SoC01 Tutumie Vyuo Vikuu na HESLB Kukabiliana na Ukosefu wa Ajira na Mitaji kwa Wahitimu wa Elimu ya Juu

SoC01 Tutumie Vyuo Vikuu na HESLB Kukabiliana na Ukosefu wa Ajira na Mitaji kwa Wahitimu wa Elimu ya Juu

Stories of Change - 2021 Competition

Imalamawazo

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2021
Posts
1,343
Reaction score
3,269
1. Utangulizi

Inawezekanaje tutumie vyuo vikuu kukabiliana na tatizo la ajira ikiwa wahitimu wa vyuo hivyo ndilo kundi linaloongoza kwa kusota mitaani bila ajira?


Japo ni kweli kuwa tatizo la ukosefu wa ajira nchini linadhihirika zaidi miongoni mwa wahitimu wa vyuo vikuu, ni vyema tukataraji pia kuwa suluhisho la ajira kwa vijana hawa litapatikana vyuo vikuu.

Taraja yetu inatokana na utayari wa wahitimu wengi kutosubiri ajira kwenye fani walizozisomea badala yake wanapambana kusaka ujuzi mbadadala nje ya fani zao. Tumekuwa tukishuhudia wahitimu walijitokeza kuomba nafasi za mafunzo ya ufundi stadi (VETA) yanayogharamiwa serikali. Lakini pia wapo wahitimu wanaojifunza mitaani ufundi makenika, mbinu za kilimo, ufugaji wa kisasa, usafirishaji n.k kutoka kwa wenzao wasio na elimu ya juu.

Taswira kubwa tunayopata hapa ni kuwa wahitimu hao wanahangaika kujifunza upya stadi ambazo walipaswa kuwa wamejifunza katika safari yao ya kielimu. Lakini pia wakishatatua chngamoto ya ujuzi wanakumbana na changamoto nyingine hasa hasa ukosefu mitaji. Makala hii inapendekeza mkakati wa kukabiliana na ombwe la stadi na mitaji kwa wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu kwa kuhusisha vyuo vyenyewe na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB).

2. Vyuo vikuu vifanye nini cha ziada?

Chuo kikuu ni sehemu ya kupata maarifa na ujuzi wa kila namna kupitia mifumo na taratibu zilizowekwa. Taratibu hizo kwa namna moja au nyingine zinarahisisha mwanafunzi apate maarifa nje ya shahada aliyodahiliwa kwayo, mhitimu anapata shahada yake pamoja na kitu kingine cha nyongeza. Kutokana na urahisi huo makala hii inapendekeza mkakati maalumu utakao vifanya vyuo vikuu kuanza kutoa shahada na stadi flani ya nyongeza kwa wanafunzi wake, kwa urahisi tuuite, Shahada++.

Vyuo vikuu vinazo fursa za kutekeleza miradi kama hii bila kuathiri mitaala yake wala pasipo kuhitaji kurekebisha mitaala na mifumo ya elimu za msingi na sekondari. Mfano, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na taasisi ya Empower inaendesha program ya Generation Empower inayolenga kuwajengea wahitimu maarifa yanayohitajika karne ya 21 ili waweze kuajiriwa au kujiajiri (Generation Empower, 2020 Generation Empower Media Press Release | Empower imepatikana 27 Julai, 2021). Kumbe hata utekelezaji wa mkakati wa Shahada++ hautaonekana kuwa ni jambo geni katika uwanda wa kitaaluma nchini na duniani kote. Kupitia mkakati wa Shahada++ mhitimu atapata shahada aliyodahiliwa kwayo lakini pia atapata nafasi ya kujifunza stadi flani flani za nyongeza kulingana na hobi zake au fursa zinazopatikana maeneo yake.

