Tuwe makini na vyakula vya njiani,yamemkuta huyu jamaa!

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Kuna jirani yangu hapa katoka kazini kafika Sinza mori akakuta pweza basi akala pweza wa buku na kachori za mia tano! Akaomba na supu ya pweza ya mia tatu akashushia!

Baadae kaelelekea nyumbani kwake kamkuta mkewe akamuomba maji ya kunywa alipopewa akayanywa kisha akavua viatu, mkewe akamtengea maji ya kuoga baada ya kuoga akawa anapitia madaftari ya wanae, alipomaliza akajumuika na familia kula Chakula cha usiku kisha wakalala huku wamefunga milango yote.

Asubuhi kaamka, baada ya kuoga kavaa vizuri tu kaenda kazini... kwa ujumla Yuko vizuri katika kazi na anapiga kazi kama kawaida.

Kiufupi jamaa kanisimulia pweza walinoga sana.

The wish was usikie Habari mbaya! Ila ndo hivyo haijawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…