KERO Ubadhirifu wa fedha za ushirika wilayani Tunduru

KERO Ubadhirifu wa fedha za ushirika wilayani Tunduru

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Wiki Moja iliyopita Chama kikuu cha ushirika Tunduru kiliendesha mafunzo kwa viongoz wa vyama msingi yaani AMCOS zote za wilaya hii, jumla ya wajumbe waliohudhuria mafunzo ya walikuwa 586 na mkufunzi mmoja na viongozi kutoka Chama kikuu hawakuzidi 15, mafunzo yalikuwa ya siku mbili tu.

Ambapo wajumbe wote wa kutoka vyama vya msingi AMCOS waligharamiwa na AMCOS zao maradhi na nauli.
Chama kikuu cha ushirika Tunduru kiligharamia chakula yaani CHAI, vinywaji na chakula cha mchana na pia walimlipa mkufunzi na gharama za ukimbi na mapambo gharama yake sio zaidi ya mil.5 Kwa vile ukumbi na sh laki 7.

Cha kushangaza Chama kikuu kimetumia sh.mil 476

Huu ni ubadhiirifu wa fedha za uma

Tunaomba Waziri wa Kilimo achuguze hili Jambo na achukue hatua ,hizi pesa ni zetu sisi wakulima tunakatwa kwenye Kila kilo Moja ya mazao tunayoyauza.
 
Back
Top Bottom