3. Je, vyuo vikuu havitageuka vyuo vya kati?

Hapana: Mkakati wa shahada++ hautaingiliana na mafunzo yanayotolewa na vyuo vya chini au chini kwani mafunzo yatakayotolewa yatawalenga wanafunzi wa vyuo vikuu tu. Lakini pia mkakati huu unaweza kutekelezwa sambamba na program za vyuo vikuu pasipo kushusha ubora wa elimu ya vyuo husika. Katika kutekeleza mkakati huu, vyuo vikuu vitatakiwa kushirikiana na wadau kuandaa mitaala ya mafunzo ya stadi zinazotakiwa katika sekta ambazo zinazalisha ajira nyingi au sekta zitakazowawezesha wahitimu kujiajiri.

Mfano wa sekta hizo ni pamoja na ufundi stadi, kilimo, uongezaji wa thamani wa mazao ya kilimo, ufugaji, uchakataji wa malighafi kwa ajili ya viwanda, stadi za TEHAMA, mbinu za ujasiriamali, michezo, sanaa na kadhalika. Kwa hiyo wanafunzi watachagua stadi wazipendazo miongoni mwa stadi za ziada zinazotolewa chuoni kwao kuzingatia hobi zao na fursa zinazowazunguka katika mazingira yao. Kupitia Shahada++ vyuo vitazalisha wahitimu ambao wanajua stadi nyingi zitakayomwezesha kujiajiri na kuajiri wengine.

4. HESLB iwafikie wahitimu wanaotaka kujiajiri

Ili kuufanya mpango wa Shahada++ ulete matokeo tarajiwa ni lazima uambatanishwe na upatikananji wa mitaji. Lakini sehemu kubwa ya wahitimu wa elimu ya juu hawana mitaji wala dhamana zinazokubalika na taasisi za fedha. Katika huo mtanziko wa upatikanaji wa mitaji tunatambua kuwa HESLB ndiyo taasisi pekee itayokuwa ikiwadai wahitimu wa elimu ya juu pesa nyingi.

Isitoshe, HESLB ndiyo taasisi pekee ya kifedha inayoweza kuwaamini wanafunzi na kuwakopesha pesa bila dhamana. Hivyo basi HESLB haipaswi kuondoa imani kwa wanafunzi hao pindi wanapohitimu masomo na kuanza kupambana kupata kujiingizia kipato ambacho pia kitasaidia wahitimu hao kurejesha deni wanalodaiwa. Aidha, ni bora HESLB ikashiriki pia kuwajengea uwezo wa kiuchumi ili kukabiliana na changamoto ya ajira ili waweze kurejesha pesa hizo kwa wakati.

Kwa hiyo inapendekezwa, HESLB itoe fursa ya wahitimu wanaopenda kujiajiri kuomba mkopo usiopungua pesa yao ya boom ya mwaka wa mwisho wa masomo yao ili kuwafanya wahitimu hao waanze safari yao ya kujiajiri kwa kujiamini.

6. Ni nani anaweza kuanzisha utekelezaji wa Shahada++?

Mamlaka za vyuo vikuu, wadau wa elimu na serikali wanaweza kushawishi utekelezaji wa mkakati wa Shahada++. Mfano, serikali inaweza kuamua kutenga pesa kiasi kutokana na zile pesa ambazo zinapelekwa vyuo vya ufundi ikazipeleka pale chuo cha uhandisi pale Chuo kikuu cha Dar es Salaam na kuwataka waandae mafunzo ya ufundi mafupi kwa wanachuo wa shahada zisizo za uhandisi. Lakini pia serikali inaweza kuvipa fursa vyuo vingine vipendekeze mafunzo stadi ambazo zitagharimikiwa na serikali kutokana na maeneo yao ya umahiri kama ujasiriamali, sanaa, uandaaji picha na kadhalika.

Lakini pia wadau wa elimu wanaweza kushawishi taasisi mbalimbali ikiwemo Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) na kupeleka pendekezo la Shahada++ vyuoni kama namna ya kuvipa changamoto vyuo vikuu ili viweze kubuni njia za kuwasaidia wahitimu kukabiliana na changamoto ya soko la ajira. Hata serikali za wanafunzi zenyewe zinaweza kushirikiana na mashirika kama shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo (SIDO) na kuanza utekelezaji wa shahada++ kama mpango wa muda mfupi.

