Elections 2010 Twahitaji rais mhemea vibaba?- CCM na JK Tupatieni Jibu!

Elections 2010 Twahitaji rais mhemea vibaba?- CCM na JK Tupatieni Jibu!

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
434
'' Mimi nakwenda kule (ulaya na Marekani) kuhemea .Nikirudi narudi na Kibaba'',Kauli hiyo ilinikera kiasi cha kusababisha mapigo ya moyo kuongezeka,Kwa mtazamo wangu ,haya ni maneno ya ajabu kutamkwa na Rais wa Nchi kuliko mengine yote yaliyopatwa kutamkwa na kikwete, Hata yale kwamba wasichana wanaopata mimba shuleni ni kwa sababu ya viherehere vyao ,hayafikii hayo aliyoyatoa kwenye kampeni mkoani Mbeya

Je ?Twahitaji Rais Mhemea Vibaba?
 
Tafakuri Jadidi

mbwambo.jpg
Twahitaji rais mhemea vibaba?

Johnson Mbwambo
Septemba 15, 2010


"......Na tunapokuja kwenye suala la kuchokwa na wafadhili, nakumbuka nilipokuwa nimelazwa THI nilisoma, kwenye gazeti la Mwananchi, kauli moja ya Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati akihutubia mkutano wa kampeni huko Mbeya.

Kauli hiyo ilinikera kiasi cha kusababisha mapigo yangu ya moyo kuongezeka na kunifanya ghafla nizidiwe (tangu tukio hilo magazeti yakazuiwa kuingia wodini chumbani kwangu).

Kauli hiyo ni ile aliyoitoa kuwajibu wanaomshutumu kwamba anatumia mapesa mengi ya walipa kodi kufanya ziara nyingi za nje zisizo na ulazima. Alisema maneno mengi kuhalalisha ziara hizo, lakini yaliyoniacha hoi ni haya: “Mimi nakwenda kule (Ulaya na Marekani) kuhemea. Nikirudi narudi na kibaba.”

Kwa mtazamo wangu, haya ni maneno ya hovyo kutamkwa na rais wa nchi kuliko mengine yote yaliyopatwa kutamkwa na Kikwete. Hata yale kwamba wasichana wanaopata mimba shuleni ni kwa sababu ya viherehere vyao, hayafikii hayo aliyoyatoa kwenye kampeni mkoani Mbeya.

“Mimi nakwenda kule (Ulaya na Marekani) kuhemea. Nikirudi narudi na kibaba”, ni maneno ambayo ukiyatafakari utagundua kwamba yanatolewa na mtu anayeifurahia hali hiyo.

Ningemwelewa Kikwete kama angeueleza umati ule kwa hali ya kusikitisha kwamba sisi Watanzania tunamwangusha kwa sababu hatuchapi kazi vya kutosha; kiasi cha kufikia hatua ya kujitegemea, na hivyo tunamfanya ajidhalilishe kwa kwenda Ulaya na Marekani kuombaomba hata mambo ambayo tungeyamudu wenyewe kujitafutia.

Ningemwelewa Kikwete kama angeielezea hali hiyo kwa uchungu na kwa masikitiko, na hata kutisha kwamba hatakubali tena kwenda Ulaya na Marekani kuombaomba mambo ambayo sisi wenyewe tuna uwezo nayo (kama vile kutengeneza na kusambaza vyandarua vya bei nafuu).

Lakini sivyo alivyofanya kwenye hotuba hiyo. Kikwete aliitoa kauli hiyo kwa namna inayoonyesha kwamba anazifurahia ziara hizo za nje za kuomba misaada. Kwa maneno mengine, ujumbe wake kwa waliokuwa wanamsikiliza ulikuwa huu: “Nichagueni mimi; maana ni hodari wa kwenda nje kuhemea na kurudi na vibaba.”

Labda niwaulize Watanzania wenzangu: Je, tunamhitaji rais anayefurahia kutembeza bakuli la omba omba nje ya nchi au tunahitaji rais mwenye uwezo wa kutujengea misingi ya kujitegemea?

Je, kuna nchi dunia iliyopata kuendelea na kuondokana na umasikini kwa kutegemea misaada ya nje ya nchi? Je, ni familia gani duniani iliyopata kujikomboa kwenye umasikini inayoongozwa na baba ambaye kila kukicha hutembelea nyumba za majirani kuhemea vibaba vya unga kwa ajili ya ugali wa wanawe?

