Tuzisaidie Shule za Msingi Zilizo Jirani na Maeneo Tunayoishi

Tuzisaidie Shule za Msingi Zilizo Jirani na Maeneo Tunayoishi

Sabi Sanda

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
409
Reaction score
31
Watanzania Wenzangu,

Naomba tuanzishe utaratibu wa kuzitembelea mara kwa mara shule za msingi za umma ambazo ziko jirani na maeneo tunayoishi. Lengo kuu liwe ni kujenga uhusiano na ushirikiano wa karibu na walimu wa shule husika pamoja na kamati za shule na kuona ni kwa jinsi gani tunaweza kuunganisha nguvu zetu pamoja ili kuinua na kuimarisha taaluma katika shule zetu za msingi za umma.
 
kwani kodi tunayolipa inafanya kazi gani.?

Asante kwa swali ulilouliza. Kivitendo tatizo kubwa katika nchi yetu ni kuwa elimu si kipaumbele. Huo ndiyo ukweli kutokana na hali halisi ilivyo. Utakapoitembelea shule iliyo jirani nawe si lazima sana uisaidie kifedha. Ushauri na kujenga hamasa ya kusoma kwa bidii na kwa malengo ni muhimu sana kwa watoto wetu walioko katika shule zetu za msingi.

Kwa mfano, Tebo za Kuzindisha ni tatizo kubwa sana katika shule zetu za msingi. Kazi ya ziada inatakiwa kufanywa ili kuhakikisha kuwa vijana wetu wanakuwa mahiri katika eneo hili na masomo yao yote kwa ujumla.
 
Watanzania Wenzangu,

Naomba tuanzishe utaratibu wa kuzitembelea mara kwa mara shule za msingi za umma ambazo ziko jirani na maeneo tunayoishi. Lengo kuu liwe ni kujenga uhusiano na ushirikiano wa karibu na walimu wa shule husika pamoja na kamati za shule na kuona ni kwa jinsi gani tunaweza kuunganisha nguvu zetu pamoja ili kuinua na kuimarisha taaluma katika shule zetu za msingi za umma.

Wazo zuri sana Mtanzania mwenzangu. Nadhani uzalendo huu upanuliwe na usiishie kwenye Taaluma tu. Unaweza kuongezea Michezo kwa Wanafunzi na mbinu mbalimbali za kuinua uchumi kwa Waalimu.
Mfano, Miaka michache iliyopita nikiwa Mkoa wa Shinyanga nilihamasisha na kuwajengea uwezo Waalimu wa Shule moja ya Sekondari hadi wakaanzisha Kikundi cha HISA kilichojumuisha baadhi ya Waalimu, baadhi ya Wafanykazi wasio Waalimu katika Shule hiyo na baadhi ya Wazazi. Mafanikio yalikuwa makubwa na mengi yakiwemo kupunguza kwa kiasi hulka ya Waalimu kukopa kwa "Loan Sharks" wa mitaani kwa dhamana ya Kadi zao za Benki, kuwawezesha Waalimu kufungua Miradi yao midogomidogo ikiwemo Kilimo na ufugaji wa Kuku, kuwaunganisha Waalimu na Wazazi na mwisho wa mwaka kugawana HISA na Faida iliyowawezesha baadhi yao kulipia Ada za Shule za Watoto wao. Mafanikio ya Kikundi hicho kwa Mwaka wa Kwanza yalisababisha kuundwa kwa Kikundi kingine hapo Shuleni. Leo ni Mwaka wa tatu, ninaamini wanaendela vizuri.

A happy Teacher is a Productive Teacher!

NB. Nilianzisha vilevile Kikundi kama hicho, cha HISA, kwa Manesi wa Hospitali ya Serikali.

Hivi sasa ninaishi kama viwanja/nyumba kumi kutoka Shule ya Msingi ya Serikali. Kutokana na wazo lako nitaonana na Mwalimu Mkuu tuone namna ninavyoweza kusaidia - kujitolea kwa masaa mawili kwa Wiki sio hasara.

Pamoja Tunaweza!
 
Wazo zuri sana Mtanzania mwenzangu. Nadhani uzalendo huu upanuliwe na usiishie kwenye Taaluma tu. Unaweza kuongezea Michezo kwa Wanafunzi na mbinu mbalimbali za kuinua uchumi kwa Waalimu.
Mfano, Miaka michache iliyopita nikiwa Mkoa wa Shinyanga nilihamasisha na kuwajengea uwezo Waalimu wa Shule moja ya Sekondari hadi wakaanzisha Kikundi cha HISA kilichojumuisha baadhi ya Waalimu, baadhi ya Wafanykazi wasio Waalimu katika Shule hiyo na baadhi ya Wazazi. Mafanikio yalikuwa makubwa na mengi yakiwemo kupunguza kwa kiasi hulka ya Waalimu kukopa kwa "Loan Sharks" wa mitaani kwa dhamana ya Kadi zao za Benki, kuwawezesha Waalimu kufungua Miradi yao midogomidogo ikiwemo Kilimo na ufugaji wa Kuku, kuwaunganisha Waalimu na Wazazi na mwisho wa mwaka kugawana HISA na Faida iliyowawezesha baadhi yao kulipia Ada za Shule za Watoto wao. Mafanikio ya Kikundi hicho kwa Mwaka wa Kwanza yalisababisha kuundwa kwa Kikundi kingine hapo Shuleni. Leo ni Mwaka wa tatu, ninaamini wanaendela vizuri.

A happy Teacher is a Productive Teacher!

NB. Nilianzisha vilevile Kikundi kama hicho, cha HISA, kwa Manesi wa Hospitali ya Serikali.

Hivi sasa ninaishi kama viwanja/nyumba kumi kutoka Shule ya Msingi ya Serikali. Kutokana na wazo lako nitaonana na Mwalimu Mkuu tuone namna ninavyoweza kusaidia - kujitolea kwa masaa mawili kwa Wiki sio hasara.

Pamoja Tunaweza!

Asante sana kwa feedback nzuri uliyotupatia, kwa ushauri ulioutoa na kwa juhudi zako ambazo umekuwa ukizifanya katika kusaidia Watanzania wenzako kujijengea uwezo na kuweza kusimama wenyewe. Hongera sana. Pia nakushukuru sana kwa kulipokea hilo wazo na kwa uamuzi wako wa kuonana na mkuu wa Shule ya Msingi iliyo jirani nawe. Tutashukuru sana kupata mrejesho toka kwako.

 
Kuzitembelea shule za msingi zilizo jirani nasi na kushiriki katika kuboresha taaluma katika shule hizo yapasa kuwa moja ya majukumu yetu muhimu kama Watanzania. Kijana aliyepata elimu bora ya msingi na kupatiwa muongozo mzuri ana uhakika wa kufika mpaka ngazi ya chuo kikuu na kuweza kutimiza ndoto zake maishani.
 
Back
Top Bottom