Tuwe makini na mafundi hasa kwenye ubadilishaji wa spare na oil

Tuwe makini na mafundi hasa kwenye ubadilishaji wa spare na oil

kingjohn255

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
400
Reaction score
513
Nianze uzi huu kwa kutambua uwepo wa watu mbalimbali na wenye ufundi na ujuzi wa kila aina. Kuna kitu bado wamiliki wa magari wanashindwa kukielewa pale ambapo wamekuwa wakipeleka gari zao kwa mafundi kubadilishiwa oil na baadhi ya vipuri lakini katika utafiti wangu mdogo kwenye swala la oil na vipuri nimegundua wamiliki wanapigwa sana.

Maana unakuta wewe umemwamini fundi umemwachia gari akubadilishie oil na unamwambia kabisa niwekee oil Fulani lakini atakachokifanya kwa vile oil ile bei yake imesimama kidogo atamuwekea oil hizi maarufu za kupima ambazo bei yake kwa dumu la litre 5 linauzwa 25,000 na hazina ubora wa kuaminika na ile inayobakia anachukua.

Wewe ukija ukitumia wiki moja tu unaanza kusikia gari inaunguruma kivingine baadae unaanza kulaum oil hii mbona nimeweka juzi lakini hadi saa hii sioni muungurumo ule wa gari! Itoshe kusema ukimpelekea fundi hasa kubadilisha oil na oil filter naomba usimamie gari yako na oil nenda mwenyewe dukani ununue umpelekee na sio kununuliwa na mafundi naona wengi wanavyopigwa hivyo nimekosa uvumilivu nimeona niwasemee but naomba mafundi mnaofanya hivyo mnisamehe.
 
Mimi huwa nikienda kufanya service huwa nakomaa na mafundi na kujua wanatoa nini na kwanini. Ni njia nzuri ya kujifunza pia na wao watakufanyia kazi yako vizuri
Ukitaka fundi umkomeshe mwambie naomba nipate rist ya bei uliyonunulia oil hapo utakua umemkomoa maana hakuna muuzaji atakaetoa rist ya EFD kwa kitu ambacho hajakiuza.
 
Kama uliweza kununua gari, unashindwaje kununua spare au maintanance items wewe mwenyewe?

Unapata kuna mtu hajui gari yake inatumia oil gani na litre ngapi, ama hajui size za magurudumu, hajui habari za coolant n.k

Mi naona watu wa hivi wapigwe tu hakuna jinsi
 
Kama uliweza kununua gari, unashindwaje kununua spare au maintanance items wewe mwenyewe?

Unapata kuna mtu hajui gari yake inatumia oil gani na litre ngapi, ama hajui size za magurudumu, hajui habari za coolant n.k

Mi naona watu wa hivi wapigwe tu hakuna jinsi
Kiongozi mimi nawaona hao wamiliki wanavyopigwa kuna hizi dumu za total na castrol zinatafutwa kama hazina akili nzuri na baadhi ya wauzaji wa oil nao wamekua sio waaminifu wanachukua Yale madumu tupu wanajaza oil za kupima wanaweka dukani mteja akija anauziwa oil nyingine na dumu linasomeka castrol au total kwa bei rahisi kabisa jaman ukiona hizo oil bei yake ni tofaut na iliyoko sokoni kuwa na mashaka nayo muulize yeye ananunua wapi hadi iwe rahisi kuliko wengine?
 
Kiongozi mimi nawaona hao wamiliki wanavyopigwa kuna hizi dumu za total na castrol zinatafutwa kama hazina akili nzuri na baadhi ya wauzaji wa oil nao wamekua sio waaminifu wanachukua Yale madumu tupu wanajaza oil za kupima wanaweka dukani mteja akija anauziwa oil nyingine na dumu linasomeka castrol au total kwa bei rahisi kabisa jaman ukiona hizo oil bei yake ni tofaut na iliyoko sokoni kuwa na mashaka nayo muulize yeye ananunua wapi hadi iwe rahisi kuliko wengine?

Ndio uduanzi huu huu nautaja mkuu...
Castrol inauzwa fuel stations za BP/Puma..
Total inauzwa kwa fuel stations za Total...
Unapata mtu anaenda hizo sehemu kujaza wese tu na asinunue oil zao
 
Best solution ni kuomba list ya vitu vya kubadilishwa, ingia dukani mwenyewe nunua mletee...

Msimamie akibadilisha...

Usimbane kwenye pesa yake ya ufundi hatakuumiza...


Cc: mahondaw
 
Tatizo letu hatupeani taarifa hili wengine wajue na waache kwenda hio sehemu. Sehemu yoyote inayotoa uduma mbovu dawa yake nibkuacha kwenda mpaka biashara yake ife.

Wengi wanaona kupewa/ kutoa uduma mbovu ni sawa tu.
 
Tatizo letu hatupeani taarifa hili wengine wajue na waache kwenda hio sehemu. Sehemu yoyote inayotoa uduma mbovu dawa yake nibkuacha kwenda mpaka biashara yake ife.