Ndugu zangu, tunapokuwa na rais wa nchi anayeona ni jambo la kawaida na linalofurahisha kwenda Ulaya na Marekani ‘kuhemea vibaba’, hatuwezi kamwe kujenga utamaduni wa kujitegemea.

Kwa hakika, rais wa namna hiyo huwa ana udhaifu mmoja mkubwa; nao ni kwamba si kiongozi visionary. Si kiongozi mwona mbali anayeifikiria Tanzania ya miaka 50 ijayo. Na si kuifikiria tu; bali kuweka misingi na mwelekeo wa kuifikia.

Najua kuwa wanayo hiyo wanayoiita vision 2025 iliyopo kabatini. Nadhani waliiandaa tu ili wakiulizwa kama wanayo wajibu ndio, lakini si kuifuata.

Kwa hiyo, mnapomchagua mtu asiye na vision kumiongoza, mjue kwamba mtapotea na mtatangatanga nyikani; maana hana uwezo wa kuiona njia itakayowatoa nyikani.

Labda nikumbushe kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere aliiona njia mapema na aliwaonyesha hawa kina Kikwete njia ya kutokea nyikani, lakini wameitelekeza, na ndiyo sababu tunatangatanga nyikani.

Naamini kwamba kama Kikwete na CCM yake ya sasa, ambayo imekumbatia mafisadi, atashinda uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, basi, tujue wazi kwamba tutakuwa tumejikatia tiketi nyingine ya miaka mingine mitano ya kutangatanga nyikani.

Nasema hivyo bila kupepesa kope; maana kiongozi anayefurahia ‘kuhemea vibaba’ Ughaibuni, hakika, si yeye wa kututoa nyikani.

Nihitimishe kwa kusema kwamba, kwa sasa, tunaweza kuikejeli siasa ya Ujamaa ya Mwalimu Nyerere, lakini ni upofu na ujinga kuitelekeza dhana yake ya Kujitegemea.

Ndugu zangu, Tutakuja kulipia kwa makosa hayo kama ambavyo tumeanza sasa ambapo tunasaidiwa hata vyandarua, na tunachekelea kwa hilo!

Huko mbele tutakuja kusaidiwa na Wazungu hata miswaki, na kwa ujinga wetu tutaendelea kuchekelea; huku wenzetu tuliokuwanao nyuma wakichanja mbuga kiteknolojia na kimaendeleo kiasi cha kufikia hata hatua ya kutuma vyombo anga za mbali!

Wakati wenzetu wengine tuliopata nao uhuru wakati mmoja sasa wana treni za kasi zinazotumia umeme, sisi hata reli aliyotuachia mkoloni inatushinda kuiendesha. Wakati wenzetu wana mashirika yao imara ya ndege ambayo ni alama ya taifa, sisi ATCL yetu iko taabani.

Kwa ufupi, tumepotea na tunahitaji kuitafuta njia aliyotuonyesha Nyerere. Kwa bahati mbaya CCM ya sasa haiwezi kuturejesha kwenye njia sahihi kwa sababu haina viongozi wenye vision japo ya miaka 50 au zaidi.

Ndiyo maana nasisitiza; Mtanzania yeyote mwerevu na mwona mbali (visionary) ataona kwamba rais tunayemhitaji na anayeifaa Tanzania yetu, ni yule anayetu....."alie na maono ya kuifanya Tanzania ijitegemee kwa kutumia rasilimali zetu tulizopendelewa na Mungu na sio anaetaka kutufanya wote tukahemee vibaba, badala ya kufanya kazi"'

Source: Raia Mwema
 
karibu j mbwambo, na pole sana na kuumwa, binafsi tulikumisis sana na makala zako za raia mwema,
 
Kibaba cha mchele, ama unga wa ugali kina maanisha nini? Acheni ulofa!
 
Ni aibu sana kuwa na rais anayepende kuomba omba wakati ameshindwa kusimamia vizuri ukusanyaji wa kodi kwa kudhibiti rushwa, ukwepaji na udanganyifu katika kukusanya kodi.
Ni aibu kuwa na rais anayetetea mafanikio ya ziara zake kwa kuorodhesha idadi ya misaada aliyopewa bila kufanya tahmni ya gharama alizotumi yeye na wasidizi wake.
 
Tafakuri Jadidi

mbwambo.jpg
Twahitaji rais mhemea vibaba?

Johnson Mbwambo
Septemba 15, 2010

"...... "Nichagueni mimi; maana ni hodari wa kwenda nje kuhemea na kurudi na vibaba."

-----

Nihitimishe kwa kusema kwamba, kwa sasa, tunaweza kuikejeli siasa ya Ujamaa ya Mwalimu Nyerere, lakini ni upofu na ujinga kuitelekeza dhana yake ya Kujitegemea.

