Tuwatambue wapigania ukombozi mamboleo wasiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili

Tuwatambue wapigania ukombozi mamboleo wasiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kupigania ukombozi wa nchi ni harakati zote zenye lengo la kuitoa nchi katika mifumo ya dhuluma katika kipindi chochote. Huku kupo sawia na kupigania uhuru kwa kina Mandela, Nyerere, Samora, Museveni, Garang, au kina Kagame wa Rwanda huko.

Kwamba makwetu leo dhuluma zimetamalaki tena hadi kufikia kwenye uporaji wa maisha ya watu, kwa hakika kunahitajika ukombozi wa "caliber" zile zile za enzi za uhuru.

Jukumu la ukombozi haliwezi kuwa la mtu mmoja, kikundi au chama kimoja; bali wananchi wa matabaka yote wenye kuchukizwa na dhuluma au "status quo."

Humo hakuwezi kuwa na nafasi ya ubaguzi wa kivyama, kikabila, kikanda, kidini, kimkoa, nk.

Humo watakuwamo ma CCM, Chadema, ACT, CHAUSTA, CHAUMA, UDP, CUF nk.

Humo watakuwamo watanganyika kwa wazanzibari, wasukuma, wachaga, wahaya, wandengereko, nk.

Humo watakuwamo wamatumbi, waarabu, wahindi, nk.

Kwamba kinachotukutanisha sote pamoja ni kiu ya kupata haki au kiu ya ukombozi wa nchi yetu dhidi ya dhuluma, nani anaweza kujidhania kuwa bora au mpambanaji zaidi kuliko nani?

Kwamba kumbe tunaweza kuwa na chuki na nani baina yetu hata kama kaongoka juzi?

Kwani yuko wapi anayefurahishwa na tekaji za watanzania wenzetu? Ni CCM, Nchimbi, Tulia au Samia?

Tuwapelekee mialiko washirika wetu wote hawa katika haki, kokote waliko. Tukapate kuwakemea watesi wetu katika umoja wetu. Nani asingependa kuujua ukweli? Nani anaweza kupinga umuhimu wa uchunguzi huru?

Kwamba nani asiyeuona umuhimu wa Sep. 23?

Pamoja na yote, tujiangalie wandugu kama tuna chuki na awaye yote katika jitihada hizi za ukombozi; bila kujua:

"Tunaweza kuwa wapigania ukombozi mamboleo tusiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili."
 
imhotep, Zawadini na wale wapenzi wengine wa Mungu huu ni ukweli mwingine mchungu:

Tusipoangalia, bila kujua:

"Tunaweza kuwa wapigania ukombozi mamboleo tusiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili."
 
Mkuu sisi bado tuna ubinafsi chuki na ubaguzi na ndio mtaji wanaotumia viongozi wetu maana hatujielewi

Uko sahihi na ndiyo maana miaka 30 leo, tungali tunacheza makida makida.

Tumewekeza mno kwenye mifarakano na mitafaruku isiyokuwa na tija, bila chembe ya uwekezaji kwenye makaribiano.

Ndiyo maana huwezi kuwaona ndugu zetu wengine wa damu kabisa wa aina za kina imhotep hapa.

"Ni mwendo wa kujipitia juu kwa juu kimya kimya, wakijisemea hiiiiiiii .. iiiii ...!"

Tlaatlaah, Lucas Mwashambwa, johnthebaptist au wale wengine, kwani nyie hamchukizwi na tekaji tekaji hizi? Kwani nyie hampendi zikome?

Kwani nyie msingependa kuujua ukweli na kuwawajibisha wakora wote bila kujali nafasi zao popote?

Nchimbi kaonyesha uthubutu.

Kulikoni Sep 23 isiwe na umuhimu kwetu sote? Kama tuko sote kulikoni tusiwaletee mialiko?
 
Ngoja nisome Tena ndipo nichangie

Siyo wewe tu hata wale wengine huwezi kuwaona hapa.

Ni mwendo wa kupita juu kwa juu kimya kimya na kujisemea:


"Hiiiiiii ... iiiii ... !"

imhotep, na wale wapenzi wengine wa Mungu au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kumbuka ni Vyama vyenyewe ndivyo vinawagawa Wananchi na kuzuia Umoja na kutengeneza uadui.

Na kwa hulka ya Mtanzania wa Yanga/Simba hapa ndio kafikishwa kwenye "us and them".
 
Uko sahihi na ndiyo maana miaka 30 leo, tungali tunacheza makida makida.

