Matatizo yaliyojitokeza katika uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura Zanzibar, yamejirudia hapa Bara. Tofauti na Zanzibar ambao walikua na vigezo vya kukataa kuandikisha watu kama kutokua na kitambulisho cha mzanzibar mkazi. hapa Bara watu wamekosa haki yao ya kuandikishwa bila sababu wala maelezo.
Kwa hapa Dar es Salaam ambako wiki iliyopita zoezi la uandikishwaji na uboreshaji katika daftari la wapiga kura lilikua likifanyika, watu wengi walijitokeza tofauti na matarajio ya Tume ya uchaguzi kitu ambacho kilileta usumbufu mkubwa kutokana na uchache wa vitendea kazi vilivyo kua vimeandaliwa. Pamoja na tume hiyo kuliona hilo mapema, haikuchukua hatua zozote kuongeza vitendea kazi au muda wa kutosha kufanikisha zoezi hilo. Sijui kama ni makusudi au ni upofu wa watendaji wa tume.
Badala ya kuchukua hatua za kuboresha uandikishaji, mkurugenzi wa uchaguzi alitoa very negative remarks, ati watu wanataka tu vitambulisho kwa vile hawana ajira au inawezekana wanajiandikisha mara mbili hivyo akaongeza siku moja tu. Sijui kwa nini afikirie hivyo wakati ni kazi yake kuratibu shuhghuli za uchaguzi.
Matokeo yake muda umeisha na watu wengi hawakuweza kupata vitambulisho vya kupigia kura. Kilichotia aibu ni makarani waliokua wanaandikisha kubadili zoezi hilo kuwa mradi wao wa kujipatia hela katika dakika za mwisho. Mfano katika kituo cha Wazo Hill, makarani walikua wanachukua rushwa ya sh. 2000 kuweza kumrahisishia mtu uandikishaji na kufanya kazi ile taratibu sana ili kufanikisha azma yao. Mpaka saa ya kufunga zaidi ya watu 50 katika kituo hicho hawakua wamepatiwa vitambulisho na wakaambiwa zoezi limefungwa. Pamoja na kulalamika kwa mtendaji wa mtaa hawakufanikiwa. Tofauti na Wazanzibar, Wabara hawana mwamko wa kulalamikia haki zao kwenye siasa hivyo ni wengi walikua wamekata tamaa na kususa.
Swali hawa watu watapata wapi haki yao ya kupiga kura? Hii imepangwa makusudi kupunguza wapiga kura Dar au ni uzember tu wa Tume?
Kwa hapa Dar es Salaam ambako wiki iliyopita zoezi la uandikishwaji na uboreshaji katika daftari la wapiga kura lilikua likifanyika, watu wengi walijitokeza tofauti na matarajio ya Tume ya uchaguzi kitu ambacho kilileta usumbufu mkubwa kutokana na uchache wa vitendea kazi vilivyo kua vimeandaliwa. Pamoja na tume hiyo kuliona hilo mapema, haikuchukua hatua zozote kuongeza vitendea kazi au muda wa kutosha kufanikisha zoezi hilo. Sijui kama ni makusudi au ni upofu wa watendaji wa tume.
Badala ya kuchukua hatua za kuboresha uandikishaji, mkurugenzi wa uchaguzi alitoa very negative remarks, ati watu wanataka tu vitambulisho kwa vile hawana ajira au inawezekana wanajiandikisha mara mbili hivyo akaongeza siku moja tu. Sijui kwa nini afikirie hivyo wakati ni kazi yake kuratibu shuhghuli za uchaguzi.
Matokeo yake muda umeisha na watu wengi hawakuweza kupata vitambulisho vya kupigia kura. Kilichotia aibu ni makarani waliokua wanaandikisha kubadili zoezi hilo kuwa mradi wao wa kujipatia hela katika dakika za mwisho. Mfano katika kituo cha Wazo Hill, makarani walikua wanachukua rushwa ya sh. 2000 kuweza kumrahisishia mtu uandikishaji na kufanya kazi ile taratibu sana ili kufanikisha azma yao. Mpaka saa ya kufunga zaidi ya watu 50 katika kituo hicho hawakua wamepatiwa vitambulisho na wakaambiwa zoezi limefungwa. Pamoja na kulalamika kwa mtendaji wa mtaa hawakufanikiwa. Tofauti na Wazanzibar, Wabara hawana mwamko wa kulalamikia haki zao kwenye siasa hivyo ni wengi walikua wamekata tamaa na kususa.
Swali hawa watu watapata wapi haki yao ya kupiga kura? Hii imepangwa makusudi kupunguza wapiga kura Dar au ni uzember tu wa Tume?