Hata hivyo, katika utekelezaji wa Shahada++ ni vema kutofautisha mkakati wa Shahada++ na zile kozi fupi mithili ya zile za Microsoft office zinazotolewa kwenye baadhi ya vyuo kwa wanafunzi nyakati za likizo fupi. Shahada++ inayopendekezwa inatakiwa irasimishwe na ngazi zinazo rasimisha mitaala vyuoni. Pia mwanafunzi asilazimike kulipa tozo ya ziada ili kupata mafunzo hayo ya ziada. Kwa hiyo kumbe siyo kila mtu anaweza kuwafanya hao wazee wa vyuo vikuu wakune vichwa vyao bali ni wadau wa elimu ya juu.

7. Hitimisho

Mkakati wa Shahada++ unaopendekezwa utatuwezesha kujaziliza ombwe la stadi kwa wahitimu pasipo kulazimika kufumua na kusuka upya mitaala ya shule za msingi na sekondari. Pia mkakati huu utawasaidia wananchi kuwapuuza baadhi ya watu wanaodai kuwa wahitimu wa darasa la saba ni bora kuliko wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu nchini. Hivyo utaongeza hamu ya watu kupata elimu ya chuo kikuu, itapanua wigo wa wahitimu kujiajiri, itaongeza tija kwenye sekta za uzalishaji mali kama kilimo, ufugaji, usafirishaji, tehema na uzalishaji wa bidhaa.

Mwisho kabisa Shahada++ pia utasidia kujenga urafiki kati ya wahitimu na HESLB hivyo kuongeza ufanisi katika ukukusanyaji madeni.
 
Upvote 14
Wadau tuipigie kelele serikali HESLB itoe boom kidogo kwa wahitimu tujiajiri jamani mtaani kugumu
 
Badala ya kuja na mapendekezo mapya, kwanini tusiangalie wenzetu nchi zilizoendelea mbona elimu ya chuo kikuu imeendelea kuwa na thamani, sisi hapa ni wapi tumekosea? Je hizi siasa za kuongeza udahili bila kuzingatia ubora hazijatufikisha hapa? Unaongezaje udahili, wakati hujaboresha mazingira. Walikuwa wanasoma sayansi miaka ya nyuma , maabara zilikuwa zinatosha. Hii leo ni kawaida mtu kumaliza degree ya sayanso bila kupata muda wa kutosha maabara. Je taratibu za kuajiri waalimu zinazingatia watu wenye ubora?
 
Mimi nimeipenda, sio tunalalamika tu elimu yetu haimsaidii kijana kujiajiri wakati hatujamuwezesha skills wala Capital , na sidhani kama ni vizuri kusema vijana wa chuo kikuu wote waende Ufundi, shahada++ ni ushauri Mzuri
 
Badala ya kuja na mapendekezo mapya, kwanini tusiangalie wenztu nchi zilizoendelea mbona elimu ya chuo kikuu imeendelea kuwa na thamani, sisi hapa ni wapi tumekosea? Je hizi siasa za kuongeza udahili bila kuzingatia ubora hazijatufikisha hapa? Unaongezaje udahili, wakati hujaboresha mazingira. Walikuwa wanasoma sayansi miaka ya nyuma , maabara zilikuwa zinatosha. Hii leo ni kawaida mtu kumaliza degree ya sayanso bila kupata muda wa kutosha maabara. Je taratibu za kuajiri waalimu zinazingatia watu wenye ubora?
Mazingira yaboreshwe na muundo pia wa course uboreshwe uwe wa manufaa kwa anayesoma
 
1. Utangulizi

Inawezekanaje tutumie vyuo vikuu kukabiliana na tatizo la ajira ikiwa wahitimu wa vyuo hivyo ndilo kundi linaloongoza kwa kusota mitaani bila ajira?


Japo ni kweli kuwa tatizo la ukosefu wa ajira nchini linadhihirika zaidi miongoni mwa wahitimu wa vyuo vikuu, ni vyema tukataraji pia kuwa suluhisho la ajira kwa vijana hawa litapatikana vyuo vikuu.