Tumewekeza mno kwenye mifarakano na mitafaruku isiyokuwa na tija, bila chembe ya uwekezaji kwenye makaribiano.

Ndiyo maana huwezi kuwaona ndugu zetu wengine wa damu kabisa wa aina za kina imhotep hapa.

"Ni mwendo wa kujipitia juu kwa juu kimya kimya, wakijisemea hiiiiiiii .. iiiii ...!"

Tlaatlaah, Lucas Mwashambwa, johnthebaptist au wale wengine, kwani nyie hamchukizwi na tekaji tekaji hizi? Kwani nyie hampendi zikome?

Kwani nyie msingependa kuujua ukweli na kuwawajibisha wakora wote bila kujali nafasi zao popote?

Nchimbi kaonyesha uthubutu.

Kulikoni Sep 23 isiwe na umuhimu kwetu sote? Kama tuko sote kulikoni tusiwaletee mialiko?
Maandamano yamepigwa marufuku.sasa wewe jifanye kichwa ngumu utoe pua yako barabarani kwenda kuandamana. Tuviache vyombo vyetu viendelee kufanya uchunguzi wa kina na kutuletea ripoti .tuwe watulivu na wenye subira na kutoa ushirikianao pale itakapohitajika kufanya hivyo.jukumu la ulinzi wa Nchi yetu ni letu sote.
 
Maandamano yamepigwa marufuku.sasa wewe jifanye kichwa ngumu utoe pua yako barabarani kwenda kuandamana. Tuviache vyombo vyetu viendelee kufanya uchunguzi wa kina na kutuletea ripoti .tuwe watulivu na wenye subira na kutoa ushirikianao pale itakapohitajika kufanya hivyo.jukumu la ulinzi wa Nchi yetu ni letu sote.

Mtuhumiwa ambaye kama ndiye tunayetaka kumkemea atatuzuia je? Kwamba hataki tupaze sauti zetu kudai uchunguzi huru?

Sisi tuko na wote wanaokerwa na tekaji tekaji hizi.

Huko tuko na kina CCM, Nchimbi, Tulia, Samia, Chadema, ACT, Masheikh nk kuwataja wachache tunaosononeshwa mno na wakora hao.

Kwani wewe haumo humo? Kulikoni usibubujikwe machozi ya furaha sasa kudai haki mama akiwa mwalikwa?

Ngoja tumalize kuwapelekea wenzetu mialiko.

23 Sep inabakia siku muhimu sana kwetu.
 
Kumbuka ni Vyama vyenyewe ndivyo vinawagawa Wananchi na kuzuia Umoja na kutengeneza uadui.

Na kwa hulka ya Mtanzania wa Yanga/Simba hapa ndio kafikishwa kwenye "us and them".

Sina hakika kama unajua tuna kaugonjwa sugu ka kumnyooshea kidole kila mtu ila sisi.

Kwa hakika ka ugonjwa haka ni kabaya kuliko ukimwi!

Na kwa hakika tusipogutuka tutajikuta:

"Hatuna mchango wowote kwenye taifa hili."
 
Kupigania ukombozi wa nchi ni harakati zote zenye lengo la kuitoa nchi katika mifumo ya dhuluma katika kipindi chochote. Huku kupo sawia na kupigania uhuru kwa kina Mandela, Nyerere, Samora, Museveni, Garang, au kina Kagame wa Rwanda huko.

Kwamba makwetu leo dhuluma zimetamalaki tena hadi kufikia kwenye uporaji wa maisha ya watu, kwa hakika kunahitajika ukombozi wa "caliber" zile zile za enzi za uhuru.

Jukumu la ukombozi haliwezi kuwa la mtu mmoja, kikundi au chama kimoja; bali wananchi wa matabaka yote wenye kuchukizwa na dhuluma au "status quo."

Humo hakuwezi kuwa na nafasi ya ubaguzi wa kivyama, kikabila, kikanda, kidini, kimkoa, nk.

Humo watakuwamo ma CCM, Chadema, ACT, CHAUSTA, CHAUMA, UDP, CUF nk.

Humo watakuwamo watanganyika kwa wazanzibari, wasukuma, wachaga, wahaya, wandengereko, nk.

Humo watakuwamo wamatumbi, waarabu, wahindi, nk.

Kwamba kinachotukutanisha sote pamoja ni kiu ya kupata haki au kiu ya ukombozi wa nchi yetu dhidi ya dhuluma, nani anaweza kujidhania kuwa bora au mpambanaji zaidi kuliko nani?

