Tusisahau: Tanzania ni kubwa kuliko Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda ukiziweka pamoja

Tusisahau: Tanzania ni kubwa kuliko Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda ukiziweka pamoja

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Tunakumbushana tu kuwa Tanzania ina eneo kubwa kuzipita Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tukiziweka pamoja

Tutumie fursa ya ukubwa wa eneo letu kulead uchumi wa Afrika ya mashariki, pamoja tutaweza.

AM.jpg
Kazi Iendelee!
 
Kuna mijitu mioga humu mpaka unaionea hutuma,tutaogopa Hadi lini? Wakenya kwa sasa wanatuhofia Sana speed yetu inawatisha lakini sisi hatutaki kujiamini kwa makisudi tu hatutaki kujitambua kuwa tumekuwa tunapaswa tutoke tukapambane.

Samia tichukue utupeleke angani na UTUACHIE, Mwenye kupaa apae mzembe afiche mbawa zake mwache adondoke.
 
Tupo karibu sawa na Nigeria ambapo tumewazidi kidogo sana.

Nigeria kwa uwingi wa watu ni mara 3 na ushee zaidi yetu. Kupata ardhi ya kujenga ni mtiti haswa na wengi wa maisha ya kati wanakimbilia kujenga kwenye asili yao na kununua flats miji mikubwa kama Abuja na Lagos.

Lengo ni kusema, zile nchi 5 za EA haswa, nne zilikuwa na lengo moja la kuiteka ardhi ya TZ kwa manufaa yao. Mu7 akiwa m/kiti kwa kushirikiana na PK sio! Kenya wao wakiwa jeshi la mtu mmoja. Sasa wamewatamanisha na akina Burundi, Sudan na hata Malawi naye kaanza kututolea macho.

Sasa hawa wote kwa ujumla wao, wakifunguliwa milango, nini kitatokea? Ni kama tunavyoona sasa, koti limeshaanza kubana, ila wanasema tumeshaingiliana sana, itakuaje tukimwagana? Ingawa ukweli ni kuwa TUMEINGILIWA sana, si wanamiliki ardhi na kila kitu huku, vipi sisi kumiliki kitu kule?

Ndo yanayoenda kutokea, Wakenya watamiliki ardhi na kila kitu huku wakiwaambia hamruhusiwi kumiliki chochote kule, wale wasomi na wenye ujuaji mwingi waendelee tu kutuelewesha KWANINI HATURUHUSIWI KUMILIKI ARDHI HAPO ZNZ ila iwe rahisi kumili KENYA?
 
Hoja yako ndugu ni nzuri kwenye suala LA uchumi ila sikubaliani kama eneo LA nchi yetu ni kama ulivyo lielezea hapo juu.
Wajuvi wa mambo waje tusaidiane kujua ukubwa wa kila Taifa tajwa hapo juu.
Duh nimeingia chimbo ngoja tuone

Tanzania Km² 945,000
Kenya Km² 580,000
Uganda Km² 241,000
Burundi Km² 28,000
Rwanda Km² 26,000

Aiseee mama Tanzania is massive
 
Its true Tanzania makes 51% of the old East Africa Community (without south sudan)
Hoja yako ndugu ni nzuri kwenye suala LA uchumi ila sikubaliani kama eneo LA nchi yetu ni kama ulivyo lielezea hapo juu.
Wajuvi wa mambo waje tusaidiane kujua ukubwa wa kila Taifa tajwa hapo juu.ts
 
Hoja yako ndugu ni nzuri kwenye suala LA uchumi ila sikubaliani kama eneo LA nchi yetu ni kama ulivyo lielezea hapo juu.
Wajuvi wa mambo waje tusaidiane kujua ukubwa wa kila Taifa tajwa hapo juu.
Musukuma ndo kaandika kiongoz na elimu yake si siri
 
Nashangaa sana mama yetu kaenda hapo Kenya kufungua ukurasa mpya wa kiuchumi ila watu hoi kwa woga ooh tutaibiwa sijui nn na nn. Tutaendeleaje kwa woga wakijinga hvyo
Kuna kitu wewe na watu wengi mnadhani ndiyo silver bullet ya matatizo yetu. Nyie mnadhani solution ni kuita wawekezaji kwa wingi. Hili mimi sikubaliani nalo hata kidogo.

