BabaMorgan
JF-Expert Member
- Dec 18, 2017
- 4,869
- 13,137
Ukosefu wa ajira ni miongoni mwa changamoto sugu ulimwenguni kama taifa yatupaswa kuwa na mikakati mipya na endelevu kupunguza ukosefu wa ajira nchini.
Bendera ya Tanzania.
Kila mwaka mamia ya wahitimu wanatunukiwa vyeti vya kuhitimu katika kozi mbalimbali kutoka vyuo vya ndani na nje ya nchi ukweli mchungu ni kuwa serikali haina uwezo wa kuajiri Kila mhitimu kutokana na ufinyu wa nafasi katika taasisi za serikali kulinganisha na idadi kubwa ya wahitimu kutoka vyuo mbalimbali.
Wahitimu Tanzania
Serikali kupitia wawekezaji na wadau kwa kushirikiana wanaweza kupunguza ukosefu wa ajira nchini. sekta binafsi ikipewa nguvu na kutengenezewa mazingira wezeshi basi wahitimu wengi watapata ajira zitazowawezesha kupata kipato cha kukidhi gharama zao za maisha.
Uwepo wa wawekezaji wengi wakubwa katika sekta tofauti kama kilimo na viwanda nchini kutasaidia kwa kiwango kikubwa kumaliza tatizo la ukosefu wa ajira.
Kiwanda Cha sukari.
Je ni nini kifanyike na serikali yetu kuweza kuvutia wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza Tanzania?
1. Kutangaza fursa zinazopatikana Tanzania. Katika vitu Tanzania tunapaswa kujivunia nacho basi ni bandari imerahisisha kufanya biashara za kimataifa. Kwa faida hiyo ni jukumu la Kila Mtanzania popote pale alipo kutangaza fursa zinazopatikana Tanzania kama vile kilimo, madini na utalii pia mabalozi wetu watumie uwepo wao katika mataifa wanayotuwakilisha kutangaza Tanzania lengo kuu ni kuvutia wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza Tanzania.
Bandari Dar es salaam.
2. Kupunguza mlolongo na uchelewashaji usio na tija kwenye usajiri na uanzishwaji wa kampuni. Pamekuwa na malalamiko mengi juu ya taasisi zilizopewa mamlaka ya kutoa vibali vya uwekezaji kwa makusudi kuchelewesha na kutengeneza mianya ya rushwa kwa wawekezaji wapya kimsingi katika ulimwengu wa Sasa muda ni rasilimali muhimu panapokuwa na mlolongo mrefu katika usajiri wa kampuni tunapunguza morali ya wawekezaji kuja huku wengine wakikata tamaa na kuishia njiani. Pawepo na uadilifu kwa maafisa wetu wote kwenye mamlaka zetu.
3. Msamaha wa Kodi katika mitambo ya uzalishaji inayoingia nchini. Kimsingi uwekezaji ni gharama kubwa kama serikali inabidi kuwashika mikono wawekezaji kwa kuwapunguzia gharama hususani Kodi mamlaka ya mapato Tanzania itoe misamaha ya Kodi kwa mitambo ya uzalishaji inayoingia nchini ili kuchochea uanzishwaji wa viwanda vingi.
4. Uongozaji wa haki na demokrasia. Wawekezaji kabla ya uwekezaji ufanya tathmini juu ya uongozi wa sehemu husika kujua ni aina gani ya uongozi unafuatwa tukiwa na uongozi wa haki utachochea wawekezaji kuja kwa wingi
Bendera za vyama vya siasa Tanzania.
5. Uboreshaji wa miundombinu ya usafiri, maji, umeme na huduma za kijamii kama vile elimu na afya. Muwekezaji anashawishika kuwekeza mahali ambapo Kuna uhakika wa upatikanaji wa huduma muhimu kama maji, umeme na miundombinu ya barabara zinazopitika wakati wowote
Morogoro Road.
