidi kawajaza wachezaji ambao waliokosa match fitness na waliokosa kujiamini kutokana na kutocheza mara kwa mara. Nadhani hata yeye akikaa kwa kutulia baada ya mechi anaweza akajikataa kama ni yeye kafanya jambo kama hilo. Lakini kwake halitakuwa wa kwanza kukosea, Nabi mbele ya sherehe za unbeaten kaumbuliwa na Ihefu na hakuna aliyeamini tena ni Nabi tuliyemuamini, Nabi tuliyemuimba, Nabi aliyebatizwa uprofesa kashindwa kusherekea sherehe ya unbeaten mbele ya Ihefu.

2) Magoli ya mapema zaidi kwa Yanga

Mechi ya msimu uliopita Yanga alipata goli la mapema kabisa dakika ya 9 tu huku mechi ya jana tena Yanga wanatangulia kupata goli la mapema kabisa dakika ya 3 tu .

3) Timu kuzidiwa na kukosa utulivu baada ya kupata goli.

Mwaka jana, Baada ya Bangala kuifungia goli, iliwaamsha Ihefu huku wachezaji wa Yanga wakianza kupoteana na kutoka mchezoni kwa kushindwa kucheza mpira wao uliozoeleka.

4) Aina ya magoli ya kusawazisha

Msimu uliopita Ihefu waliweza kusawazisha goli kupitia mpira wa kutengwa, jambo ambalo limekuja kujirudia kwenye mchezo wa jana.

5) Vurugu kutokana na kuhamaki.
Msimu uliopita benchi la ufundi la Yanga walihamaki na kusababisha rapsha za hapa na pale kama ilivyokuwa jana kwa benchi la ufundi la Yanga kulikuwa na fujo za hapa na pale na mashabiki nao wakasababisha vurugu.

Mashabiki wa mpira, mpira una mambo mengi nje na ndani ya uwanja tusiishie kunyosha vidole tu kwa Gamond lakini hatujui alikumbwa na mazingira ya namna gani kimaamuzi. Na pia tukumbuke Nabi pamoja na uprofesa wake na Mayele akiwa ndani ya uwanja walipoteza mechi. Mwisho ni kwamba uongozi wa Yanga na ufundi tutumie hii mechi kama funzo kwetu tusikosee tena kuzicheza hizi mechi hasa za mkoani japo kwa msimu uliopita tuliweza kwa asilimia kubwa hivyo tujifunze tulipokosea.
 
Nyie si mlikuwa mnajigamba kuwa mnakikosi kipana

Sasa kwanini upeleke lawama kwa wachezaji walioaminiwa na Kocha ambao nao ni sehemu ya kikosi kipana?

Sawa tufanye kwamba wale walioanza waliifelisha timu, lakini mbona hao wachezaji wenu mliotaka kuwaona wakianza nao waliingia second half.

Mbona hawakuweza kutumia ubora wao kuoata matokeo ili kuonesha utofauti kati ya wao na hao walioanza kipindi cha kwanza?

Yanga kwa Ihefu huwa haijawahi kuwa na game nyepesi.

Hata ile game yenu ya second leg hapa kwa Mkapa mlipata goli moja kwa shida sana. Na wakati huo mliita mechi ya kisasi mkafanya maandalizi kem kem kuhakikisha mnapata ushindi mkubwa.

Your browser is not able to display this video.
 
UMEFANYA ANALYSISI NZURI MNO..

shida ni pale Mimi kusikia Unamwita NABI Professa unanishangaza sana mkuu..

1. Uprofesa WA Darasani si Lelemama

2. Mimi kijana Mdogo kabisa ninahangaika Na PhD hatari.
Hadi MACHOZI yananitoka

3. Nabi Hana Hata Certificate Ya Human Resource unamwita Prof for what........

4. Ama ana Kitu Gani Cha Ajabu amewahi kukifanya Tanzania???????

Shame....
 
Wapi umesikia Gamond amebebeshwa lawama
 
Unaweza kuwa na point, Ila kinachonishangaza ni madai ya wanayanga wengi kocha alipanga wachezaji wasiokuwa fit. Hivi kocha anayekaa na wachezaji kambini na mashabiki wanaowaona wachezaji kwenye mechi Nani anajua fitness ya wachezaji.
 
Una uhakika kile kikosi cha Jana kapanga Gamondi?
 
Una uhakika kile kikosi cha Jana kapanga Gamondi?
Mimi navyojua kocha ndiye anayepanga kikosi, kama wewe unamjua mtu mwingine aliyepanga kikosi ukiachana na kocha basi nijuze, kikosi kimepangwa na nani?
 
Unaweza kuwa na point, Ila kinachonishangaza ni madai ya wanayanga wengi kocha alipanga wachezaji wasiokuwa fit. Hivi kocha anayekaa na wachezaji kambini na mashabiki wanaowaona wachezaji kwenye mechi Nani anajua fitness ya wachezaji.
Ufiti ni nini?
Ni utimamu wa kiakili na kimwili, nadhani hata wewe unafahamu ya kwamba mchezaji asipopewa nafasi ya kucheza mara kwa mara inampunguzia fitness na hali ya kujiamini. Kibwana, Skudu, Mauya, na Sureboy ni moja wa waathirika wa hiyo hali.
 
Hilo jina kapewa na wadau wa mpira wa miguu, hizo ni nickname tu ila ajabu unachukulia serious hadi kwenye nickname wanazopeana watu.
 
Kumtetea kocha bado hakuwezi kumuepusha na lawama. Maana yeye ndiye anayehusika na upangaji wa kikosi! Na kama anapangiwa kikosi cha kucheza kwenye mechi, basi atuambie mapema.

Asisubiri mpaka aondoke ndiyo akalalamike kwenye vyombo vya habari vya kwao, kama alivyofanya yule kocha wa Singida Fountain Gate! Raia wa Afrika ya Kusini.

Kimsingi kikosi kilichoanzishwa kipindi cha kwanza kwenye ile mechi kilikuwa ni dhaifu kupitiliza. Na kwa upande wangu nilikigundua mapema tu hata kabla ya mchezo kuanza. Na mpaka sasa bado sijajua sababu hasa ya kupanga kikosi cha aina ile ilikuwa ni ipi hasa, na katika mechi ngumu ya ugenini kama ile.


Yaani uwaache wachezaji tegemeo nje, halafu uwaanzishe wachezaji unaowapa dakika chache tu za kucheza kwenye mechi zako zote zilizopita! Ile ilikuwa ni akili, au matope!
 
Kocha ajua kwa nini alipanga vile, anawajua wachezaji zaidi kuliko sisi huku mitaani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…