Ubinafsi kikwazo kikuu Katiba Mpya

Ubinafsi kikwazo kikuu Katiba Mpya

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Hakuna asiyejua kuwa Katiba Mpya ni majumuisho ya mustakabala ulio bora zaidi katika uendeshaji wa nchi kwa wakati husika.

Hayupo mwenye akili timamu anayeweza kupinga matumizi au ujio wa mustakabala kama huo.

Taabu gani makwetu Tanzania basi?

Kwa hakika ubinafsi uliopitiliza ndiye aliye mchawi wetu mkuu.

Kuangalia tu yaliyo maslahi binafsi na kujiweka kando kwa lolote lisilokuwa na maslahi ya moja kwa moja kwetu ni kikwazo kikubwa. Kama hatushiriki shughuli za wengine, kwa nini wao washiriki zetu?

Yaliwakuta kina Lissu, Mbowe, Mdude, Ben Sanane, Azory, Lijenje, Mawazo nk.

Yakawakuta kina Polepole, Ndugai, nk.

Hivi yuko wapi Job Ndugai? Yuko huru, hai au mfu?

Kwanini tusitake kumwona Ndugai kwa juhudi ile ile kama tuliyo nayo kwa wenzetu akina Ben, Lijenje, Azory na wote waliopotezwa?

Kwa mwendo huu yatawakuta kina Mpina.

Yanawakuta Ukraine na pia Palestina.

Yanatukuta kwenye bei za mafuta.

Mwendelezo ni kila mtu kula na wa kwao.

Batili ni batili tu. Bila ya kuzikabili batili zote kama zinavyokuja, tuupate wapi umoja wetu muhimu wa kushughulikia ya halali yote yakiwamo ya Katiba Mpya?

Maneno mazito toka kwake Askofu Bagonza ni ya kuzingatia:

Wapinzani si wamoja. Kuna wapinzani-Katiba Mpya na Wapinzani-Nusu Katiba Mpya. Kuna wapinzani-Mtungi na Wapinzani-Mahela. Kuna Wapinzani-Zanzibar huru na Wapinzani-Zanzibar Mkoa. Unahitajika muafaka kati ya wapinzani kabla ya muafaka wa kitaifa.

Tunahitaji muafaka baina yetu.
------------------

Source:

Askofu Bagonza: Taifa linahitaji miafaka, siyo muafaka
 
Kiukweli Tanzania hakuna Wapinzani yote ni matawi ya CCM chini ya TCD!

Kwa hakika CCM wanaona hivyo.

Kwamba Polepole ikawa baridi tu kama vile. Leo kapotezwa Ndugai badala ya kudai kumwona hadharani tunamzodoa ajiuzuru ubunge eti kuwa hataki kwenda bungeni.

Kwani tunajua kama aliko yuko hai au yuko huru?
 
Upinzani wa Tanzania umeweka nguvu kubwa katika makundi yasiokuwa na tija kwa taifa letu. Mfano NCCR Mageuzi enzi za Mrema iliwekeza nguvu kubwa kwa wafanyabiashara mbali mbali, ili itapoingia madarakani wafanyabiashara hao waweze kuneemeka kupitia serikali waliopanga kuiweka wenyewe.

CUF pia ilikuwa hivyo hivyo hasa kwa wafanyabiashara wa kipemba. CHADEMA yenyewe imewekeza nguvu kubwa kwa wauza unga na mateja wao, wauza viloba na walevi wao, makamu mwenyekigoda kule ubelgiji akiwa mstari wa mbele kuwatetea machoko nk.

Kwahiyo kwa aina hii ya viongozi wa upinzani tuliona tusitarajie lolote la maana kutoka ndan ya wapinzani hao. Sana sana wanaofaidika au wataofaidika ni chawa tu ambao hudanganywa kwa viji bando na viela vya kula kwa kila chawa atakaeandika uzi unaohusu serikali au kiongozi wa serikali nk.
 
Upinzani wa Tanzania umeweka nguvu kubwa katika makundi yasiokuwa na tija kwa taifa letu. Mfano NCCR Mageuzi enzi za Mrema iliwekeza nguvu kubwa kwa wafanyabiashara mbali mbali, ili itapoingia madarakani wafanyabiashara hao waweze kuneemeka kupitia serikali waliopanga kuiweka wenyewe. CUF pia ilikuwa hivyo hivyo hasa kwa wafanyabiashara wa kipemba. CHADEMA yenyewe imewekeza nguvu kubwa kwa wauza unga na mateja wao, wauza viloba na walevi wao, makamu mwenyekigoda kule ubelgiji akiwa mstari wa mbele kuwatetea machoko nk. Kwahiyo kwa aina hii ya viongozi wa upinzani tuliona tusitarajie lolote la maana kutoka ndan ya wapinzani hao. Sana sana wanaofaidika au wataofaidika ni chawa tu ambao hudanganywa kwa viji bando na viela vya kula kwa kila chawa atakaeandika uzi unaohusu serikali au kiongozi wa serikali nk.

Kwa hiyo Riz moko, Askofu Rashid, Manji, na watuhumiwa wazungu wengine waliporukiwa na Jenerali Makonda ilikuwa ni katika kuwapunguza nguvu Chadema?

