Twende mbele turudi nyuma, maswali ya msingi, inawezekanaje rais Uhuru alishindwa

Twende mbele turudi nyuma, maswali ya msingi, inawezekanaje rais Uhuru alishindwa

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Mengi yamesemwa, kwamba udukuzi ulitendeka kwenye upeperushaji wa matokeo baada ya uchaguzi, kwamba ushindi wa rais Uhuru sio halali na hii imepelekea hadi wana NASA kuomba nchi igawanywe mara mbili.

Sasa maswali ambayo sipati majibu yake, ni kwamba viongozi kwenye nyanja zingine zote hawakutegemea upeperushaji wa matokeo na ushindi wao ulihesabiwa mashinani na kutangazwa huko huko. Takwimu na tarakimu zinaonyesha chama cha Uhuru kilizoa viti vingi sana nchini, iweje wote hawa wapigiwe lakini waliowapigia kura wakose kumpa rais Uhuru.

Chama cha Jubilee kiliongoza kwenye idadi ya MCA ambao ni 582 wakati chama cha Odinga kikizoa 338
Uhuru ana wabunge 140 wakati Odinga akiambulia 61
Pia Uhuru anaongoza kwenye idadi ya magavana na maseneta, hii haingii akilini.

Japo inafahamika Uhuru alitumia nguvu nyingi ikiwemo raslimali za dola wakati wa kujinadi kwenye kampeni, lakini hili la ushindi ni wazi kwamba kashinda tena mchana, ni ukweli ambao mlengo wa upinzani unafaa kuukubali na kuupokea na kutafakari kipi kiliwakuta.

Leo hii hata kama mahakama ikiamua uchaguzi urudiwe, ifahamike hao viongozi wengi wa Jubilee waliochaguliwa watakua na nafasi muafaka ya kumfanyia kampeni Uhuru kwenye siku 60 ambazo zimeruhusiwa kikatiba. Ushindi wa pili utakua wa maamuzi makubwa ya kuhitimisha.

Mimi nafikiri upinzani ujitafakari, bado tunawahitaji lakini wajiangalie upya jinsi walinadi sera zao, ambazo mara nyingi zilikua za kutia madoa kwenye dola ilhali Uhuru alikita kwenye kueleza kile amekifanya kufikia sasa. Ni wazi Wakenya sote tunajua uongozi wa Uhuru ulikua na madoa doa ya matope, hivyo hatukuhitaji upinzani utumie hayo kama wimbo, wengi tulitegema kuambiwa nini kipo tayari kama mbadala wa utawala wa Uhuruto.

Rais Uhuru alikatiza na kupenya kwenye nchi yote kwa nguvu nyingi sana akijieleza. Kwanza alitumia uzinduzi wa reli ya SGR mpaka basi, yaani aliabiri treni na kuhutubia kila kituo alipokuta umati umemsubiri, ikumbukwe mamilioni ya Wakenya walikua wanafuatilia kwenye runinga zao. Upinzani ulijibu huo mtiti kwa kusema wazo la hiyo reli lilikua lao awali.
 
Tokea Raila aanze kulalamika kuwa kaibiwa kura hajatoa ushahidi hata kidogo. Kila siku anakuja na sarakasi mpya za kitoto. Nadhani ni katika hali ya kutapatapa lakini siku si nyingi akili yake itakubali kushindwa.

Huku nako 2015 wapinzani walilalamika kuwa wameibiwa lakini hawakutoa ushahidi hata kidogo. Ngazi ya ubunge na udiwani walibwagwa vibaya na CCM lakini bado wakadai kuwa wameibiwa kwenye Uraisi.

Hii tabia ya malalamiko yasiyo na kichwa wala miguu kuachwa ndio wakati mwingine huleta machafuko.
 
