U JUHA WA AJIBU NI WA KIWANGO CHA FLYOVER

marcoveratti

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2017
Posts
1,019
Reaction score
1,824
Samatta angekua Simba leo angekua Genk? Simba inatamani kuwa kama Mazembe lkn bado haiwezi kufikia level za Mazembe mwaka leo wala kesho.

1. Kumiliki uwanja
2. Kuwa timu yenye ushindani CCL.
3. Kutwaa ubingwa wa CCL.
4. Kuuza jezi online
na vingine kibao

Alf Moise Karudi Congo Ajib analaana anapishana na gari la mshahara kila mwaka.

nilichogundua wabongo tunatabia ya kuridhika mapema ukisoma soma stori za wachezaji weusi waliotoboa mbele unakuta walipitia mengi sijui kaenda ulaya kwa meli ya kudandia kapita italy ubaguzi ukamshinda kaenda ufaransa kalala barabarani kwenye baraza ndio anakuja kutoboa lkn huku kwetu mtu akicheza Simba Yanga kazi imeisha

Hata kama hujui radha ya kutoboa ulaya...inamana samata hamuoni?.
Jamaa anapokelewa na mawaziri kuliko Hata mabalozi wa nchi

Mchezaj ambae hata team ya taifa anastruggle kupata no ndo umsajil then ukapambane na Esperance, waydad, eto, al ahaly , zesco nk alaf Eti anagoma ! kweli mapimbi hawataisha duniani
 
kafanya nini tena?
 
Tp mazembe ndiyo wamesitisha huo mpango sio Ajib
Watu wanakimbilia kumlaumu ajibu bila kuangalia upande wa pili. Wana uhakika gani kama alifanikiwa majaribio? Hata kama walionesha interest lakini wanaweza kubadilika baada ya kugundua kitu ambacho hawakukijua awali
Kataka dau kubwa ndio sababu. Katazama mshahara kuliko future. Meneja wake anahusishwa kwa hilo. Duru nyingine zinadai Simba ndio chanzo cha dili kufa
 
Watu wanakimbilia kumlaumu ajibu bila kuangalia upande wa pili. Wana uhakika gani kama alifanikiwa majaribio? Hata kama walionesha interest lakini wanaweza kubadilika baada ya kugundua kitu ambacho hawakukijua awali
We nani alikwambia kama TP walitaka wamjaribu kwanza, wenyewe walitaka kumsajili moja kwa moja bt habari zilizopo ni kwamba Ajib kakataa kwa madai wameshindwana maslahi (ujinga)
 
Binadamu wa ajabu wanataka ajibu akubali kulipwa kijimshahara kisa kuitwa mchezaji wa mazembe, huo ndio ujinga sasa,samatta alianza na mshahara wa $10000 hakuwa boya, football ni mchezo wa muda hakuna haja ya kuwafurahisha watu wakati Tanzania hii mchezaji anavuta $3000-$7000
 
Ishu ni kwamba Ajibu kajichanganya mwenyewe kwa tamaa zake, alishachukua hela ya usajili wa awali Simba, TP Mazembe ikabidi waifuate Simba, Simba wakawaambia TP kwamba ili tumruhusu tunataka Mil 220 mezani, Ndipo TP Mazembe wakasusia dili
Kafanyaje mbona povu tu mjomba.
Ajib ana talent, lkn hana character ya kuchezea timu kubwa. Yule mtu ni bro-yo, full kujisikia. Hajui kujituma.

Naamini ni Mazembe ndio watakuwa wamemuasses na kumuomba arudi tu akacheze na Manara dhidi ya Amber Rutty
Kataka dau kubwa la shilingi ngapi na tp mazembe walitaka kumpa shilingi ngapi???
Wakikujibu nitarge
Jamaa nimemwona ni mpumbav wa kiwango cha lami

Jinga kabisa yaani ....

Sijui limerogwa ....
We nani alikwambia kama TP walitaka wamjaribu kwanza, wenyewe walitaka kumsajili moja kwa moja bt habari zilizopo ni kwamba Ajib kakataa kwa madai wameshindwana maslahi (ujinga)
Ndio maana ya makubaliano ya maslahi binafsi
Sasa mbona watu wanamlaumu wakati hawajui chochote...bongo bwana kuna watu ni wataalamu wa kuwapangia wenzao maisha,yaani mtu ukikuta anamshauri mtu namna ya kutoboa wakati ye maisha yamempiga hana lolote unabaki kushangaa tu
 
Wachezaji wetu wanahitaji sana kupata elimu ya mikataba. Pili ni wakati muafaka sasa TFF iwekeze kwenye kuandaa mawakala wadogo wadogo ili kuwasimamia wachezaji wetu. Tatu TFF na SPUTANZA ziwe zinandaa semina kwa ajili ya wachezaji wetu wawe wanaweza kupambana na kuwa wavumilivu na sio kusubiri kesi za wachezaji kuvunjiwa mikataba.

Pia tuiombe wizara ya michezo/vijana iangalie kwa jicho la tatu suala la elimu ya mikataba, ukakamavu, upambanaji na kutokutaa tamaa kwa wachezaji wetu wa michezo yote kwani michezo ni ajira. Unapokuwa na wanamichezo takribani 10,000 wa michezo mbali mbali kama ngumi, mpira wa miguu, riadha, kuogelea n.k. wa kimataifa kwanza tayari wanakuwa na ajira, pili mapato watakayopata yatakuja kusaidia nchi na wao wataajiri pia watu wa kuwasaidia.

Mimi ni shabiki wa Simba, lakini kama ni kweli Ajibu ametema dili la Mazembe kwa ajili ya Simba hapo kachemka. Hata Simba wenyewe watakuwa wamechemka kwa sababu kiasili Ajibu ni mchezaji mvivu mvivu, hajitambui kabisa kipaji chake. Angekuwa makini yeye ndiye angekuwa anafuata njia ya Samata kabla hata ya Msuva.

Mpira ni mchezo wa muda maalum umri ukipita ndio basi tena. Leo hii wapo wapi Gerson Tegete, Haruna Moshi na Halfan Ngasa. Siasa za Simba na Yanga zimeharibu kabisa maisha yao ya baadae.

Ajibu alipaswa ajifunze moyo wa kupambana kama Samatta. Sijui wachezaji wa Tanzania wanakwama wapi. Ukipata historia za wachezaji wengi wa Afrika Magharibi wanavyokwenda Ulaya njia wanazopitia ni za hatari sana lakini hatimaye wanafanikiwa. Lakini hawa wa kwetu hata kupita njia halali hawawezi sijui tumelogwa na nani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…