Ubaya na uzuri wa katiba inayopendekezwa

Ubaya na uzuri wa katiba inayopendekezwa

ntamaholo

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
12,938
Reaction score
6,942
Wakuu salamu.

Tayari nakala za katiba pendekezwa zimefika katika mamlaka za serikali za kata. katika kata ninayoishi ambayo ndo inatengeneza makao makuu ya wilaya, mtendaji kata pekee ndiye kapewa nakala 900 za katiba inayopendekezwa.

Ni vigumu kila mtu kupata nakala yake hivyo mtendaji alicho kifanya amegawa katiba hizo kwa taasisi za serikali, ngos, mashirka ya dini, vikundi vilivyosajiliwa, wenyeviti wa vitongoji na makundi mengine. lengo ni kuwasaidia makundi hayo kama watakuwa na mijadala basi wasikose japo nakala tano za kufanyia rejea.

Sasa wasomi wa JF na hasa wale wanaotengeneza makundi mawili ya kuikubali au kuikataa katiba hii tunaomba mtupe mwongozo.

1. Wanaotaka tuikatae, kwa nini tupige kura ya hapana?
(a) Ni maeneo gani ambayo labda yamechakachuliwa ili yatusaidie kujua hila za waliochakachua?

2. Wanaosema tupige kura ya ndiyo, kwa nini tupige kura ya ndiyo?
(a) Kwa nini baadhi ya vipengele vilivyopendekezwa na wananchi kama sehem ya kusimamia uwajibikaji mlivitoa? mfano kumpuzisha mtu ubunge
(b) Kwa nini mlifuta kuanzishwa kwa tanganyika huru na kuamua kuianzisha Zanzibar huru yenye mamlaka kamili?

Hayo ni maswali chokozi ambayo naamini mkitupa ukweli itatusaidia kuijua katiba kwa haraka na hivyo kuandaa kura ya ndiyo au hapana.

Karibuni mtuelimishe. ni vizuri kutumia ulinganisho wa rasimu ya katiba na katiba pendekezwa ili kurahisha kuelewa.

Wabheja sana.
 
mbona kuna mengine yako vilevile? na kama yamebadilika baadhi yamebadilishiwa ibara

mfano kwenye kipengele cha tunu za taifa zimetajwa
(a) kiswahili
(b) muungano
(c) utu na udugu
(d) amani na utulivu
haya yapo ktk ibr ya 5.

mengine yaliyotajwa kwa warioba bmk wamehamishia ibr ya 6 misingi ya utawala bora. ambapo yametajwa yote.

sasa shida ni kuitwa tunu za taifa au ni kuwepo kwake ktk katiba?

wajuzi tufundisheni.
 
Mimi nikisoma nikifika Uk.7 Sehemu ya Nne, Sura ya 21 (2), huwa naona hakuna haja ya kuendelea kusoma zaidi. Kwa kweli huwa naona kama kinyesi kimewekwa kwenye kisima cha maji.

Maji ya kisima yote yatakuwa contaminated hayafai kwa kunywa, biashara ya kusema "tutarekebisha" huko tuendako ni kudanganyana. Tuondoe kwanza uchafu huo na maji yake, tusafishe kisima ndipo tuanze upya kupata maji safi ambayo tutakwenda kuyachemsha kwa matumizi.

Katiba ya Chenge Uk. 7.jpg
 
Mimi nikisoma nikifika Uk.7 Sehemu ya Nne, Sura ya 21 (2), huwa naona hakuna haja ya kuendelea kusoma zaidi. Kwa kweli huwa naona kama kinyesi kimewekwa kwenye kisima cha maji.

Maji ya kisima yote yatakuwa contaminated hayafai kwa kunywa, biashara ya kusema "tutarekebisha" huko tuendako ni kudanganyana. Tuondoe kwanza uchafu huo na maji yake, tusafishe kisima ndipo tuanze upya kupata maji safi ambayo tutakwenda kuyachemsha kwa matumizi.

View attachment 227698
Ha ha ha bora hukudoma mkuu, maana mkuu wa sasa hana habari na hilo neno linaloitwa katiba mpya
 
Back
Top Bottom