Taraja yetu inatokana na utayari wa wahitimu wengi kutosubiri ajira kwenye fani walizozisomea badala yake wanapambana kusaka ujuzi mbadadala nje ya fani zao. Tumekuwa tukishuhudia wahitimu walijitokeza kuomba nafasi za mafunzo ya ufundi stadi (VETA) yanayogharamiwa serikali. Lakini pia wapo wahitimu wanaojifunza mitaani ufundi makenika, mbinu za kilimo, ufugaji wa kisasa, usafirishaji n.k kutoka kwa wenzao wasio na elimu ya juu.

Taswira kubwa tunayopata hapa ni kuwa wahitimu hao wanahangaika kujifunza upya stadi ambazo walipaswa kuwa wamejifunza katika safari yao ya kielimu. Lakini pia wakishatatua chngamoto ya ujuzi wanakumbana na changamoto nyingine hasa hasa ukosefu mitaji. Makala hii inapendekeza mkakati wa kukabiliana na ombwe la stadi na mitaji kwa wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu kwa kuhusisha vyuo vyenyewe na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB).

2. Vyuo vikuu vifanye nini cha ziada?

Chuo kikuu ni sehemu ya kupata maarifa na ujuzi wa kila namna kupitia mifumo na taratibu zilizowekwa. Taratibu hizo kwa namna moja au nyingine zinarahisisha mwanafunzi apate maarifa nje ya shahada aliyodahiliwa kwayo, mhitimu anapata shahada yake pamoja na kitu kingine cha nyongeza. Kutokana na urahisi huo makala hii inapendekeza mkakati maalumu utakao vifanya vyuo vikuu kuanza kutoa shahada na stadi flani ya nyongeza kwa wanafunzi wake, kwa urahisi tuuite, Shahada++.

Vyuo vikuu vinazo fursa za kutekeleza miradi kama hii bila kuathiri mitaala yake wala pasipo kuhitaji kurekebisha mitaala na mifumo ya elimu za msingi na sekondari. Mfano, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na taasisi ya Empower inaendesha program ya Generation Empower inayolenga kuwajengea wahitimu maarifa yanayohitajika karne ya 21 ili waweze kuajiriwa au kujiajiri (Generation Empower, 2020 Generation Empower Media Press Release | Empower imepatikana 27 Julai, 2021). Kumbe hata utekelezaji wa mkakati wa Shahada++ hautaonekana kuwa ni jambo geni katika uwanda wa kitaaluma nchini na duniani kote. Kupitia mkakati wa Shahada++ mhitimu atapata shahada aliyodahiliwa kwayo lakini pia atapata nafasi ya kujifunza stadi flani flani za nyongeza kulingana na hobi zake au fursa zinazopatikana maeneo yake.

3. Je, vyuo vikuu havitageuka vyuo vya kati?

Hapana: Mkakati wa shahada++ hautaingiliana na mafunzo yanayotolewa na vyuo vya chini au chini kwani mafunzo yatakayotolewa yatawalenga wanafunzi wa vyuo vikuu tu. Lakini pia mkakati huu unaweza kutekelezwa sambamba na program za vyuo vikuu pasipo kushusha ubora wa elimu ya vyuo husika. Katika kutekeleza mkakati huu, vyuo vikuu vitatakiwa kushirikiana na wadau kuandaa mitaala ya mafunzo ya stadi zinazotakiwa katika sekta ambazo zinazalisha ajira nyingi au sekta zitakazowawezesha wahitimu kujiajiri.

Mfano wa sekta hizo ni pamoja na ufundi stadi, kilimo, uongezaji wa thamani wa mazao ya kilimo, ufugaji, uchakataji wa malighafi kwa ajili ya viwanda, stadi za TEHAMA, mbinu za ujasiriamali, michezo, sanaa na kadhalika. Kwa hiyo wanafunzi watachagua stadi wazipendazo miongoni mwa stadi za ziada zinazotolewa chuoni kwao kuzingatia hobi zao na fursa zinazowazunguka katika mazingira yao. Kupitia Shahada++ vyuo vitazalisha wahitimu ambao wanajua stadi nyingi zitakayomwezesha kujiajiri na kuajiri wengine.

