TZ ya Viwanda: Viwanda Vidogo Majumbani

HaveANiceDay

New Member
Joined
Feb 15, 2019
Posts
1
Reaction score
1
Viwanda Vidogo Majumbani – Mijini, Miji Midogo na Vijijini

Jinsi ya kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo-vidogo

Tokea miaka mingi viwanda vidogo-vidogo vimeonyesha umuhimu wa kusaidia ukuaji wa ajira. Mipango mingi imesaidia uendelezaji wake.

Lakini kwa muda mrefu matatizo madogo madogo yanaonekana kwa uwazi, kama upatikanaji wa malighafi, mitaji, nguvumali kazi ujuzi (skilled labor), utafutaji wa masoko, n.k

Matatizo mengi yanatatuliwa na kutafutiwa ufumbuzi na Serikali Kuu pamoja na Serikali za Mitaa kwa mipango mirefu na mifupi. Pia kwenye udhibiti, uongozaji na usaidiaji (regulate, control, and support). Hili pia linaonekana wazi.

Baadhi ya hatua za ziada zinazoweza kukuza na kuendeleza viwanda vya aina zote na vya ngazi zote zinazoweza kutumika kwa mapana nitakazoandika ni kwa ajili ya:
  1. usaidiaji wa viwanda vidogo vidogo vilivyopo vikapewa nguvu- endelevu kuweza kuvuka hatua vilivyopo ya viwanda vidogo vidogo kwenda kuwa viwanda vya kati, na
  2. vya kati viwezeshwe kuwa viwanda vikubwa,
  3. na pia kusaidia uendelevu, uongezefu na uanzishwaji wa viwanda vidogo majumbani.
Kuendeleza kwa usaidiaji wa viwanda vidogo vidogo (VVV) vilivyopo kupewa nguvu endelevu kuweza kuvuka hatua vilivyopo vya viwanda vidogo vidogo kuwa viwanda vya kati (VVK) na vya kati kuwa viwanda vikubwa (VV), (Pointi ya 1 & 2 juu) inaweza kuwa kwa hatua zifuatazo:

• ‘Established VVV’ kuwa VVK na ‘already established VVK’ kuwa VV ndani ya miaka 2 mpaka 3. Njia zinazoweza kutumika kama:
o Kuviongezea hizo VVV nguvu ili ziongeze nguvumali kazi, malighafi na vifaa kwa namna kama zifuatazo:
  1. Capital-wise: Kupewa mikopo ya benki kwa malengo hayo.
  2. Market-wise: Waonyeshwe jinsi ya kutafuta masoko
    duniani kwa kuwasaidia kufungua akaunti kwenye masoko makubwa kama alibaba, n.k na jinsi ya kutumia hizo international platforms, na/au kuwatengenezea local-platforms.
  3. Customer Care-wise: Waelekezwe jinsi ya ‘packaging’, usafirishaji na ufuatiliaji wa mizigo mpaka unapofika kwa mteja.
  4. Income-wise: Waelekezwe jinsi ya kutumia huduma za utumaji na upokeaji hela kwenye masoko ya dunia nzima kama paypal, n.k ikiwezekana kuwafungulia accounts kwenye huduma zinazotumika masokoni na/au kuwatengenezea local platforms.
  5. Technical-wise: Kwa njia hizo i-iv juu ambazo zimejumuisha technology, zinaweza kutumika kufuatilia na kununua vifaa (cheap machinery) na technolojia mbalimbali vitavyoweza kuongeza ufanisi wa kazi na bidhaa zao. Wataweza kununua vifaa kwenye hayohayo masoko wanayotumia kuuzia, kwa kutumia upokeaji hela na utumaji hela huo huo husika.
• Uongezefu na uanzishaji wa viwanda vidogo majumbani:
o Njia moja inayoweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo
vingi na kwa haraka ni kwa kupromote “viwanda vidogo majumbani (VVM)” sehemu za mijini na vijijini. Ni muhimu kutoa elimu na kuhamasisha juu ya “household small scale industries-VVM, kwani zina faida mbali mbali kama zifuatazo:
  1. Kuondoa ‘unemployment’ kwa wingi zaidi na kwa muda mfupi zaidi. (mfano: China, India, Vietnam, Nepal, Phillipines, Nigeria nk)
  2. VVM vipo kwenye ngazi ya familia, hivyo basi watu wa kwanza kabisa kupata kazi na kuwa waajiriwa hapo ni watu wa hiyo familia. Hii inaongeza kwenye point (i) juu hapo, kuwa kama unemployment inaweza kuondoka kwenye ngazi ya familia basi kwenye ngazi ya Taifa itapungua pia kwa kasi kubwa na kiasi kikubwa.
  3. VVM havitahitaji ujenzi mkubwa wa ‘viwanda’ kwani nyumbani ndiyo uzalishaji wa kwanza unapofanyika.
Jinsi ya kuanzisha hivyo VVM kwenye ngazi ya juu ili kutoa hamasa na jamii ifahamu hayo na kuwawezesha kufungua VVM majumbani na kufanya ‘concept’ ifike hadi vijijini/mijini inaweza kufanyika kwa:
Kuanzisha Kituo cha Viwanda Wilayani (District Industry Centers- DIC) kwenye kila wilaya. Vikiwa na hizi kazi:​
a. Raw Material Assistance: DIC zitapromote VVM vijijini ambavyo vinaendana na mazingira ya hapo, na malighafi zinazipatikana hapo wilayani.
b. Marketing Assistance: DCI itawaonyesha na kuwafunza jinsi ya kuongeza value kwenye bidhaa ili ziweze kuwa bidhaa na bei shindani katika masoko mbalimbali ndani ya wilaya, mkoa, taifa na mataifa.
c. Technical Assistance: DCI zitoe miongozo yote ya Technolojia endelevu na jinsi ya kuagiza vifaa vye bei nafuu kwenye VVM.
d. Financial Assistance: DCI zifacilitate credits kupitia benki mbalimbali za maendeleo na viwanda ili mikopo ziwafikia households/nyumba zenye VVM
e. Training Assistance: Kipaumbele kwa wanawake na vijana wajue VVM, kuwapa miongozo, mawazo na njia hizo (a-d juu), ili kuwawezesha kufungua na kuendeleza VVM.

