ndunajr
Senior Member
- Apr 28, 2015
- 174
- 191
Habarini wanajamvi,
Kichwa cha habari hapo juu ndicho kinabeba maneno yangu humu ndani. Ni kwamba Napata masikitiko makubwa sana juu ya hizi timu zetu hasa zinazoshiriki Ligi Kuu. Jana Simba na Majimaji zimecheza mechi ya mwisho katika mzunguko wa kwanza na timu yetu ya nyumbani Ruvuma na wanalizombe kutoka pale Songea mjini wakala nne bila; sikushangaa.
Maana yake siku tatu mpaka ile siku ya mechi walipangiwa kufikia Hotel moja hivi yaitwa Kilimanjaro ipo Tandika mtaa wa bububu aka Tandika maghorofani, hotel nzuri na kibwagizo tu ni sehemu ya machinjio ya wake za watu pale aah hatari.
Lakini kilichonistua mpaka kuandika hapa ni mtindo wa maisha wachezaji wanayoishi mmmhhhh aibu sana na ndo maana wachezaji wetu hawaheshimiki.
CHAKULA
Wachezaji wa Majimaji kwa siku tatu mfululizo walikuwa wanakula chakula cha mama Ntilie anaitwa Mama Mudy. Ni chakula ambacho mimi nilikula mara moja na kuapa Mungu nisaidie sitokula tena. Chakula nyama ajinamoto, wali hamira, kipande cha nyama kimoja dagaa kama watano mchicha daaa kiduuchu sahani bei 1500/=. Nami nina kaduka kangu ka soda na maji aahh wameniungishaaa. Sasa hebu niambie mimi tu kapuku msosi ule jinsi ulivyo kula mtihani halafu leo uwende ukawape wachezaji ambapo humo ndio ukatoe timu ya Taifa aaaaah samahanini jamani.
Nje ya Hotel sasa kuna duka sisi tunapaita Frem mpya bia zinauzwa hapo hatari eeeh bwana ule usiku kesho tunaamkia mechi ohoooo jamaa wanagonga monde hatari Jerryson Tegete anakula pombe hatari wamekunywa pombe wale watu hatari afu eti kesho unaingia uwanjani kucheza na Simba kwanini usifungwe?
Watu wakawa wanashangaa mabeki wanavyoanguka anguka tu uwanjani, kwa sisi tulioona yale maisha ndani ya siku tatu zile hatukushangaa wale wachezaji kukosa nguvu.
TUZITUNZE HIZI TIMU JAMANI, kweli chakula kwa MAMA MUDY!!!??? wadhamini wapo kweli???
Kichwa cha habari hapo juu ndicho kinabeba maneno yangu humu ndani. Ni kwamba Napata masikitiko makubwa sana juu ya hizi timu zetu hasa zinazoshiriki Ligi Kuu. Jana Simba na Majimaji zimecheza mechi ya mwisho katika mzunguko wa kwanza na timu yetu ya nyumbani Ruvuma na wanalizombe kutoka pale Songea mjini wakala nne bila; sikushangaa.
Maana yake siku tatu mpaka ile siku ya mechi walipangiwa kufikia Hotel moja hivi yaitwa Kilimanjaro ipo Tandika mtaa wa bububu aka Tandika maghorofani, hotel nzuri na kibwagizo tu ni sehemu ya machinjio ya wake za watu pale aah hatari.
Lakini kilichonistua mpaka kuandika hapa ni mtindo wa maisha wachezaji wanayoishi mmmhhhh aibu sana na ndo maana wachezaji wetu hawaheshimiki.
CHAKULA
Wachezaji wa Majimaji kwa siku tatu mfululizo walikuwa wanakula chakula cha mama Ntilie anaitwa Mama Mudy. Ni chakula ambacho mimi nilikula mara moja na kuapa Mungu nisaidie sitokula tena. Chakula nyama ajinamoto, wali hamira, kipande cha nyama kimoja dagaa kama watano mchicha daaa kiduuchu sahani bei 1500/=. Nami nina kaduka kangu ka soda na maji aahh wameniungishaaa. Sasa hebu niambie mimi tu kapuku msosi ule jinsi ulivyo kula mtihani halafu leo uwende ukawape wachezaji ambapo humo ndio ukatoe timu ya Taifa aaaaah samahanini jamani.
Nje ya Hotel sasa kuna duka sisi tunapaita Frem mpya bia zinauzwa hapo hatari eeeh bwana ule usiku kesho tunaamkia mechi ohoooo jamaa wanagonga monde hatari Jerryson Tegete anakula pombe hatari wamekunywa pombe wale watu hatari afu eti kesho unaingia uwanjani kucheza na Simba kwanini usifungwe?
Watu wakawa wanashangaa mabeki wanavyoanguka anguka tu uwanjani, kwa sisi tulioona yale maisha ndani ya siku tatu zile hatukushangaa wale wachezaji kukosa nguvu.
TUZITUNZE HIZI TIMU JAMANI, kweli chakula kwa MAMA MUDY!!!??? wadhamini wapo kweli???