Kwamba kumbe tunaweza kuwa na chuki na nani baina yetu hata kama kaongoka juzi?

Kwani yuko wapi anayefurahishwa na tekaji za watanzania wenzetu? Ni CCM, Nchimbi, Tulia au Samia?

Tuwapelekee mialiko washirika wetu wote hawa katika haki, kokote waliko. Tukapate kuwakemea watesi wetu katika umoja wetu. Nani asingependa kuujua ukweli? Nani anaweza kupinga umuhimu wa uchunguzi huru?

Kwamba nani asiyeuona umuhimu wa Sep. 23?

Pamoja na yote, tujiangalie wandugu kama tuna chuki na awaye yote katika jitihada hizi za ukombozi, bila kujua:

"Tunaweza kuwa wapigania ukombozi mamboleo tusiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili."
Wote tunawakaribisha ila tukiwa tunajua katika msafara wa mamba kenge watakuwa wengi kwa lengo lilelile ovu la kumwangamiza mamba kama anavyojaribu kenge kutenda kila iitwapo leo.
 
Wote tunawakaribisha ila tukiwa tunajua katika msafara wa mamba kenge watakuwa wengi kwa lengo lilelile ovu la kumwangamiza mamba kama anavyojaribu kenge kutenda kila iitwapo leo.

1. Kuwakaribisha ni hatua njema.

2. Kuwahukumu kwa lolote wasilosema wao moja kwa moja, ni kuendelea kuogelea kwenye dimbwi lile lile la matope bila kujitambua.

3. Kwenye ukombozi wa nchi tunaunganishwa na haki pekee si chuki dhidi ya watu, vyama, dini, kabila wala tabaka.

4. Kwamba wenye makasiriko ya kudumu ndiyo hawa tuliojazana humu?

5. Kwamba Wengine ndiyo wapiga ramli na imani zetu za kishirikina za usomaji watu na katikati ya mistari?

6. Ukweli mchungu pasi na kujitambua:

"Tunaweza kuwa wapigania ukombozi mamboleo tusiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili."

7. Bila kumung'unya maneno na kama asemavyo fahad singh post #2:

"Kwa chuki hizi, bado tupo tupo sana!"
 
imhotep, binti kiziwi, Zawadini na wale wapenzi wengine wa Mungu huu ni ukweli mwingine mchungu:

Tusipoangalia, bila kujua:

"Tunaweza kuwa wapigania ukombozi mamboleo tusiokuwa na mchango wowote kwa taifa hili."
Ni katika wale wanaoisubiria siku yenyewe. Ningependa kukumbusha tu:
1. Mapambano sio lelemama, hivyo watu waji/tujitayarishe.
2. Kwenye hili kuna machungu na matamu; tuwe na subira.
3. Nilishuhudia ya 27/1/2001. Yalikuwa ni mambo makubwa na ya kutisha sana. SUBIRA INAHITAJIKA sana.
4. Waswahili huwa tunasema "ukiona vyaelea, ujue vimeundwa" Hile historia tunaizungumza leo kwasababu ilitokea (iliundwa).
5. Sisi nasi tuunde ili vielee na wengine waje kuhadithia.

Niseme tu kwamba kwenye wengi kuna mengi. Tujifunze kwa hao wengi ili kupata uzoefu.
 
Ni katika wale wanaoisubiria siku yenyewe. Ningependa kukumbusha tu:
1. Mapambano sio lelemama, hivyo watu waji/tujitayarishe.
2. Kwenye hili kuna machungu na matamu; tuwe na subira.
3. Nilishuhudia ya 27/1/2001. Yalikuwa ni mambo makubwa na ya kutisha sana. SUBIRA INAHITAJIKA sana.
4. Waswahili huwa tunasema "ukiona vyaelea, ujue vimeundwa" Hile historia tunaizungumza leo kwasababu ilitokea (iliundwa).
5. Sisi nasi tuunde ili vielee na wengine waje kuhadithia.

Niseme tu kwamba kwenye wengi kuna mengi. Tujifunze kwa hao wengi ili kupata uzoefu.

Tunauthamini sana uzoefu wenu kutokea ng'ambo ya pili.

Proved, imhotep na wale waungwana wengine, ni wazi kuwa safari yetu si nyepesi.

Kwa namna yoyote tunauhitaji umoja wetu na wote wanaoweza kuwa nasi sasa kuliko wakati wowote kabla.

Penye nia ipo njia.
 
Back
Top Bottom