Uchaguzi 2020 Tutawaadhibu kwenye sanduku la kura bila huruma, tutampa Magufuli ushindi wa 90%

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2019
Posts
1,521
Reaction score
4,381
Kwanza kwenye vita hakuna kulemba hata sisimizi ni wa kumfinyanga finyanga.

CCM tumejiandaa kufanya kampeni za kijeshi nchi nzima usiku na mchana nyumba kwa nyumba kitanda kwa kitanda

Tutawashawishi wananchi wampe Magufuli ushindi wa 90%

Ushindi huu ni wa asante kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa miaka 5 na pia itakuwa ni ishara ya kumtia moyo apambane tena kwa miaka mingine 5
 
Wananchi si ndio sisi ambao tayari tushaamua kumwaga Pombe
 
Mtanzania gani Yuko tayari kuishi kwa shida miaka mitano mingine.

Watumishi? Aah wapi
Vijana? Aah wapi
Wakulima? Ah wapi

Mliyotutenda miaka mitano iliyopita inatosha Nani Yuko tayari kuishi kwa wasiwasi wa kutekwa acheni jiandaeni kuiba kura ndio patanoga zaidi VINGINEVYO mpite na JPM milele ..
 
Magufuli hategemei box la kura kukaa madarakani zaidi ya madaraka yake. Angekuwa anategemea box la kura, tusingeona chaguzi zikinajisiwa toka aingie madarakani.
 
Alivyofanya makubwa hivyo kampeni ya nini tena! Au mlikuwa mnatuhadaa tu hajafanya lolote!
Magufuli anapendwa mno, hahitaji kampeni yoyote atashinda mapema asubuhi!
 
Sema Mtawashawishi Mataga na sio wananchi ,hakuna mwananchi mwenye akili timamu atakayechagua ccm na jiwe wake.
 
Alivyofanya makubwa hivyo kampeni ya nini tena! Au mlikuwa mnatuhadaa tu hajafanya lolote!
Magufuli anapendwa mno, hahitaji kampeni yoyote atashinda mapema asubuhi!
Makubwa yapi aliyofanya?
 
.....Tutawashawishi wananchi wampe Magufuli ushindi wa 90%
Ushindi huu ni wa asante kwa kazi kubwa aliyoifanya....
Kazi kubwa ipi??
Utawaambia nini wapiga kura kuhusu mauaji ya akina Azory, Ben Saa8, na wale weengi wa kwenye voroba??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…