Ndugu zangu, Tutakuja kulipia kwa makosa hayo kama ambavyo tumeanza sasa ambapo tunasaidiwa hata vyandarua, na tunachekelea kwa hilo!

Huko mbele tutakuja kusaidiwa na Wazungu hata miswaki, na kwa ujinga wetu tutaendelea kuchekelea; huku wenzetu tuliokuwanao nyuma wakichanja mbuga kiteknolojia na kimaendeleo kiasi cha kufikia hata hatua ya kutuma vyombo anga za mbali!

Wakati wenzetu wengine tuliopata nao uhuru wakati mmoja sasa wana treni za kasi zinazotumia umeme, sisi hata reli aliyotuachia mkoloni inatushinda kuiendesha. Wakati wenzetu wana mashirika yao imara ya ndege ambayo ni alama ya taifa, sisi ATCL yetu iko taabani.

Kwa ufupi, tumepotea na tunahitaji kuitafuta njia aliyotuonyesha Nyerere. Kwa bahati mbaya CCM ya sasa haiwezi kuturejesha kwenye njia sahihi kwa sababu haina viongozi wenye vision japo ya miaka 50 au zaidi.

Ndiyo maana nasisitiza; Mtanzania yeyote mwerevu na mwona mbali (visionary) ataona kwamba rais tunayemhitaji na anayeifaa Tanzania yetu, ni yule anayetu....."alie na maono ya kuifanya Tanzania ijitegemee kwa kutumia rasilimali zetu tulizopendelewa na Mungu na sio anaetaka kutufanya wote tukahemee vibaba, badala ya kufanya kazi"'

Source: Raia Mwema

Haya ni maneno mazito na yanamaana kubwa. Nayafananisha na yale maneno ya kwamba urais wangu hayana ubia na mtu yeyote halafu sasa tunaambiwa kuwa suala la urais wangu ni suala la familia na tumeona kwa jinsi mama na watoto wanavyopata mapokezi ya ki-falme kila wanakotembelea. Unaweza kufukuzwa au kupandishwa kazi kutokana na jinsi unavyojinyenyekeza kwa mama ama watoto wa rais. Hii ni hatari hasa pale watu hao ni wa akina Salma Kikwete.
 
TAFAKURI JADIDI

Nakala chapishi
Mtumie mwenzio
Jiandikishe utaarifiwe


Twahitaji rais mhemea vibaba?


Johnson Mbwambo
Septemba 15, 2010

NIANZE kwa kuwaomba radhi wasomaji wangu kwa safu hii kutochapishwa kwa zaidi ya mwezi mmoja. Sababu ni kwamba nilipata matatizo ya ugonjwa wa moyo yaliyosababisha nilazwe katika hospitali tatu tofauti; kuanzia TMJ na Tanzania Heart Institute (THI) za Dar es Salaam hadi Hospitali ya Apollo ya New Delhi, India. Namshukuru Mungu kwamba sasa hali yangu ya afya imetengemaa.

Naomba radhi pia kwamba nitaitumia sehemu ya safu hii, leo, kutoa shukurani zangu kwa wote walionisaidia, kwa njia moja au nyingine, katika kipindi hicho kigumu.

Naomba radhi kwa sababu, kimsingi, safu hii ni ya kujadili masuala ya nchi yanayotugusa sote, na si masuala ya mtu mmoja mmoja. Lakini kwa kuwa sina fursa nyingine muafaka ya kutoa shukrani zangu, nisameheni kwa kutumia kidogo sehemu ya safu hii kutoa shukrani hizo.

Shukrani zangu za kwanza ni kwa wafanyakazi wenzangu wote wa gazeti la Raia Mwema ambao walikuwa nami kwa hali na mali kipindi chote cha ugonjwa wangu. Vivyo hivyo kwa wafanyakazi wa shule yetu ya Mwalimu Nyerere ya Mbezi Beach, Dar es Salaam, na pia viongozi wote wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET).

Napenda pia kuwashukuru wafanyakazi wa TMJ; hususan wa kitengo cha ICU ambao walichacharika kweli kweli kuokoa maisha yangu usiku ule wa Julai 31 nilipoingizwa pale nikiwa hoi kabisa.

Vivyo hivyo kwa Dk. Fernand Masau wa THI na wafanyakazi wenzake bila kumsahau Dk. SK. Gupta wa Apollo Hospital ya India ambako ndiko hasa nilikopatia nafuu.