Raila.jpm_.orange.jpg


Huyu jamaa ndio alifanya Raila kushindwa


Swissme
 
Sasa maswali ambayo sipati majibu yake, ni kwamba viongozi kwenye nyanja zingine zote hawakutegemea upeperushaji wa matokeo na ushindi wao ulihesabiwa mashinani na kutangazwa huko huko. Takwimu na tarakimu zinaonyesha chama cha Uhuru kilizoa viti vingi sana nchini, iweje wote hawa wapigiwe lakini waliowapigia kura wakose kumpa rais Uhuru.
Mkuu mimi naomba jibu la swali moja tu: Kwanini Chris Msando aliuawa?Nani wako nyuma ya mauaji yake?
 
MK254 this same thing ilitokea bongo, nikakwambia ccm wana wabunge nyomi, but you didn't want to recognize that, sasa hivi nakuona unajitetea the same way.

Kweli what goes around comes around, sasa tatizo la uchaguzi wenu ni kwamba Msando ameuawa, na msando alihakikishia taifa this time hakutakuwa na theft.
 
MK254 pamoja na hilo suala la uhuruto kuwa na wabunge wengi kuliko nasa, Odinga anashawishika kuendelea na kesi kwa sababu zifuatazo!

1: Mwaka 2007 Mwai kibaki aliapishwa kuwa rais licha ya chama chake cha PNU kuwa na idadi ndogo ya wabunge ukilinganisha na ile ya ODM.

2: Kifo cha msendo kimetia doa kubwa na kusababisha watu wengi waamini kuwa pengine ulikuwa ni mkakati wa kisiasa.

3; Kasoro iliyojitokeza kuhusu utumaji wa taarifa ukiambatana na form. Hii nayo inaendelea kumpa nguvu.

4; Uchaguzi wa kiafrica umetawaliwa na matabaka! yawezekana hayo maeneo ambayo odinga alishindwa ubunge aliweka watu ambao hawakukubalika kitabaka



Lakini mimi nikukumbushe kuwa duniani kote kazi ya chama cha upinzani ni kukosoa pale chama tawala kinapokosea na kuahidi kuwa wao watafanya kila kitu kuwa sawa! Wakati huo huo chama tawala wao wanasifia na kuwakumbusha yale waliyofanya na kuahidi kuboresha zaidi! Hivyo RAO alikuwa sahihi kuponda UHuruto!


Ngoja nikupe mfano mwingine, hadi kufikia mwezi June mwaka huu, waingereza walikuwa wanamwamini sana na kumpenda waziri mkuu Theresa may, ila alipoitisha uchaguzi wa wabunge, akaangukia pua na kupata wabunge wachache ambao hata hawakutosha kuunda serikali! Lakini ukiangalia polls mpaka sa hz, bado mwanamama huyu anapendeka na waingereza!


Nachomaanisha hapa ni kuwa, watu wanachagua mtu sio chama! Japo kwa hapa africa hasa Kenya, chama/tabaka la mtu huangaliwa kwanza! (Ila marekani nao wameanza kubadilika, uchaguzi ulopita umetufunza vitu)
 
Mnataka kuanza kuchinjana nini majirani.

Jichungeni maana hatutapokea wakimbizi.
 
Sisi tunasubiria vita vya wenyewe kwa wenyewe apo Kenya. Ili panoge vizuri
 
jana nimemsikia akisema hataongeza mishahara ya wabunge,na hata kama Mahakama ikimpa Urais Odinga,amaesmshauri naye pia akatae kuongeza hiyo mishahara....woow what a president,He is even ready to leave office if the court rules in favour of his opponent...hapa kwetu hamna kitu hicho.[/QUOTE]


Mengi yamesemwa, kwamba udukuzi ulitendeka kwenye upeperushaji wa matokeo baada ya uchaguzi, kwamba ushindi wa rais Uhuru sio halali na hii imepelekea hadi wana NASA kuomba nchi igawanywe mara mbili.

