Tuwauze Wamachinga ughaibuni.

Tuwauze Wamachinga ughaibuni.

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Kama taifa, ninashauri tutengeneze mkakati mzuri wenye tija tuwauze Wamachinga nje ya nchi kama #nguvukazirahisi (wakafanye kazi zile ambazo ni labour intensive/mitulinga lakini wanaretain uraia wao wa Tz) ikiwa hatuna mpango maalum wa kuwatumia hapa nyumbani. Mbona Wachezaji wanauzwa! Korea Kusini Nannies alone walioko Middle East wanaiingizia nchi yao 30% ya GDP, Kenya diaspora wanaliingizia taifa 16% ya GDP kabla ya Corona kulipuka, Tz diaspora wanachangia kiasi gani cha GDP? Siyo kwamba diaspora ya Tz ni sawa na Wamachinga walio nje ya Tz? Kwasababu hatuna takwimu zao, hatujui wanachangia kiasi gani kwa pato la taifa ili tuzidi kuwafungulia wengine wapya waende nje? Taifa lije na mpango kabambe salama wa kuwauza Wamachinga (rasilimaliwatu) nje ya nchi kwa tija ya taifa. Naamini baadhi yetu walioko humu walio na white-colar occupations wataziacha na kukimbilia kuuzwa nje ya Tz kama Wamachinga pia (ikumbukwe kuna graduates wengi sana ni Wamachinga wakiwemo Masters Holders ambayo hii ni sawa na INTELLECTUAL ASSASSINATION), pia kuna baadhi yetu humu huenda tumewaajiri Wamachinga lakini tumekataa ku-declare interest kwenye mjadala huu. Kwenye dunia hii hii zipo nchi ambazo Commercial Sex is legalized, is it death sin tukicommercialize Umachinga ama ndani au nje ya nchi? Kuna wakati Tz diaspora walimuomba JPM wafadhili ujenzi wa Muungano Bridge kati ya bara na visiwani kama sehemu ya fadhila zao kwa taifa JPM hakuwakubalia, swali je, wangekuwa Wamachinga au hata Wafanyabiashara na Wafanyakazi hapa nyumbani wangekuwa na fedha za kujenga hilo daraja? What if kama tukizidisha kupeleka watu/Wamachinga officially kwenye diaspora si faida itaongezeka kwa taifa? Massive population pressure kwa nchi ambayo haina mpango jadidifu wa ku-utilize rasilimaliwatu ni hatari kwa nchi husika. (usichanganye hii na biashara ya utumwa bali zaidi ni labour-migration-protocol sort of) . Take this homework and bring the solutions for assessment.
 
Uko vizuri sana kwenye kujenga hoja ndugu msomi.

Ila waanze kwanza na suala la uraia pacha.

Hata huko nje lazima ujue kila nchi ina taratibu zake za kupokea watu, wengi watalenga taaluma fulani mfano uhandisi n.k na ujue sio kundi kubwa la wamachinga wenye hizo taaluma hivyo watauzika baadhi huku kundi kubwa tukibaki nalo.

Baada ya changamoto ya Covid-19 suala la ajira duniani kote limekua gumu kidogo hivyo hata kama tukiwauza nje ujue halitakuwa jambo la usiku mmoja huenda likachukua muda mrefu sana kuona tija yake.

Hata huko ughaibuni kuna sheria nyingi sana kwa Sasa za kudhibiti uhamiaji na wakimbizi (mfano Marekani na nchi za ulaya) hivyo kupata nchi utakakowauza hao wamachinga si rahisi hasa ukizingatia wengi wao ni nguvu kazi tu (japo wachache wana taaluma).

Nadhani suluhisho la kudumu lipo hapa hapa (japo si rahisi)...tuwape mbinu Bora za ujasiriamali, mikopo,mitaji (hasa kilimo cha kibiashara) vijana wetu kuliko kuwaacha kuwa wachuuzi tu.
 
Unadhani ughaibuni wanabeba beba tuu machokoraa?
South Korea wana Nannies Middle East wanaochangia 30% ya GDP ya South Korea. Wapo pia Nannies wa Kihindi na Kiafrika. Nannies siyo wasomi. Wamachinga wetu Tz wamo Masters Holders wengi tu.
 
Uko vizuri sana kwenye kujenga hoja ndugu msomi.

Ila waanze kwanza na suala la uraia pacha.

Hata huko nje lazima ujue kila nchi in taratibu zake za kupokea watu, wengi watalenga taaluma fulani mfano uhandisi n.k na ujue sio kundi kubwa la wamachinga wenye hizo taaluma hivyo watauzika baadhi huku kundi kubwa tukibaki nalo.