Na mwisho shukrani za pekee kwa wasomaji wangu wa ndani na nje ya nchi ambao walinitumia mamia ya sms za kuniombea kwa Mungu uponyaji. Mungu amezisikia sala zenu nyote. Asanteni sana.

Katika kipindi hicho cha ugonjwa wangu, ilikuwa dhahiri kwangu kwamba tatizo kubwa la hospitali zetu kubwa nchini ni ukosefu wa vifaa vya kisasa (state of the art) vya upimaji na vya kutolea tiba; lakini wataalamu tunao.

Binafsi, nililazimika kwenda India kwa sababu kipimo cha moyo cha teknolojia mpya kabisa nilichotakiwa kukifanya, kinapatikana katika hospitali moja tu nchini ya Regent (Dar); nacho kilikuwa kimeharibika (mpaka wakati huo).

Lakini hata kama kipimo hicho sasa kimetengenezwa na kutengemaa, wananchi wengi bado hawawezi kumudu gharama yake kubwa; na hivyo huduma hiyo imebaki kuwa ya wachache wenye uwezo au wale wanaochangiwa na marafiki na jamaa zao wenye uwezo.

Ni dhahiri gharama za kipimo hicho nchini zingeshuka kama serikali yetu ingejali kuvinunua vifaa hivyo vya state of the art na kuvisambaza kwenye hospitali zote za rufaa nchini badala ya kusubiri kupewa na Wazungu vifaa vya msaada ambavyo, mara nyingi, ni vile vilivyopitwa na wakati wanavyoviondoa katika hospitali zao ili kuweka vya kisasa zaidi.

Lakini uboreshaji wa hizi hospitali zetu za rufaa si agenda inayopewa moyoni kipaumbele na watawala wetu, kwa sababu wao wenyewe si watumiaji wa hospitali hizi. Ni mara ngapi tumesikia habari za viongozi wetu wakikimbilia hospitali za nje kupima afya zao?

Hata hayo maboresho kidogo yanayofanyika katika hospitali hizo ni yale yanayotokana na pesa za wafadhili, na si pesa za kodi zetu ambazo nyingi huishia kwenye mikondo ya mafisadi. Huwa najiuliza hali itakuaje nchini siku wafadhili watakapotuchoka kabisa!

Na tunapokuja kwenye suala la kuchokwa na wafadhili, nakumbuka nilipokuwa nimelazwa THI nilisoma, kwenye gazeti la Mwananchi, kauli moja ya Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati akihutubia mkutano wa kampeni huko Mbeya.

Kauli hiyo ilinikera kiasi cha kusababisha mapigo yangu ya moyo kuongezeka na kunifanya ghafla nizidiwe (tangu tukio hilo magazeti yakazuiwa kuingia wodini chumbani kwangu).

Kauli hiyo ni ile aliyoitoa kuwajibu wanaomshutumu kwamba anatumia mapesa mengi ya walipa kodi kufanya ziara nyingi za nje zisizo na ulazima. Alisema maneno mengi kuhalalisha ziara hizo, lakini yaliyoniacha hoi ni haya: “Mimi nakwenda kule (Ulaya na Marekani) kuhemea. Nikirudi narudi na kibaba.”

Kwa mtazamo wangu, haya ni maneno ya hovyo kutamkwa na rais wa nchi kuliko mengine yote yaliyopatwa kutamkwa na Kikwete. Hata yale kwamba wasichana wanaopata mimba shuleni ni kwa sababu ya viherehere vyao, hayafikii hayo aliyoyatoa kwenye kampeni mkoani Mbeya.

“Mimi nakwenda kule (Ulaya na Marekani) kuhemea. Nikirudi narudi na kibaba”, ni maneno ambayo ukiyatafakari utagundua kwamba yanatolewa na mtu anayeifurahia hali hiyo.

Ningemwelewa Kikwete kama angeueleza umati ule kwa hali ya kusikitisha kwamba sisi Watanzania tunamwangusha kwa sababu hatuchapi kazi vya kutosha; kiasi cha kufikia hatua ya kujitegemea, na hivyo tunamfanya ajidhalilishe kwa kwenda Ulaya na Marekani kuombaomba hata mambo ambayo tungeyamudu wenyewe kujitafutia.

Ningemwelewa Kikwete kama angeielezea hali hiyo kwa uchungu na kwa masikitiko, na hata kutisha kwamba hatakubali tena kwenda Ulaya na Marekani kuombaomba mambo ambayo sisi wenyewe tuna uwezo nayo (kama vile kutengeneza na kusambaza vyandarua vya bei nafuu).

