Tusimwonee pekee huyu Mchezaji Banka kwa kuhukumiwa kwa Kuvuta Bangi kwani 98% ya Wachezaji wa Tanzania ni Wavutaji Bangi

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Ni kweli kwamba Mchezaji Mohamed Banka kutokea Zanzibar ambaye amesajiliwa na Yanga SC amehukumiwa Kifungo cha miaka miwili kwa Kosa la Kutumia dawa za Kulevya aina ya Bangi / Bange. Sitaki kumtetea na katika hili naweka pembeni Usimba wangu ( ambao kila Mtu anaujua humu ) ila ninachowaomba Wanamichezo wenzangu ni kwamba kupitia huyu Mchezaji basi tuweze pia kuwasaidia Wachezaji wengine wenye hii tabia waweze kubadilika.

Binafsi tokea niwe Mchezaji wa Mpira kwa ngazi ya Shule ya Msingi, Upili na kidogo Chuo Kikuu nimeweza kushuhudia Wachezaji wenzangu wengi tu wakiwa wanavuta Bangi tena tukiwa Kambini kabisa. Hivyo tatizo hili ni la Mzizi mrefu na Jamii ya Wanamichezo inatakiwa ishirikiane ili kulimaliza kama siyo kulikabili.

Kwa Tasnia yangu na tabia yangu ya Kupenda Kujichanganya sana na Watu wa kila Kada na Kila rika nisifiche hapa nina Wachezaji tena ' Waandamizi ' kabisa wa Vilabu vya Simba, Yanga, Mtibwa Sugar na Azam FC ambao kwa bahati nzuri ni Marafiki zangu wazuri tu na wakubwa lakini nadhani kama kuna siku ambayo watakuja kuacha Kuvuta Bangi / Bange basi labda ni pale tu Wakifa kama siyo Kufariki.

Sema tu ni bahati mbaya sana hili ' Zigo la Lawama ' limemwangukia huyu Mchezaji mdogo wangu Mohamed Banka lakini Kaka zake wengi ( namaanisha Wachezaji Waandamizi ) wanavuta mno Bangi / Bange. Kuna Mchezaji mmoja ( namuhifadhi ) alikuwa anachezea Klabu yangu ya Simba anaishi Kimara hata muda huu ukienda Nyumbani Kwake utawakuta Wachezaji wengi Waandamizi wakiwa wanavuta nae Bange / Bangi.

Kuna Mchezaji mwingine nae ni Rafiki yangu mzuri tu anachezea Yanga SC huyu Yeye iwe ni Mazoezini au katika Mechi asipoletewa Bangi / Bange na Viongozi wake anaweza hata akasusa Kucheza hivyo Klabu huweka kabisa Bajeti yake ya Kumnunulia hicho Kilevi na huwa hachezi bila kuonyeshwa ama Kadi ya Njano au Nyekundu a.k.a Umeme.

Kuna Mchezaji mmoja tena Mwandamizi kabisa wa Simba SC ambaye ' Maskani ' yake kubwa ni Kawe karibu na Baa maarufu ya Maasai ana Urafiki na Mchezaji mmoja Mwandamizi wa Mtibwa Sugar ambaye Kaka yake alipigwa Risasi njia panda ya Kawe na Mtawala mmoja ambaye nae alikufa baadae. Huyu Mchezaji wa Simba SC Bange / Bangi zake zote anazipatia hapo hapo Kijiwe chao cha Kawe na ndiyo amemuharibu sasa na Mchezaji mwenzake mgeni ambaye alianza Kukubalika mno katika nafasi ya Beki wa Kati lakini baada ya ' Kuonjeshwa ' tu hicho Kilevi sasa hata Kiwango chake Kimeshuka.

Nina mifano mingi na hunidanganyi kitu kuhusu Wachezaji wa Tanzania na matumizi yao ya Bangi / Bange na hapa wala hawa Viongozi wa hivi Vilabu wasiwadanganye kuwa hawajui kwani wao ndiyo huwaagizia na wapo pia hadi Viongozi na Makocha wa hivyo Vilabu nao ni Wadau / Watumiaji wazuri tu wa Bange / Bangi.

Namalizia tu kwa kusema tuache Kumsakama huyu Mchezaji Mohamed Banka kwakuwa tu ameonekana Yeye bali tumsaidie Kisaikolojia ili aweze Kubadilika kusudi basi na Wachezaji wengine kupitia Yeye waweze Kubadilika na hatimaye kulitatua hili tatizo. Na kinachoniuma na kunikera ni kwamba kuna hadi Watangazaji na Waandishi wa Habari za Michezo nchini ambao ' personally ' kabisa nawajua kuwa ni Wavutaji wazuri wa hiyo hiyo Bange / Bangi lakini na wao leo hii wanajifanya ' Kumshambulia ' huyu Kijana wa Watu kana kwamba Yeye ndiyo mkosaji pekee wa hili Sakata.

