Tuzungumzie fursa zilipo maeneo yetu, mikoani na wilayani ulipo

Mimi nipo korogwe
 
nipo jiji la miamba

kuna fursa za kila aina

(¡) Biashara ya samaki & dagaa
(¡¡) minada mikubwa ya mifugo ikiwemo
mbuzi , ng'ombe, kondoo, bata, kuku, kanga nk
(¡¡¡) Mazao ya kilimo & matunda

matunda ni kama ndizi na parachichi
mazao ni kama maharage na udaga (unga wa muhogo)

zipo fursa pia za madin nk

yeyote mwenye uhitaji wa kujua zaid fursa zilizopo Mwanza ani PM
 
Wabongo hua hatupend kupeana madili ili tufanikiwe sote..hii nafsi itatusumbua San...
Shida sio ubinafsi , shida ni kupenda kulaum bila hata sababu.

Iringa &Njombe , Kuna viwanda vya nguzo.

Na marine boards.

Kwa nguzo : 20000tsh@manunuzi.
1000tsh@kukata
500tsh kuchubua
Kuskidi Toka shambani 6000 kwa tractor
Jumla ndogo 27500 ×100= 2,750,000tsh
Kupakia @5000×100=500,000
Ushuru@5%=1000×100=100,000
Kuhakiki uzito 1,5000
Kupunguza ulefu 50,000
Kukodi gari 1,200,000
Jumla 1,8650,000+2,750,000=5,200,000

Mauzo 30×120,000=3,600,000
70×70,000 =4,900,000
Jumla. =Tsh8,500'000
Faida =3,200,000 -800,000 gharama nyinginezo , za uendeshaji

Guest , usafiri posho zahapa na pale hutokosa (2 m)

Changamoto.

a:Uaminifu kwenye kazi hiii kwa baazi yatu ni mdogo mno , ukikutana na mutu mbaya unauziwa Bora nguzo na sio nguzo Bora, ukizifikisha kiwandani utapata reject hazitonunuliwa.

Utaishia kukatika mtaji.

b:Bei zinabadilika badilika zinaweza kupanda aukushuka mda wowote.
c:Kuna baszi ya masoko huchelewesha malipo.

Mwenye maswali atajibiwa yasiwe nje ya mada hii ya nguzo na masoko yake.

Kuhusu plywood Au marine board , nitarejea.
 
Soko lake pa kuuzia hizo nguzo ni wapi?
Kwa tathmini yako unadhani nguzo 100 zinaweza kuuzwa na kuisha baada ya muda gani?
 
Soko lake pa kuuzia hizo nguzo ni wapi?
Kwa tathmini yako unadhani nguzo 100 zinaweza kuuzwa na kuisha baada ya muda gani?
100pcs , ni wastani wa trip 1. Hiyo ikifika kiwandani wanachukua zote. (Kama zinafaa) hata ukiweza kuandaa 1000 trip10 zote watachukua kwasiku 1.
 
100pcs , ni wastani wa trip 1. Hiyo ikifika kiwandani wanachukua zote. (Kama zinafaa) hata ukiweza kuandaa 1000 trip10 zote watachukua kwasiku 1.
PC 100 unazikusanya kwa mda gani?
 
PC 100 unazikusanya kwa mda gani?
Usipo kutana na vikwazo

Itakuchua 3-5 . truck pia ni changamoto kwa baazi ya masoko nayo itakuchua 2-3 , hapo umetafuta zile zakudandia.
Kupakia kwa kitumia watu kunamaliza ziku1 .

Kuanzia kuvuna hadi inafika kiwandani, wasitani 10 days
 
Tanga mjini au kipumbwi pangani au mkinga kuna fursa kubwa ya dagaa nyama ukitaka kuchemsha na kuuza au kununua na kuuza ni wewe tu dagaa hawa wanasoko sehemu yoyote ile ni watamu Sana kazi kwenu
Uono au
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…