Lakini sivyo alivyofanya kwenye hotuba hiyo. Kikwete aliitoa kauli hiyo kwa namna inayoonyesha kwamba anazifurahia ziara hizo za nje za kuomba misaada. Kwa maneno mengine, ujumbe wake kwa waliokuwa wanamsikiliza ulikuwa huu: “Nichagueni mimi; maana ni hodari wa kwenda nje kuhemea na kurudi na vibaba.”

Labda niwaulize Watanzania wenzangu: Je, tunamhitaji rais anayefurahia kutembeza bakuli la omba omba nje ya nchi au tunahitaji rais mwenye uwezo wa kutujengea misingi ya kujitegemea?

Je, kuna nchi dunia iliyopata kuendelea na kuondokana na umasikini kwa kutegemea misaada ya nje ya nchi? Je, ni familia gani duniani iliyopata kujikomboa kwenye umasikini inayoongozwa na baba ambaye kila kukicha hutembelea nyumba za majirani kuhemea vibaba vya unga kwa ajili ya ugali wa wanawe?

Ndugu zangu, tunapokuwa na rais wa nchi anayeona ni jambo la kawaida na linalofurahisha kwenda Ulaya na Marekani ‘kuhemea vibaba’, hatuwezi kamwe kujenga utamaduni wa kujitegemea.

Kwa hakika, rais wa namna hiyo huwa ana udhaifu mmoja mkubwa; nao ni kwamba si kiongozi visionary. Si kiongozi mwona mbali anayeifikiria Tanzania ya miaka 50 ijayo. Na si kuifikiria tu; bali kuweka misingi na mwelekeo wa kuifikia.

Najua kuwa wanayo hiyo wanayoiita vision 2025 iliyopo kabatini. Nadhani waliiandaa tu ili wakiulizwa kama wanayo wajibu ndio, lakini si kuifuata.

Kwa hiyo, mnapomchagua mtu asiye na vision kumiongoza, mjue kwamba mtapotea na mtatangatanga nyikani; maana hana uwezo wa kuiona njia itakayowatoa nyikani.

Labda nikumbushe kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere aliiona njia mapema na aliwaonyesha hawa kina Kikwete njia ya kutokea nyikani, lakini wameitelekeza, na ndiyo sababu tunatangatanga nyikani.

Naamini kwamba kama Kikwete na CCM yake ya sasa, ambayo imekumbatia mafisadi, atashinda uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, basi, tujue wazi kwamba tutakuwa tumejikatia tiketi nyingine ya miaka mingine mitano ya kutangatanga nyikani.

Nasema hivyo bila kupepesa kope; maana kiongozi anayefurahia ‘kuhemea vibaba’ Ughaibuni, hakika, si yeye wa kututoa nyikani.

Nihitimishe kwa kusema kwamba, kwa sasa, tunaweza kuikejeli siasa ya Ujamaa ya Mwalimu Nyerere, lakini ni upofu na ujinga kuitelekeza dhana yake ya Kujitegemea.

Ndugu zangu, Tutakuja kulipia kwa makosa hayo kama ambavyo tumeanza sasa ambapo tunasaidiwa hata vyandarua, na tunachekelea kwa hilo!

Huko mbele tutakuja kusaidiwa na Wazungu hata miswaki, na kwa ujinga wetu tutaendelea kuchekelea; huku wenzetu tuliokuwanao nyuma wakichanja mbuga kiteknolojia na kimaendeleo kiasi cha kufikia hata hatua ya kutuma vyombo anga za mbali!

Wakati wenzetu wengine tuliopata nao uhuru wakati mmoja sasa wana treni za kasi zinazotumia umeme, sisi hata reli aliyotuachia mkoloni inatushinda kuiendesha. Wakati wenzetu wana mashirika yao imara ya ndege ambayo ni alama ya taifa, sisi ATCL yetu iko taabani.

Kwa ufupi, tumepotea na tunahitaji kuitafuta njia aliyotuonyesha Nyerere. Kwa bahati mbaya CCM ya sasa haiwezi kuturejesha kwenye njia sahihi kwa sababu haina viongozi wenye vision japo ya miaka 50 au zaidi.

Ndiyo maana nasisitiza; Mtanzania yeyote mwerevu na mwona mbali (visionary) ataona kwamba rais tunayemhitaji na anayeifaa Tanzania yetu, ni yule anayetu
 
Mbona haya matusi ya wazi hatupingani kama hivi jamani au ninakosea kujuwa maana ya upinzani?
 
Back
Top Bottom