Siyo kama sitaki waje ila nachotaka kusema ni kuwa nchi inajengwa na wananchi wake. Sehemu nzuri sana ambayo tungeweza kuanzia ni kilimo. Kwa kuwa tuna ardhi, maji na hali ya hewa nzuri sana tukiamua kukifanya kilimo ndicho kiwe kipaumbele chetu tutafika mbali.

Mtu kama mchina ukimkaribisha anakuja lakini anakuja na makandokando mengi sana. Tusipokuwa makini miaka ijayo itakuja kutokea vita ya kuikomboa nchi yetu.
 
Tunakumbushana tu kuwa Tanzania ina eneo kubwa kuzipita Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tukiziweka pamoja

Tutumie fursa ya ukubwa wa eneo letu kulead uchumi wa Afrika ya mashariki, pamoja tutaweza.

Kazi Iendelee!
Kama wenyewe tumeshindwa hats kutumia fursa hiyo kibiashara kilimo,ufugaji nk.
 
Kuna kitu wewe na watu wengi mnadhani ndiyo silver bullet ya matatizo yetu. Nyie mnadhani solution ni kuita wawekezaji kwa wingi. Hili mimi sikubaliani nalo hata kidogo...
Miaka 60 hatjjaweza tujekuweza leo,huo utakuwa ni wivu na roho mbaya kisa wenyewe tumekuwa wazembe na wavivu.
 
Kiswahili huzaa uswahili

Aliyetuletea Lugha hii ya Kiswahili, ndiyo kasababisha haya yote,

Tanzania hatujafikia na hatuna sababu ya kusema eti nchi Yetu fursa hakuna, nchi Yetu inakubali kila utachowekeza, Kwenye kilimo, tunagusagusa tu, kwenye madini ndio kabisaa, wawekezaji na wanafahamika zaidi Kwa uwekezaji wa madini, ni wale wezi wa madini Yetu,

Tukiweza Sisi wenyewe tutalifanya Taifa letu kuwa Bora zaidi, mjenzi wa nchi ni mwananchi mwenyewe, hao wa kuja kuwekeza, ni wanakuja kuuolezea tu kidogo lakini mambo yote mengi ni Sisi Watanzania wenyewe
 
Eneo kubwa ! Ila CCM walitengeneza mfumo wa elimu ambayo utawadumaza watanzania kutofikiri nje ya box na...

Nchi ikishakua kubwa inatusaidia nini kama resources haziwanufishi wote zaidi ya familia,koo, vikundi vya watu wachache?

CCM naamini mtaji wao mkubwa ni watanzania wengi walio wajinga na ndio wanachopenda na kufurahia sababu hawa hakuna kuhoji, wala kudai haki na hata wakipewa haki wanaona kama hisani awamu iliyopita walibatizwa jina la "wanyonge".

Hao wanyonge waliamini katika umasikini wao na wakitaka kila mtu alingane nao walifurahi watu wakifukuzwa kazi bila taratibu za kiutumishi.

Mwisho niseme tu kupitia hili watanzania wengi hawana uthubutu wengi wanapenda kukaa kwenye comfort zone! Nakumbuka miaka 19 iliyopita nilipopata fursa adhimu ya kupiga kazi ughaibuni sikusita wala kuacha kujaribu maisha ambayo ndio ilikua njia yangu ya mafanikio hadi leo!

Huku utawakuta wakenya kibao na wanigeria ila wabongo ukiwakuta basi ni wachache sana! Na zile tabia za uswahili wengi hazijawaisha na janja janja nyingi
 
Tunakumbushana tu kuwa Tanzania ina eneo kubwa kuzipita Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda tukiziweka pamoja

Tutumie fursa ya ukubwa wa eneo letu kulead uchumi wa Afrika ya mashariki, pamoja tutaweza.

Kazi Iendelee!
Nashangaa kwamba watu hawaelewi Tanzania inachukua asilimia 52 ya eneo zima la E.A, yaani ukichanganya kenya, uganda, rwanda, burundi zina eneo la 48% pekee huku 52% zilizobaki likiwa ni eneo la Tanzania. Kwa hiyo utaona Tanzania inaweza single-handed kujenga uchumi imara na kuwa na ushawishi eneo zima la E.A bila kujipendekeza kwa lolote kenya...
 
Back
Top Bottom