Tusipokataa wabunge kujazana kwenye Bunge Maalum la Katiba tumekwisha

Tusipokataa wabunge kujazana kwenye Bunge Maalum la Katiba tumekwisha

Nikupateje

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2009
Posts
1,334
Reaction score
989
Inaelekea draft ya katiba imetupotosha na kusahau jambo la msingi kuliko yote. Moja ya mambo ambayo yalifanya vyama vya upinzani kutaka kugomea process ya katiba mpya ni kubadilishwa kwa sheria inayotaja compsition ya wajumbe wa bunge la katiba au Bunge Maalum.

Tunafahamu kwamba Bunge lilijitungia Sheria hii na kujichagua lenyewe liwe mjumbe wa Bunge la Katiba yaani wabunge wote wa sasa na wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wawe wajumbe wa bunge hili.

Kwa maana hiyo Bunge la Katiba litakuwa na zaidi ya asilimia 66 (absolute majority) ya wabunge wa CCM na hivyo itakuwa katiba ya CCM.

Tunavyojua wabunge wa Bunge la Jamhuri hawakuchaguliwa ili kutunga katiba bali walichaguliw ili kutunga sheria za kawaida.

Hoja hii haikuweza kupingika na hata Waziri Mkuu mwanzoni mwa kikao hiki cha bajeti March 2013, alisihi vyama hasa Chadema kisijitoe bali sheria ya marekebisho italetwa bungeni kabla ya kuisha kikao hiki cha Bajeti ili tujue ni akina nani wataingia kwenye bunge la katiba.

Hivyo, Chadema na vyama havikujitoa vikaahidi kusubiri kuisha kwa bunge hili la bajeti ili tuone serikali italeta vipi huo muswada wa kurekebisha watakaoingia kwenye Bunge Maalum la Katiba.

Sasa bajeti ya serikali imepitishwa. Kilichobaki na kinachoendelea sasa ni miswada ya kadhaa.

Kwa kelele zote zile za mwanzo nilitegemea sasa hivi kila mmoja wetu apige kelele kuwa sasa ni wakati muafaka wa kuona ni vipi serikali inapeleka muswada kurekebisha composition ya bunge la katiba ili kusiwe na kundi lenye majority na eventually likawa kama ndiyo decison maker inapofika kupiga kura.

Inaeleka kila mmoja hata wasomi wanaolielewa jambo hili kana kwamba kutolewa kwa rasimu ya katiba kumewafumba macho hadi wasiweze kuona jambo hili.

Hata Kitila Mkumbo nimeona maoni yake kwenye gazeti moja akilalamika kwamba wingi wa CCM kwenye bunge la Katiba unaweza kuwa kiwazo ikawa katiba ya CCM na si ya wananchi.

Kauli kama hizi ni za kukata tamaa maana ni kama vile mahesabu yalipigwa kwamba ikitoka rasimu basi kila mmoja atajikita kwenye rasimu na tutasahau kudai sheria ya kubadili wingi wa wabunge kwenye bunge la katiba.

Kama ni mahesabu yalipigwa basi inaelekea yanafaulu maana hakuna sasa anayechangamkia hii topic ya Bunge la katiba na hivyo wanaofaidika na kuzubaa kwetu wanachekelea na wanaweza kuudhika na thread kama hii kwa sababu ninakumbusha kisichotakiwa kukumbushwa kwani ukimuamsha aliyelala utalala wewe.

Kikubwa ni kwamba Waziri Mkuu kwa mdomo wake bungeni aliahidi kuleta muswada kama nilivyosema. Sasa, haina maana kupiga kelele kuhusu uzuri au ubovu wa rasimu wakati tunaacha kupiga kelele kuhusu mabadiliko ya sheria wakati rasimu hata ikiwa nzuri vipi, wakijazana wabunge mle kwenye Bunge la Katiba wote tunajua yatafanyika yaleyale ambayo hufanyika Dodoma.

Wataulizana kifungu hiki cha kutokuwa na Serikali ya Tanganyika kinaafikiwa? Watajibu Ndiyooooooooooooooooo. Sasa usiyetaka utafanya nini

Mwisho katiba ikikaa kama wanavyotaka wao wataulizwa na Spika wao hivi: Sasa nitawauliza, wanaoafiki waseme ndiyo. Utasikia wengi wenye chama chao wakijibu Ndiyooooooooooooooooo. Watauliza wasioafiki wasema siyo. Watajibu Siooooooooooooooooo.