4. HESLB iwafikie wahitimu wanaotaka kujiajiri

Ili kuufanya mpango wa Shahada++ ulete matokeo tarajiwa ni lazima uambatanishwe na upatikananji wa mitaji. Lakini sehemu kubwa ya wahitimu wa elimu ya juu hawana mitaji wala dhamana zinazokubalika na taasisi za fedha. Katika huo mtanziko wa upatikanaji wa mitaji tunatambua kuwa HESLB ndiyo taasisi pekee itayokuwa ikiwadai wahitimu wa elimu ya juu pesa nyingi.

Isitoshe, HESLB ndiyo taasisi pekee ya kifedha inayoweza kuwaamini wanafunzi na kuwakopesha pesa bila dhamana. Hivyo basi HESLB haipaswi kuondoa imani kwa wanafunzi hao pindi wanapohitimu masomo na kuanza kupambana kupata kujiingizia kipato ambacho pia kitasaidia wahitimu hao kurejesha deni wanalodaiwa. Aidha, ni bora HESLB ikashiriki pia kuwajengea uwezo wa kiuchumi ili kukabiliana na changamoto ya ajira ili waweze kurejesha pesa hizo kwa wakati.

Kwa hiyo inapendekezwa, HESLB itoe fursa ya wahitimu wanaopenda kujiajiri kuomba mkopo usiopungua pesa yao ya boom ya mwaka wa mwisho wa masomo yao ili kuwafanya wahitimu hao waanze safari yao ya kujiajiri kwa kujiamini.

6. Ni nani anaweza kuanzisha utekelezaji wa Shahada++?

Mamlaka za vyuo vikuu, wadau wa elimu na serikali wanaweza kushawishi utekelezaji wa mkakati wa Shahada++. Mfano, serikali inaweza kuamua kutenga pesa kiasi kutokana na zile pesa ambazo zinapelekwa vyuo vya ufundi ikazipeleka pale chuo cha uhandisi pale Chuo kikuu cha Dar es Salaam na kuwataka waandae mafunzo ya ufundi mafupi kwa wanachuo wa shahada zisizo za uhandisi. Lakini pia serikali inaweza kuvipa fursa vyuo vingine vipendekeze mafunzo stadi ambazo zitagharimikiwa na serikali kutokana na maeneo yao ya umahiri kama ujasiriamali, sanaa, uandaaji picha na kadhalika.

Lakini pia wadau wa elimu wanaweza kushawishi taasisi mbalimbali ikiwemo Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) na kupeleka pendekezo la Shahada++ vyuoni kama namna ya kuvipa changamoto vyuo vikuu ili viweze kubuni njia za kuwasaidia wahitimu kukabiliana na changamoto ya soko la ajira. Hata serikali za wanafunzi zenyewe zinaweza kushirikiana na mashirika kama shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo (SIDO) na kuanza utekelezaji wa shahada++ kama mpango wa muda mfupi.

Hata hivyo, katika utekelezaji wa Shahada++ ni vema kutofautisha mkakati wa Shahada++ na zile kozi fupi mithili ya zile za Microsoft office zinazotolewa kwenye baadhi ya vyuo kwa wanafunzi nyakati za likizo fupi. Shahada++ inayopendekezwa inatakiwa irasimishwe na ngazi zinazo rasimisha mitaala vyuoni. Pia mwanafunzi asilazimike kulipa tozo ya ziada ili kupata mafunzo hayo ya ziada. Kwa hiyo kumbe siyo kila mtu anaweza kuwafanya hao wazee wa vyuo vikuu wakune vichwa vyao bali ni wadau wa elimu ya juu.

7. Hitimisho

Mkakati wa Shahada++ unaopendekezwa utatuwezesha kujaziliza ombwe la stadi kwa wahitimu pasipo kulazimika kufumua na kusuka upya mitaala ya shule za msingi na sekondari. Pia mkakati huu utawasaidia wananchi kuwapuuza baadhi ya watu wanaodai kuwa wahitimu wa darasa la saba ni bora kuliko wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu nchini. Hivyo utaongeza hamu ya watu kupata elimu ya chuo kikuu, itapanua wigo wa wahitimu kujiajiri, itaongeza tija kwenye sekta za uzalishaji mali kama kilimo, ufugaji, usafirishaji, tehema na uzalishaji wa bidhaa.

