Ubishi Umetuponza: Katiba Mpya Haiwezekani

Ubishi Umetuponza: Katiba Mpya Haiwezekani

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Ukisikiliza sana hoja za pande mbili zinazokinzana kuhusiana na mchakato wa Katiba Mpya unaweza kuamini kuwa tatizo ni UKAWA au CCM. Naomba kupendekeza kuwa tatizo ambalo tunalishushudia na ambalo tumeshalishuhudia huko nyuma ni la kina zaidi. Ni kutokukubali ukweli ndio maana watu bado wana matumaini ya kupata katiba mpya.

Tatizo la Msingi ni uharamu mzima wa mchakato huu; hili nimelionesha toka Kikwete alipotangaza 'nia' yake ya kuanzisha mchakato huu akiwa mwenyewe ni mvunjaji mkubwa wa Katiba ya sasa. Ikumbukwe kuwa Katiba ya sasa hairuhusu uandikwaji wa Katiba Mpya na Rais wa Jamhuri ya Muungano hana Mamlaka wala Madaraka ya kuanzisha mchakato wa kufuta Katiba iliyomwingiza madarakani na kuanzisha Katiba Mpya.

Wanasiasa wetu, wanaharakati, na Watanzania kwa ujumla walipokubali uharamu huu uwe halali walikuwa wamekubali matokeo ya uharamu huo. Ikatungwa Sheria iliyoweka upendeleo wa wazi ndani ya CCM na tukakubali; tukaona sheria hiyo ilivyotengenezwa kuharibu mchakato mzima tukalalamika lakini tukakubali.

Sheria hiyo iliyotungwa na magenius wetu ikaweka kuwa wajumbe wote wa Bunge la Muungano na Baraza la Wawakilishi kuwa ni wajumbe wa Bunge la Katiba. Hili wengine tulilipinga mapema lakini wanaharakati wetu walilikubali na kuwa sehemu ya mchakato huu haramu. Walijua toka mwanzo kwa kufanya hivyo 2/3 ya wajumbe wa Bunge la Katiba watakuwa ni wana CCM au watu wenye kusogeleana na kukonyezana na CCM kwa karibu!

Ukweli wa mambo unabakia kuwa mchakato huu hauendi popote. Mabingwa wetu watabishana, watasemana na kutunishiana macho lakini mchakato hauendi popote; fedha ishaliwa na Katiba Mpya haiji isipokuwa kama kwa kulazimisha. Hakuna uwezekano wowote ule wa kuwa na Katiba Mpya itakayoweza kutumika kwenye uchaguzi mkuu ujao. Kwa vile uwezekano huu haupo tunachoshuhudia sasa na tutakachoshuhudia wiki ijayo ni kuvunjika kwa mchakato huu na kama utaendelea tutashuhudia uharamu wake ukiongezwa kufanywa haramu.

Uhalali hautakuja kwa vikao, kwa makubaliano na kuombewa. Uhalali utakuja kwa kuufuta mchakato huu - siyo kuuahirisha tu - kukubali kuwa umekosewa toka mwanzo na hivyo kuacha uongozi ujao uanze mchakato upya. Lakini hata watu wakiombea na kufunga uharamu hauondoki kwani uharamu huu si mapepo.

MMM
 
Tupo tuliosema msimwachie Rais auhodhi mchakato huu. Wapo waliobisha ila leo wanalalamika. Hayo ndiyo matokeo ya kumwachia madaraka makubwa ya kuteua wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Baraza Maalum la Katiba. Yamepelekea pia kupata Wenyeviti kutoka Chama Tawala. Na kupata Mwenyekiti aliyekuwa anamwongezea maneno Rais wakati anahutubia leo. Kazi kubwa kwa wanaodai Serikali 3 sasa ni kuwashawishi wajumbe wapatao 80 ambao kwa mujibu wa hesabu alizochambuliwa Rais ndio wanahitajika kupata hiyo theluthi mbili ya kura kuipitisha. Na kwa Chama Tawala kazi rahisi ni kuwashawishi (kuwatisha?) wajumbe wapatao 16 ambao kama hesabu alizozisema Rais ziko sawa ndio wanahitajika kupitisha Serikali 2. Pia hapo tujiulize hizo hesabu alipigiwa lini - je, kabla au baada ya kuwachagua wale wajumbe 201 wasio wabunge?

"Ndiyo maana, wachache wetu tulipendekeza tuwe na Bunge Maalum la kuchaguliwa na wananchi moja kwa moja. Lakini watawala wetu, pamoja na watawala watarajiwa na wengi wa wanaharakati, katika busara zao na kwa maslahi yao, hawakutilia maanani pendekezo letu. Tumepoteza nafasi ya kipekee ya kihistoria ya kuwa na Bunge Maalum la kuchaguliwa, jambo ambalo limetufikisha hapa tuliko" - Profesa Issa Shivji: Dhana na Maana ya Bunge Maalum la Katiba

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...e-wa-bunge-la-katiba-someni-ili-msiyumbe.html


 
Acha unafiki wewe usiyejitambua!!! Bendera hufuata upepo huns msimamo kabisa miaka mitano ya dhalimu magufuli ulimkubatia huyo dhalimu bila hata aibu.
Mkuu si kila anepingana nawe kimitizamo ni adui,

Huenda yeye aliangalia pande zote za Magufuli, na kwake mazuri yakawa mengi kuliko mabaya

Mimi nashauri umkosoe kwa hoja zenye ushawishi, kuliko kumtusi.
 
