Tuwe makini na mitungi ya gesi

Tuwe makini na mitungi ya gesi

Lugano Edom

Senior Member
Joined
Dec 2, 2021
Posts
122
Reaction score
186
Ndugu zangu,

Kwa wale mnaonunua gesi ya kupikia kwa kutumia njia ya usafiri wa bodaboda,kuweni makini sana hasa pale mtungi wa gesi unaposhushwa kwenye pikipiki.

Inashauriwa tuacheni dakika chache ili gesi itulie kabla ya kuikonekti kwenye jiko na kutumia. Ni kama chupa iliyojaa soda halafu unaitikisa kabla ya kuifungua.

Ni siku mbili zilizopita jamaa yangu alipatwa na mkasa mbaya wa mkewe kuungua na gesi kwa kiwango cha asilimia 25 na baadae kupoteza maisha baada ya kuagiza gesi na kuletewa kwa bodaboda na kuikonekti hapo kwa hapo na kuwasha jiko ili atumie. Ilimlipukia usoni mwake na kuungua. Alikuja kufia hospitalini baadae.

Jaribu kuisambaza taarifa hii kwa uwapendao, unaweza kuokoa maisha ya watu wengi na ukabarikiwa👏🏼👏🏼
 
Ndugu zangu,
Kwa wale mnaonunua gesi ya kupikia kwa kutumia njia ya usafiri wa bodaboda,kuweni makini sana hasa pale mtungi wa gesi unaposhushwa kwenye pikipiki.Inashauriwa tuacheni dakika chache ili gesi itulie kabla ya kuikonekti kwenye jiko na kutumia.
Ni kama chupa iliyojaa soda halafu unaitikisa kabla ya kuifungua.
Ni siku mbili zilizopita jamaa yangu alipatwa na mkasa mbaya wa mkewe kuungua na gesi kwa kiwango cha asilimia 25 na baadae kupoteza maisha baada ya kuagiza gesi na kuletewa kwa bodaboda na kuikonekti hapo kwa hapo na kuwasha jiko ili atumie.Ilimlipukia usoni mwake na kuungua.Alikuja kufia hospitalini baadae.

Jaribu kuisambaza taarifa hii kwa uwapendao,Unaweza kuokoa maisha ya watu wengi na ukabarikiwa👏🏼👏🏼
Asante kwa tarifa
 
Nadhani kulikuwa na sababu nyingine. Mitungi mingi Ina kitu kinaitwa Safety switch. Kama gasi inazidi kipimo kwa sababu yoyote ile, switch uwa inafunguka na kuachia ile ziada.
 
Back
Top Bottom