Kama kweli mpo serious anzeni na yule dada aliyeweka bandiko lake humu kama week moja iliyopita akilalamikia unyanyasaji wa kingono Hospital ya rufaa mbeya...
Sent using Jamii Forums mobile app
Wachunguzi wa hizi kesi usikute nao walipata ajira kwa njia hizo hizo
Mtoa tuhuma za rushwa ya ngono Mbeya, Alitengeneza tuhuma za kuchafua na kuwakomoa walimu kwa kuwataja majina yao kwa hisia tu. Kwani hakutoa uthibitisho kuwa amewahi kutoa rushwa ya ngono.Kweli kunahitajika ushahidi maana watuhumiwa wanetajwa live wana famili ni wazi watakuwa wamefedheheka sana. Mtoa tuhuma ajitokeze na kutoa ushahidi vinginevyo ni udgalilishaji kwa watuhumiwa na familia zao. Fikiria mme, babako, ba mkwe, kaka, shemeji anaanikwa hadharani namna ile kuwa anaomba na kulazimisha rushwa ya ngono? So bad!
Sent using Jamii Forums mobile app
Ule Uzi wa malalamiko ya huyo mwanafunzi wa mbeya ulipowekwa hapa nilishauri malalamikaji aende PCCB HQ lifanyiwe kazi haraka kuna mtu mmoja hapa akajifanya mjuaji kwamba asipeleke malalamiko yatafanyiwa kazi kutokea hapa, hovyo kabisa kuna majitu yanadhani yanajua kila kitu lakini hayaelewi, sasa Leo waziri anataka ushahidi upelekwe, lazima tujue kulalamika tu hakutoshi kuchunguza na kupata ushahidi bila kuwepo mlalamikaje!
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli, panahitajika umakini hapa, tena sana, laa sivyo wanaume wanaweza wakawa waathirika wasio na hatia. I would advise anayeona hajatendewa haki awe anaenda mahakamani, mtuhumiwa akikutwa na hatia anachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi na sheria za ajira yake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kweli wanaume tumetofautiana! Anikatae mwanamke halafu nimtishie!Tatizo ni mwanaume kuendelea kuwa king'ang'anizi, mwanamke akikukataa mwache na sio kumtishia kuharibu maisha yake.
trueJamiiForums, Tatizo whistle blowers wengi wanaishia kupata matatizo.
Kwanini msifanye kazi kama FBI, ukipata tip unaifanyia kazi kimyakimya.
Wengine wamejaribu hata kupiga picha maeneo wanaishia kusikojulikana na kesi kibao.