KERO TUWASA kuweni na huruma, maji hayatoki Kata ya Mwinyi - Tabora, yakitoka ni machafu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
HIvi nyie Watu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tabora (TUWASA) hapa Tabora huwa mnachukuliaje Wananchi? Tangu wiki iliyopita Kata ya Mwinyi hakuna huduma za maji na hata yanapotoka yanakuwa machafu na yanatoka kwa muda mfupi, mnataka Watu tuishije!

Mwinyi iko Manispaa ya Tabora inakuwaje Manispaa tunakosa maji na hawa watu wapo? Mamlaka au viongozi mnaohusika angalieni hili suala, linatuumiza Wananchi, tunapata wakati mgumu kupata huduma hii na tukiipata tunalazimika kutumia gharama kubw aya usafiri na hata kununua sehemu tofauti.

 

Attachments

  • 20241217_185140.jpg
    369 KB · Views: 4
  • 20241217_185137.jpg
    372.7 KB · Views: 3
  • 20241217_185131.jpg
    645.2 KB · Views: 4
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…