Sasa maswali ambayo sipati majibu yake, ni kwamba viongozi kwenye nyanja zingine zote hawakutegemea upeperushaji wa matokeo na ushindi wao ulihesabiwa mashinani na kutangazwa huko huko. Takwimu na tarakimu zinaonyesha chama cha Uhuru kilizoa viti vingi sana nchini, iweje wote hawa wapigiwe lakini waliowapigia kura wakose kumpa rais Uhuru.

Chama cha Jubilee kiliongoza kwenye idadi ya MCA ambao ni 582 wakati chama cha Odinga kikizoa 338
Uhuru ana wabunge 140 wakati Odinga akiambulia 61
Pia Uhuru anaongoza kwenye idadi ya magavana na maseneta, hii haingii akilini.

Japo inafahamika Uhuru alitumia nguvu nyingi ikiwemo raslimali za dola wakati wa kujinadi kwenye kampeni, lakini hili la ushindi ni wazi kwamba kashinda tena mchana, ni ukweli ambao mlengo wa upinzani unafaa kuukubali na kuupokea na kutafakari kipi kiliwakuta.

Leo hii hata kama mahakama ikiamua uchaguzi urudiwe, ifahamike hao viongozi wengi wa Jubilee waliochaguliwa watakua na nafasi muafaka ya kumfanyia kampeni Uhuru kwenye siku 60 ambazo zimeruhusiwa kikatiba. Ushindi wa pili utakua wa maamuzi makubwa ya kuhitimisha.

Mimi nafikiri upinzani ujitafakari, bado tunawahitaji lakini wajiangalie upya jinsi walinadi sera zao, ambazo mara nyingi zilikua za kutia madoa kwenye dola ilhali Uhuru alikita kwenye kueleza kile amekifanya kufikia sasa. Ni wazi Wakenya sote tunajua uongozi wa Uhuru ulikua na madoa doa ya matope, hivyo hatukuhitaji upinzani utumie hayo kama wimbo, wengi tulitegema kuambiwa nini kipo tayari kama mbadala wa utawala wa Uhuruto.

Rais Uhuru alikatiza na kupenya kwenye nchi yote kwa nguvu nyingi sana akijieleza. Kwanza alitumia uzinduzi wa reli ya SGR mpaka basi, yaani aliabiri treni na kuhutubia kila kituo alipokuta umati umemsubiri, ikumbukwe mamilioni ya Wakenya walikua wanafuatilia kwenye runinga zao. Upinzani ulijibu huo mtiti kwa kusema wazo la hiyo reli lilikua lao awali.
 
Kukubaliana na wewe Uhuru ameshinda kihalali wakati shauri bado liko mahakamani, ni kuhalalisha kisicho halali. Kaa usubiri kitakacho amuliwa na mahakama, but kwa upande mwingine nina wasiwasi na mtu mwenye access ya database container.
 
jana nimemsikia akisema hataongeza mishahara ya wabunge,na hata kama Mahakama ikimpa Urais Odinga,amaesmshauri naye pia akatae kuongeza hiyo mishahara....woow what a president,He is even ready to leave office if the court rules in favour of his opponent...hapa kwetu hamna kitu hicho.
[/QUOTE]
Hiyo inaitwa kucheza na Akili za watu,
Many bad man will pretend very good, decent and innocent in public, wayanenayo ni tofauti na wayatendayo.
 
MK254 pamoja na hilo suala la uhuruto kuwa na wabunge wengi kuliko nasa, Odinga anashawishika kuendelea na kesi kwa sababu zifuatazo!

1: Mwaka 2007 Mwai kibaki aliapishwa kuwa rais licha ya chama chake cha PNU kuwa na idadi ndogo ya wabunge ukilinganisha na ile ya ODM.

2: Kifo cha msendo kimetia doa kubwa na kusababisha watu wengi waamini kuwa pengine ulikuwa ni mkakati wa kisiasa.

3; Kasoro iliyojitokeza kuhusu utumaji wa taarifa ukiambatana na form. Hii nayo inaendelea kumpa nguvu.