Baada ya changamoto ya Covid-19 suala la ajira duniani kote limekua gumu kidogo hivyo hata kama tukiwauza nje ujue halitakuwa jambo la usiku mmoja huenda likachukua muda mrefu sana kuona tija yake.
Ushauri wako mzuri sana, naukubali, ila tusiogope Mipango ya muda mrefu, hiyo ndiyo mizuri maana inatoa suluhisho la kudumu kuliko mipango ya zimamoto (dharura).
 
Siku hizi ughaibuni, mitulinga inafanywa na roboti. Roboti anafanya kazi masaa 24 hapumziki, hana njaa, hajisaidii, hachoki sasa wamachinga wa nini?
 
South Korea wana Nannies Middle East wanaochangia 30% ya GDP ya South Korea. Wapo pia Nannies wa Kihindi na Kiafrika. Nannies siyo wasomi. Wamachinga wetu Tz wamo Masters Holders wengi tu.
Ukosefu wa ajira ndounaopelekea watu kuingia mtaani tena hao machinga waliosambaa barabarani asilimia kubwa ndowenye mitaji ya 5m kwenda juu ambao hawakustaili kuitwa wamachinga
 
Siku hizi ughaibuni, mitulinga inafanywa na roboti. Roboti anafanya kazi masaa 24 hapumziki, hana njaa, hajisaidii, hachoki sasa wamachinga wa nini?
Rasilimaliwatu haijasitirika kwa ajili ya sekta moja tu ya uzalishaji hata na utoaji huduma. Nchi zenye teknolojia ya Robot duniani ziko ngapi? Ripoti ya vipimo vya maendeleo ya binadamu (Human Development Index) vya UN 2013 iliiweka Shelisheli katika kundi la juu sana (Very High Human Development Category) la maendeleo ya binadamu ikishika nafasi ya 46 ikiwa nchi pekee ya Afrika iliyoingia kundi hilo ikiacha kwa mbali nchi nyingi za mabara ya Ulaya na Amerika. Shelisheli haina teknolojia ya Robot katika kupaisha maendeleo ya binadamu.
 
Ukosefu wa ajira ndounaopelekea watu kuingia mtaani tena hao machinga waliosambaa barabarani asilimia kubwa ndowenye mitaji ya 5m kwenda juu ambao hawakustaili kuitwa wamachinga
Umachinga ni ajira hiyo, serikali haiku-guarantee kukupa ajira kwa sababu haitengenezi ajira ila wewe ndiyo ujiajiri mwenyewe. Serikali imebaki kutoa ajira za kimkakati na za kipaumbele tu na zinazotambuka agenda pana ya maendeleo ya taifa. Aidha, kuhisi tu kwamba baadhi ya Wamachinga wana mitaji ya 5ml nadhani haitoshi, hatuwezi kuratibu changamoto za Umachinga kwa mitazamo tu kwamba wana hiki wana kile. Ili tuwajuwe vizuri tunahitaji kuwekeza muda na rasilimaliakili za kutosha kujuwa yafuatayo kwa tafiti za kutosha:-
1. Wako wangapi?
2. Nani ana ukubwa gani wa mtaji.
3. Wako wapi?
4. Wanafanya nini?
5. Kwa wakati gani?
6. Kwa muda gani tangu 1985?
7. Huko walipo ni sahihi kwa mujibu wa sheria za nchi kama za mipango miji endapo hakuna sheria inayowaratibu?
8. Mamlaka za mapato ya serikali zinawafikiaje? nk nk.
 
Rasilimaliwatu haijasitirika kwa ajili ya sekta moja tu ya uzalishaji hata na utoaji huduma. Nchi zenye teknolojia ya Robot duniani ziko ngapi? Ripoti ya vipimo vya maendeleo ya binadamu (Human Development Index) vya UN 2013 iliiweka Shelisheli katika kundi la juu sana (Very High Human Development Category) la maendeleo ya binadamu ikishika nafasi ya 46 ikiwa nchi pekee ya Afrika iliyoingia kundi hilo ikiacha kwa mbali nchi nyingi za mabara ya Ulaya na Amerika. Shelisheli haina teknolojia ya Robot katika kupaisha maendeleo ya binadamu.
Kwa hiyo unataka wamachinga waende shelisheli? Washelisheli wenyewe watakubali?
 
Kwa hiyo unataka wamachinga waende shelisheli? Washelisheli wenyewe watakubali?
Umeelewa vizuri maudhui ya mada/hoja? Natarajia huko kama Maasai mwenye kesi ambaye hakimu akimwambia haya jitetee yeye kwa uelewa wake mdogo anatafsiri kwamba kujitetea ni kuchomoka mbio kutoroka ili asifungwe jela.
 
Umeelewa vizuri maudhui ya mada/hoja? Natarajia huko kama Maasai mwenye kesi ambaye hakimu akimwambia haya jitetee yeye kwa uelewa wake mdogo anatafsiri kwamba kujitetea ni kuchomoka mbio kutoroka ili asifungwe jela.
Waende nchi gani sasa sema?
 