Hakika tukifanya haya basi tutawavutia wawekezaji wengi kuja nchini mwetu kuwekeza na kupunguza ukosefu wa ajira nchini.
Picha zote chanzo Mtandaoni
Bendera ya Tanzania.
Kila mwaka mamia ya wahitimu wanatunukiwa vyeti vya kuhitimu katika kozi mbalimbali kutoka vyuo vya ndani na nje ya nchi ukweli mchungu ni kuwa serikali haina uwezo wa kuajiri Kila mhitimu kutokana na ufinyu wa nafasi katika taasisi za serikali kulinganisha na idadi kubwa ya wahitimu kutoka vyuo mbalimbali.
Wahitimu Tanzania
Serikali kupitia wawekezaji na wadau kwa kushirikiana wanaweza kupunguza ukosefu wa ajira nchini. sekta binafsi ikipewa nguvu na kutengenezewa mazingira wezeshi basi wahitimu wengi watapata ajira zitazowawezesha kupata kipato cha kukidhi gharama zao za maisha.
Uwepo wa wawekezaji wengi wakubwa katika sekta tofauti kama kilimo na viwanda nchini kutasaidia kwa kiwango kikubwa kumaliza tatizo la ukosefu wa ajira.
Kiwanda Cha sukari.
Je ni nini kifanyike na serikali yetu kuweza kuvutia wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza Tanzania?
1. Kutangaza fursa zinazopatikana Tanzania. Katika vitu Tanzania tunapaswa kujivunia nacho basi ni bandari imerahisisha kufanya biashara za kimataifa. Kwa faida hiyo ni jukumu la Kila Mtanzania popote pale alipo kutangaza fursa zinazopatikana Tanzania kama vile kilimo, madini na utalii pia mabalozi wetu watumie uwepo wao katika mataifa wanayotuwakilisha kutangaza Tanzania lengo kuu ni kuvutia wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza Tanzania.
Bandari Dar es salaam.
2. Kupunguza mlolongo na uchelewashaji usio na tija kwenye usajiri na uanzishwaji wa kampuni. Pamekuwa na malalamiko mengi juu ya taasisi zilizopewa mamlaka ya kutoa vibali vya uwekezaji kwa makusudi kuchelewesha na kutengeneza mianya ya rushwa kwa wawekezaji wapya kimsingi katika ulimwengu wa Sasa muda ni rasilimali muhimu panapokuwa na mlolongo mrefu katika usajiri wa kampuni tunapunguza morali ya wawekezaji kuja huku wengine wakikata tamaa na kuishia njiani. Pawepo na uadilifu kwa maafisa wetu wote kwenye mamlaka zetu.
3. Msamaha wa Kodi katika mitambo ya uzalishaji inayoingia nchini. Kimsingi uwekezaji ni gharama kubwa kama serikali inabidi kuwashika mikono wawekezaji kwa kuwapunguzia gharama hususani Kodi mamlaka ya mapato Tanzania itoe misamaha ya Kodi kwa mitambo ya uzalishaji inayoingia nchini ili kuchochea uanzishwaji wa viwanda vingi.
4. Uongozaji wa haki na demokrasia. Wawekezaji kabla ya uwekezaji ufanya tathmini juu ya uongozi wa sehemu husika kujua ni aina gani ya uongozi unafuatwa tukiwa na uongozi wa haki utachochea wawekezaji kuja kwa wingi
Bendera za vyama vya siasa Tanzania.
5. Uboreshaji wa miundombinu ya usafiri, maji, umeme na huduma za kijamii kama vile elimu na afya. Muwekezaji anashawishika kuwekeza mahali ambapo Kuna uhakika wa upatikanaji wa huduma muhimu kama maji, umeme na miundombinu ya barabara zinazopitika wakati wowote
Morogoro Road.
Hakika tukifanya haya basi tutawavutia wawekezaji wengi kuja nchini mwetu kuwekeza na kupunguza ukosefu wa ajira nchini.
Picha zote chanzo Mtandaoni
Upvote
2