4; Uchaguzi wa kiafrica umetawaliwa na matabaka! yawezekana hayo maeneo ambayo odinga alishindwa ubunge aliweka watu ambao hawakukubalika kitabaka



Lakini mimi nikukumbushe kuwa duniani kote kazi ya chama cha upinzani ni kukosoa pale chama tawala kinapokosea na kuahidi kuwa wao watafanya kila kitu kuwa sawa! Wakati huo huo chama tawala wao wanasifia na kuwakumbusha yale waliyofanya na kuahidi kuboresha zaidi! Hivyo RAO alikuwa sahihi kuponda UHuruto!


Ngoja nikupe mfano mwingine, hadi kufikia mwezi June mwaka huu, waingereza walikuwa wanamwamini sana na kumpenda waziri mkuu Theresa may, ila alipoitisha uchaguzi wa wabunge, akaangukia pua na kupata wabunge wachache ambao hata hawakutosha kuunda serikali! Lakini ukiangalia polls mpaka sa hz, bado mwanamama huyu anapendeka na waingereza!


Nachomaanisha hapa ni kuwa, watu wanachagua mtu sio chama! Japo kwa hapa africa hasa Kenya, chama/tabaka la mtu huangaliwa kwanza! (Ila marekani nao wameanza kubadilika, uchaguzi ulopita umetufunza vitu)

Hoja yako ina mantiki kiaina, ila hiyo tofauti ya idadi ya wabunge, meseneta, magavana na MCA ni kubwa sana kiasi kwamba hata Odinga akiibuka mshindi kwa kweli sijui ataitawala vipi nchi. Kwa Kenya na Afrika niijuavyo, haiwezekani idadi kubwa ya wapiga kura wawe walimpigia Odinga kura na wakaishia kuchagua viongozi wengine wote wa mlengo wa serikali, sio kwa tofauti ya mamilioni ya wapiga kura.

Kifo cha Msando (RIP) hadi kufikia leo hakuna mtu anakihusisha kitaalam kwenye huu uchaguzi. Kila mtu anaishia kutuhumu tu kwamba jamaa aliuawa ili password yake itumike. Hakuna anayejiongeza na kuibua hoja ambayo inaweza kuleta mantiki.
Kwamba Msando alisema kwenye runinga yeye ndiye mwenye password ya nchi yote, hilo halitoshi maana hakuna mfumo wa kihivyo, labda kama yeye ndiye angekua ameutengeneza huo mfumo, lakini inafamika ulitengenezwa na kampuni ya Ulaya na ndio ilikua na dhamana ya kuhakikisha usalama wa mfumo, na pia kama angeuawa usiku wa kuamkia uchaguzi, hapo ingeleta picha, lakini mdau kauliwa siku kadhaa kabla, ina maana password yake iliachwa siku zote hivyo bila kubadilishwa.

Kwamba mtu mmoja mwenye password kwa ajili ya Wakenya zaidi ya milioni 44 alikua anapiga misele usiku kwenye vilabu, maana CCTV ilionyesha mienendo yake mjini. Haileti picha wala mantiki, naomba JF great thinkers washirikishe ubongo kwenye hili. Kuna watu kadhaa wamekamatwa, ikiwemo dogo mwenye umri wa miaka 17 aliyepatikana na simu iliyomtumia ujumbe wa kumtishia maisha, hivyo tuachie vyombo vya dola nafasi ya kutupa majibu.

Japo pia na naomba ifahamike, binafsi nilichukizwa sana na kifo cha huyo jamaa, alikua mzalendo Mkenya mwenzangu aliyejitolea katika kufanikisha uwajibikaji kwenye uchaguzi, hivyo nitapata raha sana siku nikiskia wauaji wake wamekamatwa, na wawe wauaji hasa na sio walalahoi wa kuzuga tu maana michezo ya mjini naijua, mtu anabambikiziwa kesi kizembe tu.
 