Mwisho kabisa Shahada++ pia utasidia kujenga urafiki kati ya wahitimu na HESLB hivyo kuongeza ufanisi katika ukukusanyaji madeni.
Andiko zuri sana, hongera mkuu

Kwa kuongezea, Wizara ya Elimu ishirikiane na taasisi mbalimbali kuangalia namna ya kuboresha mfumo wetu wa elimu ambao unatujenga kusubiri ajira badala ya kubuni namna tofauti za kukabiliana na maisha nje ya ajira, hii mbinu uliyoirleza hapa ni moja kati ya mbinu mbora zidi, naamini andiko hili litasomwa na wahusika

Ukiangalia kwa sasa ni kama Heslib wanapata hasara kwa sababu asilimia kubwa ya wahitumu wapo majumbani hawana ajira na hawana namna ya kurejesha mkopo, kwa hiyo vi vyema wakatumia mbinu hii kuwasaifia wahitimu kurejesha mikopo kwa wakati ili iweze kuwasaidia na wengine
 
Maoni yangu ni kwamba kuna wizi, ufisadi na ubadhirifu wa kutisha Serikalini. Kwa hesabu za haraka haraka toka 2015 hadi leo hii wizi, ufisadi na ubadhirifu Serikalini umetugharimu zaidi ya trillion 10. Ununuzi mbali mbali ikiwemo ndege, V8 etc vitu ambavyo havina tija kwa Taifa, ujenzi wa nyumba za marais wastaafu kila nyumba ni bilioni na ushee Kikwete, Mkapa, Mwinyi. Magufuli. Ujenzi wa chato airport na mazagaza mengine kule chato kijijini ambavyo si kipaumbele kwa Taifa.
inasemekana Serikali inakusanya kodi kila mwezi trillioni moja, nusu ya hiyo amount inalipa mishahara ya Wafanyakazi Serikalini T shs 500 billions.
Hebu fikiria kama ndani ya miaka mitano tu wizi, ufisadi na ubadhirifu umeligharimu Taifa letu zaidi ya trillion 10 au zaidi ya trillion 2 kila mwaka, hiyo mianya ingekuwa haipo au ingezibwa basi Serikali ingeweza kabisa kuajiri idadi hata ya mara nne ya Wafanyakazi wa sasa Serikalini.
Tunaziona ripoti za CAGs kila mwaka yaliyomo yanatisha na kusikitisha sana lakini hakuna ANAYEWAJIBISHWA!!! Hivi sasa maccm yamefikia hadi kumtisha CAG kwamba YATAMUUA!!!
1627492889498.jpeg

The Monk Saint Anne Baba Swalehe Abrianna The Boss BAK Paul Alex Paula Paul tunaomba michango yenu kuhusiana na hii mada pamoja na kura zenu lol
 
Maoni yangu ni kwamba kuna wizi, ufisadi na ubadhirifu wa kutisha Serikalini. Kwa hesabu za haraka haraka toka 2015 hadi leo hii wizi, ufisadi na ubadhirifu Serikalini umetugharimu zaidi ya trillion 10. Ununuzi mbali mbali ikiwemo ndege, V8 etc vitu ambavyo havina tija kwa Taifa, ujenzi wa nyumba za marais wastaafu kila nyumba ni bilioni na ushee Kikwete, Mkapa, Mwinyi. Magufuli. Ujenzi wa chato airport na mazagaza mengine kule chato kijijini ambavyo si kipaumbele kwa Taifa.
inasemekana Serikali inakusanya kodi kila mwezi trillioni moja, nusu ya hiyo amount inalipa mishahara ya Wafanyakazi Serikalini T shs 500 billions.
Hebu fikiria kama ndani ya miaka mitano tu wizi, ufisadi na ubadhirifu umeligharimu Taifa letu zaidi ya trillion 10 au zaidi ya trillion 2 kila mwaka, hiyo mianya ingekuwa haipo au ingezibwa basi Serikali ingeweza kabisa kuajiri idadi hata ya mara nne ya Wafanyakazi wa sasa Serikalini.
Tunaziona ripoti za CAGs kila mwaka yaliyomo yanatisha na kusikitisha sana lakini hakuna ANAYEWAJIBISHWA!!! Hivi sasa maccm yamefikia hadi kumtisha CAG kwamba YATAMUUA!!!
View attachment 1872029

