A
Anonymous
Guest
Siku za karibuni tunazidi kuona upotovu wa ukweli kwenye Vyombo vya Habari unaozidi kukithiri nchini. Hii inatokana na Waandishi wa Habari za kiupelelezi kuangalia maslahi yao binafsi kwa kupokea hongo, na kuishia kuminya ukweli wa habari zinazotakiwa kutolewa.
Sijui niseme Waandishi wa Habari za kiupelelezi wengi walikuwa wanapenda na kuitumikia miaka ya nyuma wamekufa moyo kwasababu za kubanwa na Serikali au labda mambo kuwa magumu kiuchumi, ila siku hizi ukiwa na shida ukiweza kumpata Mwandishi wa kweli ambaye ataipika taarifa inayogusa pande mbili zenye mgogoro wa aina yoyote basi imekuwa ngumu, kwasababu ya Waandishi wengi kuangalia maslahi yalipo.
Naandika hii baada ya kutokewa na mgogoro kwenye mtaa ninaoishi. Nikatafuta Waandishi wa Habari ili hii habari ipate kuonekana na wanaohusika na lifanyiwe kazi.
Cha kushangaza Waandishi wa Habari kwanza wanataka hela yao ili waweke mfukoni, na mbaya zaidi waliwaruka walalamikaji kwa kwenda kwa mlalamikiwa na habari mzima ikaishia kubadilishwa, na walalamikaji wakaoneshwa wao ndio wabaya.
Hicho kitu kinauma sana jamani. Watu wanashida then wanaona labda wakienda kwa Waandishi wa Habari ili wasaidie malalamiko yao yapazwe Serikali ichukue hatua za kisheria hao Waandishi wanaishia kuwageuka walalamikaji na kuwafanya waonekane ni wabaya.
Soma Pia:
Waandishi wa Habari badilikeni, wananchi tunaumizwa, tusaidieni kupaza sauti zetu sisi wananchi tunaokandamizwa, na sio kutugeuka. kwasababu ya maslahi yenu binafsi.
Sijui niseme Waandishi wa Habari za kiupelelezi wengi walikuwa wanapenda na kuitumikia miaka ya nyuma wamekufa moyo kwasababu za kubanwa na Serikali au labda mambo kuwa magumu kiuchumi, ila siku hizi ukiwa na shida ukiweza kumpata Mwandishi wa kweli ambaye ataipika taarifa inayogusa pande mbili zenye mgogoro wa aina yoyote basi imekuwa ngumu, kwasababu ya Waandishi wengi kuangalia maslahi yalipo.
Naandika hii baada ya kutokewa na mgogoro kwenye mtaa ninaoishi. Nikatafuta Waandishi wa Habari ili hii habari ipate kuonekana na wanaohusika na lifanyiwe kazi.
Cha kushangaza Waandishi wa Habari kwanza wanataka hela yao ili waweke mfukoni, na mbaya zaidi waliwaruka walalamikaji kwa kwenda kwa mlalamikiwa na habari mzima ikaishia kubadilishwa, na walalamikaji wakaoneshwa wao ndio wabaya.
Hicho kitu kinauma sana jamani. Watu wanashida then wanaona labda wakienda kwa Waandishi wa Habari ili wasaidie malalamiko yao yapazwe Serikali ichukue hatua za kisheria hao Waandishi wanaishia kuwageuka walalamikaji na kuwafanya waonekane ni wabaya.
Soma Pia:
- Baraza la Habari Tanzania lahimiza Weledi, umahiri kwa vyombo vya habari kulinda heshima kada hiyo
- Baraza la Habari Tanzania (MCT) linazindua Ripoti ya Hali ya Sekta ya Habari Tanzania 2022/23 leo Julai 4, 2024
Waandishi wa Habari badilikeni, wananchi tunaumizwa, tusaidieni kupaza sauti zetu sisi wananchi tunaokandamizwa, na sio kutugeuka. kwasababu ya maslahi yenu binafsi.