Habari za mwaka mpya wanaJF!
Awali ya yote nimpongeze Rais Magufuli kwa uchapakazi wake uliotukuka na kuwa Rais wa Mfano Afrika. Pia Rais wetu amekua mstari wa kupambana na rushwa katika taifa letu ili kuleta usawa.
Kimsingi hoja hapa baada ya pongezi kwa kiongozi wetu wa nchi, niende kwenye hoja mahususi:
Buluba ni shule ya pili kwa ukongwe mkoani Shinyanga, ikiwa inamilikiwa na SHIRECU (1984) Ltd imepita vipindi tofauti tofauti!
Hadi Mei mwaka wa Jana ambapo yalifanyika mabadiliko makubwa na kumpata Mwenyekiti wa bodi kijana, Richard Luhende ambaye aliahidi kuboresha Ushirika pamoja na shule ya sekondari ya Buluba kwa kuanzisha ofisi ya meneja wa shule ambayo awali haikuwepo!
Mambo yageuka kilio baada ya Richard Luhende mwaka wa bodi na rafiki yake Maduhu Nkamakazi kuchota kiasi cha million sitini na ushee pesa ya kitanzania.
Pesa hizo zinajumuisha ada ya mitihani ya wanafunanzi kidato cha pili 2018 na kidato cha NNE 2018. Ada ya mitihani waliokula inakadriwa kuwa million tano! Hivyo ada ya mitihani ambayo imekwisha fanyika haijalipwa.
Luhende na wenzake wameisababishia shule hasara ya million 116 baada ya kuwafukuza walimu 8 ambao walienda kutafuta haki mahakamani!
Wito kwa mamlaka husika ya kusimamia Elimu na vyama vya ushirika nchini kuchukua hatua!
Wizara za TAMISEMI na ELIMU zimshauri Mh. Rais achukue Buluba iwe ya Serikali ili iendelee kutoa huduma kwa Watanzania wote!
TAKUKURU iwahoji Luhende na Rafiki yake Nkamakazi werejeshe pesa za shule!
Mwanaharakati!
Karibu sana mwaka 2019
Awali ya yote nimpongeze Rais Magufuli kwa uchapakazi wake uliotukuka na kuwa Rais wa Mfano Afrika. Pia Rais wetu amekua mstari wa kupambana na rushwa katika taifa letu ili kuleta usawa.
Kimsingi hoja hapa baada ya pongezi kwa kiongozi wetu wa nchi, niende kwenye hoja mahususi:
Buluba ni shule ya pili kwa ukongwe mkoani Shinyanga, ikiwa inamilikiwa na SHIRECU (1984) Ltd imepita vipindi tofauti tofauti!
Hadi Mei mwaka wa Jana ambapo yalifanyika mabadiliko makubwa na kumpata Mwenyekiti wa bodi kijana, Richard Luhende ambaye aliahidi kuboresha Ushirika pamoja na shule ya sekondari ya Buluba kwa kuanzisha ofisi ya meneja wa shule ambayo awali haikuwepo!
Mambo yageuka kilio baada ya Richard Luhende mwaka wa bodi na rafiki yake Maduhu Nkamakazi kuchota kiasi cha million sitini na ushee pesa ya kitanzania.
Pesa hizo zinajumuisha ada ya mitihani ya wanafunanzi kidato cha pili 2018 na kidato cha NNE 2018. Ada ya mitihani waliokula inakadriwa kuwa million tano! Hivyo ada ya mitihani ambayo imekwisha fanyika haijalipwa.
Luhende na wenzake wameisababishia shule hasara ya million 116 baada ya kuwafukuza walimu 8 ambao walienda kutafuta haki mahakamani!
Wito kwa mamlaka husika ya kusimamia Elimu na vyama vya ushirika nchini kuchukua hatua!
Wizara za TAMISEMI na ELIMU zimshauri Mh. Rais achukue Buluba iwe ya Serikali ili iendelee kutoa huduma kwa Watanzania wote!
TAKUKURU iwahoji Luhende na Rafiki yake Nkamakazi werejeshe pesa za shule!
Mwanaharakati!
Karibu sana mwaka 2019