Papa Francis akutwa na Nimonia

Papa Francis akutwa na Nimonia

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Vatican imethibitisha kuwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis ameugua nimonia (bilateral pneumonia) hali inayohusisha maambukizi kwenye mapafu yote mawili.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Vatican Madaktari wake wamebaini ugonjwa huo baada ya vipimo vya kitabibu na kwa sasa anapatiwa matibabu maalum huku hali yake ikiwa chini ya uangalizi wa karibu.

Papa Francis mwenye umri wa miaka 87 amekuwa na changamoto za kiafya kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na matatizo ya kupumua na maumivu ya mifupa hata hivyo Vatican imesisitiza kuwa anaendelea kupokea huduma bora za kitabibu na anaendelea vizuri matibabu.

Maelfu ya Waumini wa Kanisa Katoliki duniani kote wameendelea kumuombea afya njema huku Viongozi wa dini na Viongozi wa mataifa wakionesha mshikamano na kumtakia ahueni ya haraka.
#MillardAyoUPDATES

Screenshot_20250219-140120_1.jpg
 
Back
Top Bottom