Nawasilisha.
 
Kakamatwa na kilo ngapi za bangi?

Jifunze jinsi ya ' Kuposti ' hapa JF kwani ' Kuposti ' kitu kimoja na hicho hicho zaidi ya mara tatu kinaonyesha ni jinsi gani si tu kwamba una Upumbavu / Upopoma uliotukuka bali pia una ' Ukichaa ' wa Kiwango cha Kimataifa ambacho pia kina kinahitaji Madaktari wa Kimataifa kuweza Kukusadia ili angalau uweze kupona kidogo kwani kupona kabisa itashindikana.
 
Watanzania wengi wetu ni watu wa ovyo sana. Wavivu, Hatuna umakini kwenye kazi, Kuendekazi starehe mbele kuloko kazi, Bidii kwenye utafutaji ni mdogo. Halafu mwisho tunaishia choyo kwa wengine.
Ni aibu kabisa mpaka wenzetu kenya, Uganda, Congo, wachezaji wanafika mbali. Ukenda france, Belgium, England, Qatar,U.A.E, Sweden, Denmark, Waafrika kibao. Lakini mbongo humuoni.
 
Ni nyuzi chache ktk jukwaa la michezo ambazo huwa hazina chembechembe za ushabiki na mahaba niue. Huu ni mmojawapo
 
Ni kweli kabisa Mkuu
Kwanza, nimependa uwasilishaji wako uliojaa hekima na ulinganifu wa matatizo yaliyopo ktk jamii ya wana michezo pasina kujali we ni mpenzi wa timu gani bali kwa kuijali jamii nzima

Pili, umelielezea tatizo ktk uzito wake na kulifikisha kwa jamii tena kwa kutoa mifano isiyo na shaka ndani yake

Mwisho ni jukumu letu sote wanamichezo na jamii kwa ujumla kuliangalia hili tatizo katika muktadha wa kuwasaidia waathirika wa hiki kilevi (bangi). Kuna haja hata TFF kuwasaidia wanamichezo walioshikwa na tatizo hili kwa kuwafanyia "counselling" kupitia kwa madaktari na wataalam wa afya ya akili ikiwa wapo magerezani au hata wanapoitwa ktk timu ya Taifa na kuanzisha dawati huru la ushauri nasaha juu ya matumizi ya vilevi na dawa za kusisimua misuli (kama dawati la ushauri nasaha lipo TFF basi liwezeshwe zaidi)
 
Banka amekula nyundo 2.. pole yake ajifunze kutokana na kosa.
Player wengi wanalamba moshi.. Nafikiri wengine wakae chonjo msako unakuja.
 
jamaa anakipaji kikubwa mno, kama bangi zinamsaidia kumaintain kiwango chake basi tumuache, maana ni private life

Kwa mchezaji sio private life ni lazima wachezaji wapimwe vilevi na dawa za kuongeza nguvu kila baada ya kucheza mechi, inaonekana kwenye ligi yetu hakuna huu utaratibu na sitoshangaa kukawa na wachezaji wanaotumia dawa za kuongeza kwenye mechi.
 

Haya Mamlaka Ya Kuwasemea Wengine Kakupa Nani????

Si ujisemee Wewe Mwenyewe tu Kuwa Ni Mtu Wa Ovyo Sana! Hata Huu Uandishi Wako Unaonesha Kuwa Ni Mtu Wa Aina Gani.
 
Haya Mamlaka Ya Kuwasemea Wengine Kakupa Nani????

Si ujisemee Wewe Mwenyewe tu Kuwa Ni Mtu Wa Ovyo Sana! Hata Huu Uandishi Wako Unaonesha Kuwa Ni Mtu Wa Aina Gani.

Unaonekanwa ni mshabiki wa Yanga.
Poleni sana.
 
Kwa mchezaji sio private life ni lazima wachezaji wapimwe vilevi na dawa za kuongeza nguvu kila baada ya kucheza mechi, inaonekana kwenye ligi yetu hakuna huu utaratibu na sitoshangaa kukawa na wachezaji wanaotumia dawa za kuongeza kwenye mechi.
Ni kweli mkuu upo sahihi....lakini miundombinu mibovu ya soka letu inafanya issue kama hizi ziwe private life.... since boban miaka ile hadi leo no action zinachukuliwa......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…