Kwa jinsi alivyokuwa akiandika huyu wakati wa Kikwete KAMWE asingeweza kumuunga mkono dhalimu magufuli. Ghafla tu abadilika na wengi tuliomfahamu humu tukabaki na mshangao mkubwa. Kule Twitter haandiki siku hizi kutokana na kupigwa madongo kwa UNAFIKI wake. Uzuri wa mtandao huwa HAUDANGANYI ukiwa mnafiki iko siku tu UTAADHIRIKA.

Mkuu si kila anepingana nawe kimitizamo ni adui,

Huenda yeye aliangalia pande zote za Magufuli, na kwake mazuri yakawa mengi kuliko mabaya

Mimi nashauri umkosoe kwa hoja zenye ushawishi, kuliko kumtusi.
 
Hivi mnafaidkaje na upuuzi tuliouona wakati wa Magufuli?
Ukisikiliza sana hoja za pande mbili zinazokinzana kuhusiana na mchakato wa Katiba Mpya unaweza kuamini kuwa tatizo ni UKAWA au CCM. Naomba kupendekeza kuwa tatizo ambalo tunalishushudia na ambalo tumeshalishuhudia huko nyuma ni la kina zaidi. Ni kutokukubali ukweli ndio maana watu bado wana matumaini ya kupata katiba mpya.

Tatizo la Msingi ni uharamu mzima wa mchakato huu; hili nimelionesha toka Kikwete alipotangaza 'nia' yake ya kuanzisha mchakato huu akiwa mwenyewe ni mvunjaji mkubwa wa Katiba ya sasa. Ikumbukwe kuwa Katiba ya sasa hairuhusu uandikwaji wa Katiba Mpya na Rais wa Jamhuri ya Muungano hana Mamlaka wala Madaraka ya kuanzisha mchakato wa kufuta Katiba iliyomwingiza madarakani na kuanzisha Katiba Mpya.

Wanasiasa wetu, wanaharakati, na Watanzania kwa ujumla walipokubali uharamu huu uwe halali walikuwa wamekubali matokeo ya uharamu huo. Ikatungwa Sheria iliyoweka upendeleo wa wazi ndani ya CCM na tukakubali; tukaona sheria hiyo ilivyotengenezwa kuharibu mchakato mzima tukalalamika lakini tukakubali.

Sheria hiyo iliyotungwa na magenius wetu ikaweka kuwa wajumbe wote wa Bunge la Muungano na Baraza la Wawakilishi kuwa ni wajumbe wa Bunge la Katiba. Hili wengine tulilipinga mapema lakini wanaharakati wetu walilikubali na kuwa sehemu ya mchakato huu haramu. Walijua toka mwanzo kwa kufanya hivyo 2/3 ya wajumbe wa Bunge la Katiba watakuwa ni wana CCM au watu wenye kusogeleana na kukonyezana na CCM kwa karibu!

Ukweli wa mambo unabakia kuwa mchakato huu hauendi popote. Mabingwa wetu watabishana, watasemana na kutunishiana macho lakini mchakato hauendi popote; fedha ishaliwa na Katiba Mpya haiji isipokuwa kama kwa kulazimisha. Hakuna uwezekano wowote ule wa kuwa na Katiba Mpya itakayoweza kutumika kwenye uchaguzi mkuu ujao. Kwa vile uwezekano huu haupo tunachoshuhudia sasa na tutakachoshuhudia wiki ijayo ni kuvunjika kwa mchakato huu na kama utaendelea tutashuhudia uharamu wake ukiongezwa kufanywa haramu.

Uhalali hautakuja kwa vikao, kwa makubaliano na kuombewa. Uhalali utakuja kwa kuufuta mchakato huu - siyo kuuahirisha tu - kukubali kuwa umekosewa toka mwanzo na hivyo kuacha uongozi ujao uanze mchakato upya. Lakini hata watu wakiombea na kufunga uharamu hauondoki kwani uharamu huu si mapepo.

MMM
 
Huu uzi aliandika miaka 7 iliyopita lakini kwa UNAFIKI wake kipindi chote cha miaka 7 hakuona umuhimu wa kuufufua hadi hii leo!!! STUKA Mkuu.

Mkuu si kila anepingana nawe kimitizamo ni adui,

Huenda yeye aliangalia pande zote za Magufuli, na kwake mazuri yakawa mengi kuliko mabaya

Mimi nashauri umkosoe kwa hoja zenye ushawishi, kuliko kumtusi.
 
Mjitoe Jumuiya ya Madola muone urahisi wa kuwa na Katiba mpya.

Bibie kule yupo na Hayati J.P.M
Na huyo Mfalme kabla hajasimikwa rasmi aelewe kuwa tuna Ulazima wa kujitoa ili tuweze kuamua mambo yetu.
 
Kwa jinsi alivyokuwa akiandika huyu wakati wa Kikwete KAMWE asingeweza kumuunga mkono dhalimu magufuli. Ghafla tu abadilika na wengi tuliomfahamu humu tukabaki na mshangao mkubwa. Kule Twitter haandiki siku hizi kutokana na kupigwa madongo kwa UNAFIKI wake. Uzuri wa mtandao huwa HAUDANGANYI ukiwa mnafiki iko siku tu UTAADHIRIKA.
Nilimchukia kikwete sana,kwa sababu ya ufisadi,ulojolojo na utepetevu wa serikali yake,

Nilimpenda magufuli kwa sababu ya ushupavu wake wa kiuongozi na kutokubali kucheka na wezi wa Mali ya umma,
 
Back
Top Bottom