Ubora wa choroko (mung beans) ule na kimelea.

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011





Choroko ni zao tunalolitumia sehemu nyingi, wengi tunakula choroko kama kitweo. Kupata ubora wa ziada katika choroko ni kula na kimelea, katika halii hii unapata protein kwa ubora wake. Hii pia ni nzuri kwa wale waliopumzika kula nyama au kuamua kuwa walaji wa mboga mboga.

Chukua kikombe cha choroko, zioshe tu usiziloweke, zitoe kwenye maji, taarisha ungo weka tea towel au paper towel kwenye ungo kuepusha mchuruziko wa maji. Weka choroko zako humo na uziache sehemu kavu kama juu ya kabati. Zirudie baada ya siku mbili utaona zimeota vimelea. Hizi ziko tayari kuliwa. Una weza kuzichanganya kwenye kachumbari au bakuli la salad.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…