Tusioshabikia Simba wala Yanga tukutane hapa

Mtoto wa Jadu

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2018
Posts
419
Reaction score
1,020
Tukiachana na muziki, burudani inayofuatiwa kwa kupendwa na wengi ni mpira!

Lakini imekuwa bahati mbaya kwa mpira wa hapa nyumbani, umebebwa na timu mbili tu za Simba na Yanga.

Hali imekuwa mbaya sana katika ushabiki wa timu hizi, umevuka mipaka, umeingia mpaka sehemu rasmi kabisa kama vile kwenye majumba ya ibada, na hata siasani huko bungeni. Watu ni kuzungumzia simba na yanga tu

Ni mara kadhaa sasa nimeashuhudia, ushabiki wa simba na yanga ukihusishwa katika maeneo kadhaa.

Sikuhizi, aghalabu kwenye sendoff na sherehe kama hizo, unakuta watu wanaleta zawadi zao katika mtindo wa usimba na uyanga!!
Jambo hilo sio wote tunalifurahia!!

Sasa, inapotokea mechi baina ya hizo timu, stori mitaani inakuwa ni hiyohiyo, nothing else!!

Kibaya zaidi, timu hizo zinapambwa na maneno mengi sana kuliko uhalisia... Yaani mashabiki wao wamekuwa waongeaji sana, kutetea timu zao, ilhali hata hazitufaidishi na chochote kama taifa.

Hakuna maendeleo kisoka tunayoyapiga kutokana na simba na yanga, japo ukiwasikiliza wenye timu, wanaweza hata wakakumeza [emoji28]

Karibuni muongezee.. [emoji116]
 
Wewe kama sio shabiki wa hizi timu hayo yanaondelea juu ya hizo timu yanakuumiza nini?, Unawezaje kufuatilia jambo usilolipenda?.
 
Duh! Sometimes it's true
 
Timu imesajili inalipa mishahara halafu wanakaa na kujadili wawashe moto katikati ya uwanja kabla ya mechi. Mara sijui basi liingie kinyume nyume . Mara timu inaingia uwanjani bila kupita geti rasmi. Zinafanya mambo kama vile ni timu za madaraja ya chini.Timu za hovyo hizi.
 
Yaani zinaliaibisha sana taifa... Basi bora hata zingekuwa na manufaa kitaifa, lakini wapi...

Kwa ukubwa wa timu hizo angalau hata zingekuwa na viwanja vyao, lakini hola...

Maneno yanakuwa mengi sana kuliko uhalisia!! Hovyooo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…