VVM itaongeza watu kujiajiri na itafungua fursa mbalimbali zilizopo katika kila wilaya husika. Hakuna wilaya itakayokuwa nyuma ya mwenzake. Itafungua fursa za kibiashara kati ya wilaya na wilaya na kadha wa kadha.

Uendelevu wake (Overall Sustainability) wa hatua zone hizi kwa pamoja:
Baada ya miaka 2-3 VVM zilizofanikiwa zinaweza kuwa registered, kuwezeshwa kufikia VVK, na baadae hivyo VVK kuwezeshwa kuwa VV kama aya za hapo juu zinavyoeleza, na pia kutokana na growing demand, attractive opportunities, higher investments and policy support, kwa kutumia hatua zote za hapo juu. Kwahayo, kila wilaya itakua na viwanda vya steji zote (vidogo, vya kati na vikubwa), na pia vision ya Tz ya Viwanda itakua endelevu miaka hii na miaka ijayo. Pia, hii ni inclusive kwa jamii nzima: Maskini-tajiri, Wadogo-wakubwa, Kina mama-kina baba, hasa pia kwa vijana na wasio na ajira mijini-vijijini.

Baadhi ya mifano ya viwanda vidogo majumbani (VVM) Vijijini-Wilayani:
Consumer Goods: Footwear, Ready made Garments, Toys, Handloom weaving, Handicrafts, Detergent & Soap, Fabric-Textile-Thread, Woollens, Carpets, Leather goods, Pottery, Knitting, Carpentry, Woodcrafts, Candle Making,
Skilled Products: Bricks and Tiles, Jewelry, Stone Craft, Paper Product, Coir, Metal-Iron & Steel Crafts, Hand Tools, Foundry, Cutlery, Lock & Key, Small machine Tools, Paper Napkins, Toilet Rolls, Sanitary Napkins, Wooden Toothpicks,
Agro-based Products: Edible, Spices, Oils, Honey, Jams, Beverage eg. juice-water &wine, Potato powder, Potato-Cassava-Banana Chips, Tea-Coffee, Poultry Feed, Herbal, Cigarette & Tobacco, Fruit products

Upande wa Mijini: construction services, bricks and tiles, ICT, other services like: retail, transportation, delivery, advertisement, entertainment, hospitality, tourism, waste management, fashion, mobile phones, photography, na kampuni za huduma nyingine. Hivi vingi vipo, ni kuvivusha kutoka steji vilivyopo VVV kwenda VVK, na VVK kwenda VV
* Miji mikubwa na Mijini wanapata fursa ya kuwa wauzaji na wanunuzi wa bidhaa zinazotokea wilaya mbali mbali.​

----- ---- ---- --- Asante kwa kusoma --- ---- ---- ---
e-mail: vijanaelimuujasiriamali@gmail.com
- Hii ni Self-initiated proposal & insight dedicated kwa Vijana wote na kwa ajili ya support ya TZ ya viwanda, na jinsi vinavyoweza kuongezewa support na hasa uanzishwaji na ukuzwaji wa viwanda vidogo vidogo na stages kuelekea Viwanda Vya Kati na Viwanda Vikubwa.
- Ukicopy usisahau kufanya citation 🙂
- Kama utahitaji insight ya uendelevu kutoka hatua moja kwenda nyingine ya vitu mbalimbali kama Elimu, n.k email me, nikipata muda nitafikiri juu ya hiyo topic, ilimradi iwe ‘developmental’
God Bless. Feb 2019
 
We jamaa ccm hawawezi fanya hayo mambo kamwe.Mambo mazuri kama haya wanaweza watu wa Ukawa.Yaani unaonekana una akili sana .Lisu akiwa Rais tutakuweka kwenye think tank ya Tanzania Mpya.God Bless
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…