Waende nchi gani sasa sema?
Hahahaa mkuu Bepari, vipi unataka utangulie huko nini?! Wahi Uarabuni kwanza Ulaya baadaye mkuu. Mapapa wa fedha za mafuta Uarabuni watakugombania kama mpira wa kona kwenye lango la Simba. Joke! joke!
 
Juzi Kati England wamekosa madereva wa malori ya mafuta mpaka wakaita jeshi. Wangeagiza madereva kutoka bongo (nadhani nao ni RHD Kama Tzs) hata 20,000 wanapatikana ndani ya siku moja nafasi zinajaa.
Mtani kumbe na wewe uliiona hiyo! Kwani Uingereza Robot haziwezi kuendesha malori? Jeez!
 
Mtani kumbe na wewe uliiona hiyo! Kwani Uingereza Robot haziwezi kuendesha malori? Jeez!
Robot Tena. Pangekuwa na uwezekano madereva wakakutana na balozi wa UK hapa nchini ili kumweleza utayari wa kujaza nafasi huko UK hata kwa miezi 6 tu. Mtoa mada kaongea la maana Sana, Tz Kuna rasilimali watu kubwa Sana haitumiki.
 
Robot Tena. Pangekuwa na uwezekano madereva wakakutana na balozi wa UK hapa nchini ili kumweleza utayari wa kujaza nafasi huko UK hata kwa miezi 6 tu. Mtoa mada kaongea la maana Sana, Tz Kuna rasilimali watu kubwa Sana haitumiki.
Hata Ubalozi wetu UK ungechangamkia fursa hiyo bila kusubiri kuzinduliwa usingizini na mtu.
 
Kama taifa, ninashauri tutengeneze mkakati mzuri wenye tija tuwauze Wamachinga nje ya nchi kama #nguvukazirahisi (wakafanye kazi zile ambazo ni labour intensive/mitulinga lakini wanaretain uraia wao wa Tz) ikiwa hatuna mpango maalum wa kuwatumia hapa nyumbani. Mbona Wachezaji wanauzwa! Korea Kusini Nannies alone walioko Middle East wanaiingizia nchi yao 30% ya GDP, Kenya diaspora wanaliingizia taifa 16% ya GDP kabla ya Corona kulipuka, Tz diaspora wanachangia kiasi gani cha GDP? Siyo kwamba diaspora ya Tz ni sawa na Wamachinga walio nje ya Tz? Kwasababu hatuna takwimu zao, hatujui wanachangia kiasi gani kwa pato la taifa ili tuzidi kuwafungulia wengine wapya waende nje? Taifa lije na mpango kabambe salama wa kuwauza Wamachinga (rasilimaliwatu) nje ya nchi kwa tija ya taifa. Naamini baadhi yetu walioko humu walio na white-colar occupations wataziacha na kukimbilia kuuzwa nje ya Tz kama Wamachinga pia (ikumbukwe kuna graduates wengi sana ni Wamachinga wakiwemo Masters Holders ambayo hii ni sawa na INTELLECTUAL ASSASSINATION), pia kuna baadhi yetu humu huenda tumewaajiri Wamachinga lakini tumekataa ku-declare interest kwenye mjadala huu. Kwenye dunia hii hii zipo nchi ambazo Commercial Sex is legalized, is it death sin tukicommercialize Umachinga ama ndani au nje ya nchi? Kuna wakati Tz diaspora walimuomba JPM wafadhili ujenzi wa Muungano Bridge kati ya bara na visiwani kama sehemu ya fadhila zao kwa taifa JPM hakuwakubalia, swali je, wangekuwa Wamachinga au hata Wafanyabiashara na Wafanyakazi hapa nyumbani wangekuwa na fedha za kujenga hilo daraja? What if kama tukizidisha kupeleka watu/Wamachinga officially kwenye diaspora si faida itaongezeka kwa taifa? Massive population pressure kwa nchi ambayo haina mpango jadidifu wa ku-utilize rasilimaliwatu ni hatari kwa nchi husika. (usichanganye hii na biashara ya utumwa bali zaidi ni labour-migration-protocol sort of) . Take this homework and bring the solutions for assessment.
Ugaibuni hawanunui vitu visivyo na viwango!!! Hata wabunge wenu huwezi kuwauza huko
 
Ugaibuni hawanunui vitu visivyo na viwango!!! Hata wabunge wenu huwezi kuwauza huko
Sawa tu, ni uhuru wa maoni unaochagizwa na kiwango cha uelewa, madhali usivunje sheria. Katiba ya JMT 1977 Ibr 18 kama ilivyorekebishwa 2005.
 
Back
Top Bottom