Mnajua akitakachotokea. Spika wa Bunge hilo atasema, nadhani walioafiki wameshinda. Huo ndiyo unakuwa mwisho wa mchezo, tunasubiri tu referendum!

Msiojua kinachokuja hivi ndivyo itakavyokuwa. Hivyo tusiposhinikiza muswada uletwe bungeni kama ilivyoahidiwa naWaziri Mkuu, basi tujue sisi wenyewe tutakuwa tumebariki iwe hivyo wanavyotaka waliotaka wakati kwenye ilani yao ya uchaguzi 2010 hawakuwa na kipengele cha Katiba mpya.

Kazi kwetu, kusuka au kunyoa. Binafsi najisikia huru kutoa hili moyoni kama kukumbushia.

Wenu Nikupateje
 
hii katiba ni ya watanzania siyo ya ccm wakipitisha upuuzi atutaweza piga kura
 
mtoa mada usichanganye mada, bunge la katiba ni tofauti na hili la sasa, yaani si kila mbunge eti kwa vile ni mbunge ataruhusiwa kuingia!

kifupi ni la watu maalumu, tena kwa muda maalumu tu!
 
mtoa mada usichanganye mada, bunge la katiba ni tofauti na hili la sasa, yaani si kila mbunge eti kwa vile ni mbunge ataruhusiwa kuingia!

kifupi ni la watu maalumu, tena kwa muda maalumu tu!

Sawa. Swali ni kwamba hao watu maalum wanapatikanaje?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
It's too late now...mmekubali mchakato kubalini na matokeo

Mwanakijiji inaelekea hili hujalielewa kabisa. Suala si mchakato.

Serikali haikusema kuwa hii si hoja bali yenyewe ilikiri kwamba haiwekzekani compsition ya Bunge Maalum ikabaki hivihivi na hivyo inaleta muswada kubadili watakaoingia bunge hilo.

Shida yangu ni kwamba inaelekea wamefanikiwa kutusahaulisha na wangetaka tukae kimya na inalekea wameshaanza kufanikiwa kuwapata mtu kama wewe ambay kamwe hutataja hata nukta ya neno kuhusu ahadi hii ya serikali.
 
mtoa mada usichanganye mada, bunge la katiba ni tofauti na hili la sasa, yaani si kila mbunge eti kwa vile ni mbunge ataruhusiwa kuingia!

kifupi ni la watu maalumu, tena kwa muda maalumu tu!

Wewe ndiyo huna maana kabisa na hujiu ni kwa nini Chadema walitoka nje siku sheria ile inapitishwa ikitaja kuwemo wabunge wote kuingia Bunge la Katiba.

Tukiwa na wakurupukaji kama wewe ndiyo hasa hawa mabwana wangependa.
 
mtoa mada usichanganye mada, bunge la katiba ni tofauti na hili la sasa, yaani si kila mbunge eti kwa vile ni mbunge ataruhusiwa kuingia!

kifupi ni la watu maalumu, tena kwa muda maalumu tu!

ndugu wewe ndo huelewi rudi uisome sheria ya mabadiliko ya katiba vema, wabunge wa sasa na wale wajumbe wa BLW wanaingia moja kwa moja kwenye hilo bunge maalumu la katiba, mtoa hoja kaja na hoja nzito sana kuwa kama wabunge wenyewe ndio hawa, tutegemee nini katika bunge hilo la katiba?
 
Wewe ndiyo huna maana kabisa na hujiu ni kwa nini Chadema walitoka nje siku sheria ile inapitishwa ikitaja kuwemo wabunge wote kuingia Bunge la Katiba.

Tukiwa na wakurupukaji kama wewe ndiyo hasa hawa mabwana wangependa.

aisee kumbe hizi ndo approach za huku siasani!!! ungeeleza kivingine bila kutumia hayo maneno kwa red nadhani maana isingebadilika
 
ndugu wewe ndo huelewi rudi uisome sheria ya mabadiliko ya katiba vema, wabunge wa sasa na wale wajumbe wa BLW wanaingia moja kwa moja kwenye hilo bunge maalumu la katiba, mtoa hoja kaja na hoja nzito sana kuwa kama wabunge wenyewe ndio hawa, tutegemee nini katika bunge hilo la katiba?