Nakuelewa sana mkuu,ndio maana mkuu Abrianna akaweka hapa kuwe na independent body itakayo deal na dira ya taifa sio mtu mmoja kujiamulia tu anavyotaka, kampe kura hapa.......lol.... Story of Change - Umuhimu wa kuwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa inayotekelezeka kwa wakati na kwa kuzingatia rasilimali zilizopo kuwe
 
Kuwa na Dira ya Taifa ni jambo la muhimu sana, lakini kwa maoni yangu hii haitakuwa huru bila ya kuwepo Katiba mpya vinginevyo Rais kutokana na madaraka makubwa sana aliyokuwa nayo ikiwemo kuteua na kufukuza basi wajumbe wa Tume hiyo ya dira ya Taifa hawatakuwa huru na wataingiliwa katika utendaji wao matokeo yake Tume itakuwa ipo ipo tu bila ya kuwa na manufaa yoyote yale kwa Watanzania.
1627495904374.jpeg

Nakuelewa sana mkuu,ndio maana mkuu Abrianna akaweka hapa kuwe na independent body itakayo deal na dira ya taifa sio mtu mmoja kujiamulia tu anavyotaka, kampe kura hapa.......lol.... Story of Change - Umuhimu wa kuwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa inayotekelezeka kwa wakati na kwa kuzingatia rasilimali zilizopokuwe
 
Mimi nimeipenda, sio tunalalamika tu elimu yetu haimsaidii kijana kujiajiri wakati hatujamuwezesha skills wala Capital , na sidhani kama ni vizuri kusema vijana wa chuo kikuu wote waende Ufundi, shahada++ ni ushauri Mzuri
Zamani vyuo vikuu siku vilikuwa vinafanya tafiti za kufuatilia mafanikio ya wahitimu wao huko mitaani, sijui kama bado wanafanya hivyo au wameaacha?
 
Badala ya kuja na mapendekezo mapya, kwanini tusiangalie wenztu nchi zilizoendelea mbona elimu ya chuo kikuu imeendelea kuwa na thamani, sisi hapa ni wapi tumekosea? Je hizi siasa za kuongeza udahili bila kuzingatia ubora hazijatufikisha hapa? Unaongezaje udahili, wakati hujaboresha mazingira. Walikuwa wanasoma sayansi miaka ya nyuma , maabara zilikuwa zinatosha. Hii leo ni kawaida mtu kumaliza degree ya sayanso bila kupata muda wa kutosha maabara. Je taratibu za kuajiri waalimu zinazingatia watu wenye ubora?
Nchi za wenzetu wametumia mifumo kama hii. Kuna siku Spika Job Ndugai alichomekea story moja kuhusu umahiri wa vijana wa China, alisema hivi, afisa ubalozi mmoja alimwambia kijana aliyeonesha nyumba ya kuishi amtafutie fundi wa kurekebisha mfumo wa maji ndani ya nyumba, yule kijana akamwambia sawa. Kijana akafanya mwenyewe. Afisa akamwambia tena kijana amtafutiea fundi wa kerebisha taa za umeme, yule kijana akajibu sawa. Kijana akafanya mwenyewe. Afisa akamwambia tena amtafutie fundi wa kurekebisha makabati, yule kijana akamjibu sawa. Kijana akarekebisha makabati safi.
Swali la kujiuliza, je sisi hatuwezi kuwapa ujuzi wa namna hii vijana wetu? Jibu ni tunaweza.
Mtu akiniuliza hizi stadi tuzitoe katika level ipi? Ningemjibu level yoyote ya elimu kuanzia msingi hadi chuo kikuu. Lakini kwa waliokosa fursa ya kupata hizo stadi lakini wakapata fursa ya kusoma chuo kikuu tuwapatie hizo stadi, zitawafaa sana kwa maana vijana wanakuwa wameshajitambua.
 
