TV Imaan itengewe bajeti kama TBC

TV Imaan inarusha vipindi vya kuelimisha jamii. Ingefaa itengewe fungu kila mwaka kwa ajili ya kutanua wigo wa Matangazo yake duniani.
Kweli, pia serikali itenge bajeti kwa ajili ya Arise & Shine TV ya Mwamposa ili watu wengi waponywe kwa jina la Yesu.
 
TV Imaan inarusha vipindi vya kuelimisha jamii. Ingefaa itengewe fungu kila mwaka kwa ajili ya kutanua wigo wa Matangazo yake duniani.
Itengewe fungu na nani? Si chombo cha serikali so wasitegemee pesa kutoka huko
 
TV Imaan inarusha vipindi vya kuelimisha jamii. Ingefaa itengewe fungu kila mwaka kwa ajili ya kutanua wigo wa Matangazo yake duniani.
ni wazo zuri sana,
nadhani wenye tv yao wakifanya hivyo itapendeza zaidi 🐒
 
Bodi ya Wakurugenzi waandike technical and financial proposal wawasilishe kwenye kamati ya bajeti kwa kujadiliwa. Kama Vyama vya upinzani wanapswa ruzuku kwann isiwe TV Imaan?
 
TV Imaan inarusha vipindi vya kuelimisha jamii. Ingefaa itengewe fungu kila mwaka kwa ajili ya kutanua wigo wa Matangazo yake duniani.
Hata hatujamaliza swala mmeanza kuleta vituko.
 
Bodi ya Wakurugenzi waandike technical and financial proposal wawasilishe kwenye kamati ya bajeti kwa kujadiliwa. Kama Vyama vya upinzani wanapswa ruzuku kwann isiwe TV Imaan?
Muwe mnajifunza kuiga mazuri ya majirani zenu ndugu zangu! Wenzenu Radio Maria kila siku wanakusanya fedha za kuendeshea redio yao, kupitia wasikilizaji wao!! Tena wasikilizaji wengine ni ndugu zako katika imaan!

Hivyo acheni kupenda mteremko ndugu zangu! Muwe mnaumiza vichwa wakati mwingine ili maisha nayo yaende.
 
TV Imaan inarusha vipindi vya kuelimisha jamii. Ingefaa itengewe fungu kila mwaka kwa ajili ya kutanua wigo wa Matangazo yake duniani.
Ukifungulia redio Maria unasikia michango ya redio yaani eneo lote inaposikilizwa wanachangia au Morning Star Redio ya wasabato hii ina fungu lake automatic huko kwenye makanisa yao, kila Sabato.

Sasa hii yetu Iman why ipewe budget na special?.

Kila muumini au msikiti ukiwekewa goal/target kwa week au mwezi mbona ni rahisi sana.

Labda tatizo liwe ile roho yetu ya kiafrika (uchoyo na roho mbaya) maana tunajuana tulivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…