hiyo hoja ilishapigiwa kelele na public siku nyingi sana na serikali ikakubali kuleta mswada wa kukibadili. Shida ni kwamba tumekuwa proactive mno kiasi cha kupoteza mwelekeo. Kama ulikuwa unafuatilia vizuri umeona baadhi ya watu walivyokuwa wanapoteza imani na tume ya warioba for no concrete reason, matokeo yake midomo yote kimya!!
 
hiyo hoja ilishapigiwa kelele na public siku nyingi sana na serikali ikakubali kuleta mswada wa kukibadili. Shida ni kwamba tumekuwa proactive mno kiasi cha kupoteza mwelekeo. Kama ulikuwa unafuatilia vizuri umeona baadhi ya watu walivyokuwa wanapoteza imani na tume ya warioba for no concrete reason, matokeo yake midomo yote kimya!!

Muswada uko wapi na bunge linamalizika wiki hii?
 
Muswada uko wapi na bunge linamalizika wiki hii?

[h=2]New draft Constitution up for House debate come August[/h]


By Guardian on sunday correspondent



30th June 2013






The new Constitution making process may take a new shape at the next Parliamentary session in August when two Bills are slated for First Reading, both of which relate to the process.
The Bills are the Constitutional Review (Amendment) Bill, 2013 and the Referendum Bill, 2013 – both of which are expected to be tabled for debate before the House at the August session which normally takes two weeks, beginning August 27 in Dodoma.
Departure from the current two-government system to the proposed three-tier system of governance remains contentious even now, and these issues are likely to kick off spirited debate in the House later this year.
Some Members of Parliament from the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) in Zanzibar who spoke to The Guardian on Sunday in Dodoma expressed fears that Zanzibar could disintegrate should the three-tier government system be adopted.
They said if the proposals pass unopposed at two critical stages -- the Constituent Assembly and Referendum process -- Pemba and Unguja may not remain together as they are today.
The outcome of deliberations on the two constitutional review Bills would then pave the way for the proposed Constituent Assembly and the Referendum process. The Constituent Assembly will be held before the turn of year 2013 whereas the Referendum will be conducted in February 2014.
The new Constitution is expected to be inaugurated on April 26, next year when Tanzania would be marking her 50 years of Union between Tanganyika and Zanzibar, the government says.
The Constitutional Review Commission (CRC) headed by retired Judge Joseph Warioba has already issued the first Draft Constitution.
However, Judge Warioba has several times defended the proposal, saying given the current state of Tanzania politics it was worth going for the three-government system.
Two more Bills that won't fall under the ambit of the constitutional making process -- The GEPF Retirement Benefit Fund Bill, 2013 and the Statistics Bill, 2013 – will also be tabled for debate this August.



SOURCE: GUARDIAN ON SUNDAY
 
New draft Constitution up for House debate come August




By Guardian on sunday correspondent



30th June 2013






The new Constitution making process may take a new shape at the next Parliamentary session in August when two Bills are slated for First Reading, both of which relate to the process.
The Bills are the Constitutional Review (Amendment) Bill, 2013 and the Referendum Bill, 2013 – both of which are expected to be tabled for debate before the House at the August session which normally takes two weeks, beginning August 27 in Dodoma.
Departure from the current two-government system to the proposed three-tier system of governance remains contentious even now, and these issues are likely to kick off spirited debate in the House later this year.
Some Members of Parliament from the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) in Zanzibar who spoke to The Guardian on Sunday in Dodoma expressed fears that Zanzibar could disintegrate should the three-tier government system be adopted.
They said if the proposals pass unopposed at two critical stages -- the Constituent Assembly and Referendum process -- Pemba and Unguja may not remain together as they are today.
The outcome of deliberations on the two constitutional review Bills would then pave the way for the proposed Constituent Assembly and the Referendum process. The Constituent Assembly will be held before the turn of year 2013 whereas the Referendum will be conducted in February 2014.
The new Constitution is expected to be inaugurated on April 26, next year when Tanzania would be marking her 50 years of Union between Tanganyika and Zanzibar, the government says.
The Constitutional Review Commission (CRC) headed by retired Judge Joseph Warioba has already issued the first Draft Constitution.
However, Judge Warioba has several times defended the proposal, saying given the current state of Tanzania politics it was worth going for the three-government system.
Two more Bills that won't fall under the ambit of the constitutional making process -- The GEPF Retirement Benefit Fund Bill, 2013 and the Statistics Bill, 2013 – will also be tabled for debate this August.



SOURCE: GUARDIAN ON SUNDAY

Mkuu,

Now we are talking.
 
Back
Top Bottom