Si mseme tu wako wapi hawa:

Ayubu Ndugai, Ben Sanane, Azory Gwanda, Moses Lijenje na wengine mlioonekana nao mara ya mwisho?
 
Watanzania tuna Njaa tupe chakula tu. Mengine anasa
 
Watanzania tuna Njaa type chakula tu. Mengine anasa

Unaweza kuwa sahihi. Labda ni laana.

Kwa nini Polepole, Chalamila au Ndugai hawakuungwa mkono?

Kwani hawakujaribu kupambana kwa haki na establishment hata kama ilikuwa kwa kuchelewa mno?

Kwa nini Ndugai hafuatiliwi kujulikana aliko huru au hai?

Kwa nini Luhaga Mpina haungwi mkono?

Angalizo: Kutokuwaunga mkono hawa hakuhalalishi lingine lolote lililo batili.
 
Kwa hiyo Riz moko, Askofu Rashid, Manji, na watuhumiwa wazungu wengine waliporukiwa na Jenerali Makonda ilikuwa ni katika kuwapunguza nguvu Chadema?

Si mseme tu wako wapi hawa:

Ayubu Ndugai, Ben Sanane, Azory Gwanda, Moses Lijenje na wengine mlioonekana nao mara ya mwisho?
Mwenyekiti alishaonya kuwa msijaribu kuionja sumu yake kwa ulimi mtaangamia chawa wote kama walivyoangamia hao uliowataja. Jamaa ni silence killer, nashangaa hii kauli ya kuonja sumu kwa ulimi sijui ilimponyokaje ponyokaje aisee. Labda Mungu alitaka kumuumbua kutokana na aliyoyafanya huko nyuma kimya kimya. RIP Chacha Wangwe 🤲
 
Mwenyekiti alishaonya kuwa msijaribu kuionja sumu yake kwa ulimi mtaangamia chawa wote kama walivyoangamia hao uliowataja. Jamaa ni silence killer, nashangaa hii kauli ya kuonja sumu kwa ulimi sijui ilimponyokaje ponyokaje aisee. Labda Mungu alitaka kumuumbua kutokana na aliyoyafanya huko nyuma kimya kimya. RIP Chacha Wangwe 🤲

Ninatambua wote niliowataja mlionekana nao nyie kwa mara ya mwisho:

IMG_20220409_144811_547.jpg


Una maana kuwa wote hao baadaye mlimwita mwenyekiti kimya kimya kuja kuwaonjesha sumu?

Cc: Jumbe Brown
 
Umuhimu wa Katiba Mpya uko pale kila mmoja wetu anauona, kwa yule asieuona inabidi aulizwe kwanini yeye yuko tofauti na wenzake, na kuulizwa huko aulizwe wakati wenzie wanaendelea kuipigania Katiba Mpya, sio wote warudi nyuma ya mstari wa mapambano ili kumuuliza asiye tayari.

Sioni ubinafsi wowote kwenye hili, mtu kuamua kutangulia mbele kupigania utakacho huku ukiacha nafasi kwa asiye tayari kuja kujiunga nawe mbele ya safari, ni kuwa makini na ukitakacho, neno "ubinafsi" umelitumia vibaya.

Milango haijafungwa mpaka uite ubinafsi, kuliko kuendelea kupoteza muda kumsubiri mtu ambaye anakula mema ya nchi na watawala asiyejua madhila wengine wanayopitia, huku ni kupoteza muda na kuchelewesha kufikia malengo.
 
Umuhimu wa Katiba Mpya uko pale kila mmoja wetu anauona, kwa yule asieuona inabidi aulizwe kwanini yeye yuko tofauti na wenzake, na kuulizwa huko aulizwe wakati wenzie wanaendelea kuipigania Katiba Mpya, sio wote warudi nyuma ya mstari wa mapambano ili kumuuliza asiye tayari.

Sioni ubinafsi wowote kwenye hili, mtu kuamua kutangulia mbele kupigania utakacho huku ukiacha nafasi kwa asiye tayari kuja kujiunga nawe mbele ya safari, ni kuwa makini na ukitakacho, neno "ubinafsi" umelitumia vibaya.

Milango haijafungwa mpaka uite ubinafsi, kuliko kuendelea kupoteza muda kumsubiri mtu ambaye anakula mema ya nchi na watawala asiyejua madhila wengine wanayopitia, huku ni kupoteza muda na kuchelewesha kufikia malengo.

Ubinafsi unakuja hapa:

Huwezi tegemea watu kwenye shughuli ya mwenzio kama wewe hushiriki za wenzako.

Hali kadhalika kutoshiriki shughuli ya wenzio hakuokoi lolote lililopita.

Wako wapi hawa:

Ben Sanane, Moses Lijenje, Azory Gwanda, Job Ndugai nk haya si ya vyama, bali ya wapenda haki wote wasio kuwa wabinafsi.

Mifano zaidi ni kama ilivyo kwenye mada.

Siyo siri, tu jamii ya kujiangalia wenyewe. Lisilotuhusu moja kwa moja, hilo ni upuuzi tu.
 
Back
Top Bottom