Wengi wanaona kupewa/ kutoa uduma mbovu ni sawa tu.
Hapa suluhisho ni kuchukua kifaa husika dukani na kwenda kumpa fundi abadilishe na wewe ukiwepo mfn kuna wenye magari wengine hawapend ubabaishaj mfano unamkuta anapenda kuweka oil filter genuine na oil may be ya castrol total or oryx lkn akishanunua hivyo vitu akimpa fund havibadilishw badala yake ataenda dukan atachukua oil filter ya Osaka na oil za kupima baadae vile vitu ataenda dukani atauza kwa hasara na atapata faida juu
 
Best solution ni kuomba list ya vitu vya kubadilishwa, ingia dukani mwenyewe nunua mletee...

Msimamie akibadilisha...

Usimbane kwenye pesa yake ya ufundi hatakuumiza...


Cc: mahondaw
Wamiliki wengine wenye magari wabishi huwezi kumwambia kitu kuhusu fundi wake yeye anachojua ni kuacha gari na kutengenezewa kumbe anaacha gari kuongezewa ugonjwa mkubwa zaidi
 
Wamiliki wengine wenye magari wabishi huwezi kumwambia kitu kuhusu fundi wake yeye anachojua ni kuacha gari na kutengenezewa kumbe anaacha gari kuongezewa ugonjwa mkubwa zaidi
Na kinachotugharimu Watanzania ni hii kusema, "Mimi fundi wangu kasema..."
Fundi wangu maana yake nini?
Mimi huwa naenda kwa fundi na kumwambia fungua hiki weka hiki coz nimegundua mafundi wengi wanabahatisha.
Magari ya siku hizi yanataka vipimo.
 
Kuna maduka wanayakua wanatoa oil fake na risiti wanakupa vizuri kabisa [emoji1787][emoji23]
Ukitaka fundi umkomeshe mwambie naomba nipate rist ya bei uliyonunulia oil hapo utakua umemkomoa maana hakuna muuzaji atakaetoa rist ya efd kwa kitu ambacho hajakiuza
 
Kuna maduka wanayakua wanatoa oil fake na risiti wanakupa vizuri kabisa [emoji1787][emoji23]
Hiyo nayo changamoto kweli kweli lakini Mimi nimegundua asilimia 90% ukikuta muuza oil ana uza zile oil za kupima ndg yangu kuwa makini hata hiyo unayonunua pengine imetolewa kwwnye hizo za kupima ila maduka wanayouza genuine wanaonekana tu huwez kukuta oil hizo
 
Ukitaka fundi umkomeshe mwambie naomba nipate rist ya bei uliyonunulia oil hapo utakua umemkomoa maana hakuna muuzaji atakaetoa rist ya efd kwa kitu ambacho hajakiuza
Bro bado hauko salama kiasi unachokifikiria wewe dawa ni kununua spare wewe mwenyewe na kumsimamia fundi wako uso kwa macho hasa kipindi hiki hali imekuwa ngumu wengi uaminifu wameuweka kando kidogo.

Mimi na-deal na mambo hayo, oils na spare so jamaa ninayefahamiana naye anaweza kuja kwangu kishkaji bwana nisaidie receipt ya 120K hii ndo bei wengi mnaonunua oil ya Toyota huko mitaani sharti nalompa ni yeye kuilipia VAT basi so uki-calculate hapo bei na bei ya hizi oil za kupima na VAT huyu fundi hakosi 35,000/= ukimpa na ufundi akitengeneza 45K yake hajakaa vibaya.

Ongezeni umakini kwenye vyombo vyenu hakuna usalama tena kwa mafundi mliokuwa mnawaamini.
 
@Sir_Mimi,Hata Mimi nadeal na biashara hiyo lakini kwangu uwe nakufahamu au sikufahamu huwaga sitoi risiti ya aina yoyote kama hujanunua kwangu mzigo. Hivyo ni hatua nzuri ya kuwakazia kuwa na umuhimu wa kujali chombo cha mwenzake but kiukweli mafundi ni pasua kichwa sana kwa wateja wao maana wakiaminiwa wenyewe hawaaminiki lazima wamlize tu mwenye chombo.
 
Kama uliweza kununua gari, unashindwaje kununua spare au maintanance items wewe mwenyewe?

Unapata kuna mtu hajui gari yake inatumia oil gani na litre ngapi, ama hajui size za magurudumu, hajui habari za coolant n.k

Mi naona watu wa hivi wapigwe tu hakuna jinsi
Pengine ndio marayake ya kwanza kumiliki gari naye unashauri apigwe tuu??
 
Na kinachotugharimu Watanzania ni hii kusema, "Mimi fundi wangu kasema..."
Fundi wangu maana yake nini?
Mimi huwa naenda kwa fundi na kumwambia fungua hiki weka hiki coz nimegundua mafundi wengi wanabahatisha.
Magari ya siku hizi yanataka vipimo.
Fundi anakwambia sina muda labda uiache urudi baadae au ukae masaa 6
 
Back
Top Bottom