MK254 pamoja na hilo suala la uhuruto kuwa na wabunge wengi kuliko nasa, Odinga anashawishika kuendelea na kesi kwa sababu zifuatazo!

1: Mwaka 2007 Mwai kibaki aliapishwa kuwa rais licha ya chama chake cha PNU kuwa na idadi ndogo ya wabunge ukilinganisha na ile ya ODM.


Point ya kwanza:
Wewe umesahau kwamba eneo la kibaki lina watu zaidi lakini maeneo ya bunge sio mengi vile.So there's a chance Kibaki won legitimately kwa kura zaidi hata kama alikuwa na wabunge wachache.
 
Mengi yamesemwa, kwamba udukuzi ulitendeka kwenye upeperushaji wa matokeo baada ya uchaguzi, kwamba ushindi wa rais Uhuru sio halali na hii imepelekea hadi wana NASA kuomba nchi igawanywe mara mbili.

Sasa maswali ambayo sipati majibu yake, ni kwamba viongozi kwenye nyanja zingine zote hawakutegemea upeperushaji wa matokeo na ushindi wao ulihesabiwa mashinani na kutangazwa huko huko. Takwimu na tarakimu zinaonyesha chama cha Uhuru kilizoa viti vingi sana nchini, iweje wote hawa wapigiwe lakini waliowapigia kura wakose kumpa rais Uhuru.

Chama cha Jubilee kiliongoza kwenye idadi ya MCA ambao ni 582 wakati chama cha Odinga kikizoa 338
Uhuru ana wabunge 140 wakati Odinga akiambulia 61
Pia Uhuru anaongoza kwenye idadi ya magavana na maseneta, hii haingii akilini.

Japo inafahamika Uhuru alitumia nguvu nyingi ikiwemo raslimali za dola wakati wa kujinadi kwenye kampeni, lakini hili la ushindi ni wazi kwamba kashinda tena mchana, ni ukweli ambao mlengo wa upinzani unafaa kuukubali na kuupokea na kutafakari kipi kiliwakuta.

Leo hii hata kama mahakama ikiamua uchaguzi urudiwe, ifahamike hao viongozi wengi wa Jubilee waliochaguliwa watakua na nafasi muafaka ya kumfanyia kampeni Uhuru kwenye siku 60 ambazo zimeruhusiwa kikatiba. Ushindi wa pili utakua wa maamuzi makubwa ya kuhitimisha.

Mimi nafikiri upinzani ujitafakari, bado tunawahitaji lakini wajiangalie upya jinsi walinadi sera zao, ambazo mara nyingi zilikua za kutia madoa kwenye dola ilhali Uhuru alikita kwenye kueleza kile amekifanya kufikia sasa. Ni wazi Wakenya sote tunajua uongozi wa Uhuru ulikua na madoa doa ya matope, hivyo hatukuhitaji upinzani utumie hayo kama wimbo, wengi tulitegema kuambiwa nini kipo tayari kama mbadala wa utawala wa Uhuruto.


Rais Uhuru alikatiza na kupenya kwenye nchi yote kwa nguvu nyingi sana akijieleza. Kwanza alitumia uzinduzi wa reli ya SGR mpaka basi, yaani aliabiri treni na kuhutubia kila kituo alipokuta umati umemsubiri, ikumbukwe mamilioni ya Wakenya walikua wanafuatilia kwenye runinga zao. Upinzani ulijibu huo mtiti kwa kusema wazo la hiyo reli lilikua lao awali.

Mambo kama haya ndio yalifanya nimshangilie sana Governor Mutua arudi kwenye kiti chake .Hata kama mimi sijatoka Ukambani lakini kazi na vitendo vya Mutua ukilinganisha na mpinzani wake there was no contest there.Yeye Mutua yuko chama tofauti lakini kazi yake ,sera zake na kuweka maslahi ya mpiga kura na Machakos county mbele ....man ,i'd vote for him in a heartbeat even if i was from a different party.
 