Andiko zuri sana, hongera mkuu

Kwa kuongezea, Wizara ya Elimu ishirikiane na taasisi mbalimbali kuangalia namna ya kuboresha mfumo wetu wa elimu ambao unatujenga kusubiri ajira badala ya kubuni namna tofauti za kukabiliana na maisha nje ya ajira, hii mbinu uliyoirleza hapa ni moja kati ya mbinu mbora zidi, naamini andiko hili litasomwa na wahusika

Ukiangalia kwa sasa ni kama Heslib wanapata hasara kwa sababu asilimia kubwa ya wahitumu wapo majumbani hawana ajira na hawana namna ya kurejesha mkopo, kwa hiyo vi vyema wakatumia mbinu hii kuwasaifia wahitimu kurejesha mikopo kwa wakati ili iweze kuwasaidia na wengine
Hivi karibuni waziri alisema wanafanya maboresho ya mitaala ya msomo yote kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha sita. Ni vizuri. Lakini changamoto watakayokumbana nayo hasa upande wa masomo ya ufundi ni waalimu. Hivyo watalazimika kuweka mikakati mipya ya kuwapata waalimu wenye ujuzi huo. Naamini wakiweka fungu mezani na kuvipa vyuo vikuu viwabrash hao hao wanafunzi wa uwalimu kwenye maeneo ya stadi za ufundi kupitia Shahada++ watakuwa wameua ndege wawili kwa jiwe moja. Yaani wamewatatulia hawa vijana tatizo la ajira lakini pia nao wao watapata waalimu.
 
Halafu anatokea mtu anakwambia nchi hii ina wasomi wengi sana, hao kina Kishimba sijui Musukuma wanaobeza elimu chunguza ujue watoto wao wamesoma shule gani.
c35ffdc1-2821-4c69-89d1-516301a6ee1e.jpg
 
Halafu anatokea mtu anakwambia nchi hii ina wasomi wengi sana, hao kina Kishimba sijui Musukuma wanaobeza elimu chunguza ujue watoto wao wamesoma shule gani.
View attachment 1872685
Kabisa mkuu, elimu ya chuo kikuu bado inahitajika hapa nchini. Tatizo vyuo vyetu vimekuwa vya kukariri vitu vya zamani wala havitafuti maarifa mapya yenye kuleta ajira kwa wahitimu.

Hivi ulishawaza kwa nini miradi kama Bwawa la Nyerere haina attachmemnt na chuo kikuu chochote cha serikali hapa nchini licha ya serikali inawekeza pesa mingi? Ikiwa hatutumii fursa kama hizi kujenga uwezo wetu wa ndani inamaana hapo baadae tutakapotaka kukarabati mabwawa haya tutalazimika kuita tena kampuni ya nje. Je ni ajira kiasi gani tutakuwa tumewapotezea vijana wetu sasa na baadae? Kwa hiyo ndo maana nasema tuvitumie vyuo vikuu kukabiliana na ukosefu wa ajira. Hao watu tukiwalazamisha wakune vichwa vyao lazima tutapata suluhu ya baadhi ya matatizo yetu.
 
Thank you Rebeca 83, i am on it
Wadogo zenu tunapiga bei simu, vitanda, godoro na mitungi ya gesi ili tupate nauli ya kurejea nyumbani baada ya kusota chuoni kwa miaka 3 au minne. Kama nauli tu inabidi tupige bei vyombo vya ndani, je tutataweza kupata pesa ya kujiajiri? Hapa tuikomalie HESLB iwajali wahitimu pia
 
Kama ambavyo suala la bima ya afya kwa wote na mikopo ya wanafunzi lilivyoibuka kwenye kampeni za uchaguzi mkuu 2020, tutarajie pia hoja za extension ya mikopo hiyo kwa wahitimu kama ilivyopendekezwa hapa litaibuka kwenye uchaguzi 2025. Vijana tuipigie chapuo hoja hii isikike kwa wahusika, tupatiwe boom tufanya miradi.
 
Back
Top Bottom