Tuwadhibiti Mamluki wasio na sifa walioingizwa kwenye mabaraza ya katiba

Tuwadhibiti Mamluki wasio na sifa walioingizwa kwenye mabaraza ya katiba

Izack Mwanahapa

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2011
Posts
497
Reaction score
236
Ndugu wazalendo wananchi wa Tanzania, tumelalamika sana kuhusu mapungufu na uchakachuaji ambao umejitokeza kwenye uundaji wa mabaraza ya katiba kiasi cha kuonesha kukosa imani na mabaraza hayo. Tutumie fursa hii maridhaya ya kuendesha mabaraza huru ya katiba kutumia Asasi, Taasisi na Makundi ya watu wenye malengo yanayofanana kutoa maoni yetu kwa ufasaha.

Naamini nguvu ya makundi haya ni kubwa kuliko nguvu ya mabaraza halisi ya katiba kwani asasi na taasisi zinaweza kupata watoa maoni wengi zaidi kuliko wale waliomo kwenye mabaraza ya katiba kwani asasi zipo kila kona ya nchi hii. Ni muda wa kuungana na kulipigania taifa letu, nchi inahitaji misingi bila kujali ni nani anategemewa kuchukua nchi 2015.

Naamini waliokuwa wakisukumwa na uzalendo kulalamikia Mabaraza ya katiba wataitumia fursa hii, samahani sana kwa wale ndugu waliokuwa wakisukumwa na posho kwasababu ni wazi kwamba mabaraza haya ya asasi na taasisi yapo kiharakati zaidi posho kidogo au hamna kabisa. Weka Taifa kwanza mengine baadae.

Nimeatach muongozo wa kuendesha mabaraza hayo ya makundi mbalimbali, humo mpaka vikundi vya wakulima vipo na vinaruhusiwa kutoa maoni yao kwa uhuru.
 

Attachments

Hi Wa Jf.
Nafkri ni vizuri kuwa na huu mwongozo, ila nafkri ni busara kama kungekua na chombo kiwakilishi (ambrela group ya tasisi zote) ambacho kitakusanya maoni yote ya taasi na kuyapitia na kuweka summary ya key findings/issues katika vipengele vyote muhimu kulingana na maoni ya wananchi na kuyawakilisha kwenye tume. Ninaloona mimi kwa sasa ni mchanga wa macho tu tunapigwa na tume ya katiba, maana tume haitaweza kupitia maoni ya kila kikundi na kimsingi watajikita zaidi kwenye maoni waliyopata kutoka kwenye mabaraza yao. Mie nafkri kwa kufanya hivyo hoja za taasisi zote zingeweza kuwakilishwa kwa mapana zaidi na kwa uzito zaidi na pia kuwa na kumbukumbu nzuri ya document moja ya maoni ya taasisi katika mchakato wakupata katiba kipengele kwa kipengele.
Kwa sasa nafkri tume inataka tu kuaminisha umma kuwa kulikua na upana wa ushirikishwaji bila kuzingatia kimsingi maoni ya kila kikundi.
Ni mtazamo wangu.
 
Back
Top Bottom