Hoja yako ina mantiki kiaina, ila hiyo tofauti ya idadi ya wabunge, meseneta, magavana na MCA ni kubwa sana kiasi kwamba hata Odinga akiibuka mshindi kwa kweli sijui ataitawala vipi nchi. Kwa Kenya na Afrika niijuavyo, haiwezekani idadi kubwa ya wapiga kura wawe walimpigia Odinga kura na wakaishia kuchagua viongozi wengine wote wa mlengo wa serikali, sio kwa tofauti ya mamilioni ya wapiga kura.

Kifo cha Msando (RIP) hadi kufikia leo hakuna mtu anakihusisha kitaalam kwenye huu uchaguzi. Kila mtu anaishia kutuhumu tu kwamba jamaa aliuawa ili password yake itumike. Hakuna anayejiongeza na kuibua hoja ambayo inaweza kuleta mantiki.
Kwamba Msando alisema kwenye runinga yeye ndiye mwenye password ya nchi yote, hilo halitoshi maana hakuna mfumo wa kihivyo, labda kama yeye ndiye angekua ameutengeneza huo mfumo, lakini inafamika ulitengenezwa na kampuni ya Ulaya na ndio ilikua na dhamana ya kuhakikisha usalama wa mfumo, na pia kama angeuawa usiku wa kuamkia uchaguzi, hapo ingeleta picha, lakini mdau kauliwa siku kadhaa kabla, ina maana password yake iliachwa siku zote hivyo bila kubadilishwa.

Kwamba mtu mmoja mwenye password kwa ajili ya Wakenya zaidi ya milioni 44 alikua anapiga misele usiku kwenye vilabu, maana CCTV ilionyesha mienendo yake mjini. Haileti picha wala mantiki, naomba JF great thinkers washirikishe ubongo kwenye hili. Kuna watu kadhaa wamekamatwa, ikiwemo dogo mwenye umri wa miaka 17 aliyepatikana na simu iliyomtumia ujumbe wa kumtishia maisha, hivyo tuachie vyombo vya dola nafasi ya kutupa majibu.

Japo pia na naomba ifahamike, binafsi nilichukizwa sana na kifo cha huyo jamaa, alikua mzalendo Mkenya mwenzangu aliyejitolea katika kufanikisha uwajibikaji kwenye uchaguzi, hivyo nitapata raha sana siku nikiskia wauaji wake wamekamatwa, na wawe wauaji hasa na sio walalahoi wa kuzuga tu maana michezo ya mjini naijua, mtu anabambikiziwa kesi kizembe tu.
Ugumu kwenye kutawala nchi unaweza kuwepo kiutekelezaji, lakini kikatiba nadhani inakubalika, ushindi wa rais hauwezi kuathiriwa na uchache/wingi wa wabunge, magavana na hao ma MCA( niko huru kukosolewa kuhusu hili). Ndo maana hata ikitokea akatawazwa mshindi, nchi itaongozwa hata kwa seeikali ya mseto kama ataamua kufanya hvyo!

Kuhusu suala la msando tusahau kuujua ukweli kuhusu kifo chake, particularly kama kweli alikufa kwa sababu za kisiasa! Bahati nzuri tu familia yake ilibahatika kupata mwili wake.

Katika kifo hicho, kama ni cha kisiasa, kila upande una haki ya kutuhumiwa! Vipi kama waloshindwa waliona mapema watashindwa, af wakamwondoa ili wakishindwa asijekuwa kikwazo kwao kudai wameibiwa! Na vipi kama waloshinda waliona huyu ndo kikwazo ikabidi wamwondoe mapema ili wawe na mwanya mzuri wa kidukua!

Hili suala libaki tu hadithi, hakutakuja kuwa na ukweli!
 
Mimi sijakataa kuhusu ushindi wa kibaki, point yangu ni kutaka kuonyesha kuwa hata kama una wabunge wachache, uwezekano wa kushinda upo! That's all
 
Back
Top Bottom