Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Siku ya jana Tume Huru Ya Uchaguzi ilikamilisha uboreshaji wa Daftari lake la kudumu lkatika mikoa ya Dodoma na Singida, ambapo uboreshaji katika maeneo hayo ulianza tarehe 25 Septemba 2024 na kumalizika rasmi tarehe 01 Oktoba 2024.
Zoezi hilo lilianza rasmi mwezi Julai katika mikoa ya Kigoma, Tabora, na Katavi, kabla ya kuendelea katika mikoa ya Geita, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, na Manyara, ikihusisha Halmashauri za Wilaya za Babati, Hanang, Mbulu, na Mji wa Babati.
Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kazi hiyo ya kusasisha daftari hilo la kudumu la wapiga kura ilihusisha baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Dodoma, Mkoa wa Singida, na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Manyara.
Akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa wadau wa uchaguzi jijini Dodoma, Mhe. Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Mbarouk Salim Mbarouk, alifafanua kuwa mzunguko wa tano wa uboreshaji ulijumuisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri za Wilaya za Bahi, Chamwino, na Kongwa.
Aidha, maeneo ya Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Wilaya za Kiteto na Simanjiro mkoani Manyara, pamoja na Mkoa wa Singida, yalishahusishwa katika zoezi hilo kna kuongeza kuwa kikawaida vituo vya uandikishaji hufunguliwa kila siku kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni.
Katika mkutano mwingine wa wadau uliofanyika mkoani Singida, Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari, alieleza kuwa Tume imechukua hatua za kiteknolojia kwa kuboresha mfumo wa uandikishaji.
Mfumo huo mpya unamruhusu mpiga kura aliyesajiliwa kuweza kuboresha taarifa zake au kubadilisha kituo cha kupigia kura kwa kutumia simu au kompyuta. Hatua hii inalenga kurahisisha mchakato mzima wa uboreshaji wa daftari.
Kwa mujibu wa ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura inatarajiwa kukamilika mwezi Machi 2025.
Zoezi hili ni sehemu muhimu ya maandalizi kuelekea uchaguzi ujao, likiwa na lengo la kuhakikisha wapiga kura wanapata fursa ya kuboresha taarifa zao kwa wakati.
Soma Pia
Zoezi hilo lilianza rasmi mwezi Julai katika mikoa ya Kigoma, Tabora, na Katavi, kabla ya kuendelea katika mikoa ya Geita, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, na Manyara, ikihusisha Halmashauri za Wilaya za Babati, Hanang, Mbulu, na Mji wa Babati.
Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kazi hiyo ya kusasisha daftari hilo la kudumu la wapiga kura ilihusisha baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Dodoma, Mkoa wa Singida, na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Manyara.
Akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa wadau wa uchaguzi jijini Dodoma, Mhe. Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Mbarouk Salim Mbarouk, alifafanua kuwa mzunguko wa tano wa uboreshaji ulijumuisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri za Wilaya za Bahi, Chamwino, na Kongwa.
Aidha, maeneo ya Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Wilaya za Kiteto na Simanjiro mkoani Manyara, pamoja na Mkoa wa Singida, yalishahusishwa katika zoezi hilo kna kuongeza kuwa kikawaida vituo vya uandikishaji hufunguliwa kila siku kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni.
Katika mkutano mwingine wa wadau uliofanyika mkoani Singida, Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari, alieleza kuwa Tume imechukua hatua za kiteknolojia kwa kuboresha mfumo wa uandikishaji.
Mfumo huo mpya unamruhusu mpiga kura aliyesajiliwa kuweza kuboresha taarifa zake au kubadilisha kituo cha kupigia kura kwa kutumia simu au kompyuta. Hatua hii inalenga kurahisisha mchakato mzima wa uboreshaji wa daftari.
Kwa mujibu wa ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura inatarajiwa kukamilika mwezi Machi 2025.
Zoezi hili ni sehemu muhimu ya maandalizi kuelekea uchaguzi ujao, likiwa na lengo la kuhakikisha wapiga kura wanapata fursa ya kuboresha taarifa zao kwa wakati.
Soma Pia
- Mbunge Christina Mnzava Azindua Uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Wilayani Kahama
- Dodoma: Tume ya Uchaguzi yawanoa Maafisa wa Polisi kuelekea uchaguzi
- Tume Huru ya Uchaguzi yakamilisha mchakato wa kutoa elimu kwa wananchi Zanzibar. Mchakato wa uandikishaji umeanza rasmi leo!
- Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutekeleza uboreshaji wa daftari la wapiga kura kisiwani Zanzibar kuanza Oktoba 7 hadi 13, 2024
- Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutekeleza uboreshaji wa daftari uboreshaji wa daftari la wapiga kura Arusha kuanzia Disemba 11 hadi 17, 2024
- Iringa: Kuna ongezeko la vituo 140 vya uandikishaji wananchi kwenye daftari la kudumu la mpiga kura
- Tume ya taifa ya Uchaguzi yatoa onyo kwa wananchi watakaojiandikisha zaidi ya mara moja!
- Afisa Uandikishaji Halmashauri ya Mbeya: Msilewe na kutumia vilevi wakati mnaandikisha wananchi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura
- Tume ya Taifa ya Uchaguzi yatangaza kuanza kuandikisha wananchi kwenye daftari mkoani Songwe, Njombe, Rukwa na Ruvuma kuanzia Januari 12
- Lindi: Wapiga kura wapya 121,187 watarajiwa kushiriki kwenye Uchaguzi mkuu mwaka 2025
- Lindi: Mkuu wa wilaya ya Nachingwea aboresha taarifa zake kwenye daftari la kudumu la mpiga kura
- Tume Uchaguzi: Wapigakura 594,494 wanatarajiwa wakuondolewa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura kwa kukosa sifa
- Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi: Ukijiandikisha mara 2 ili kupiga kura, adhabu ni jela kuanzia miezi 6
- Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi yatangaza kufanya uboreshaji wa daftari mkoani Tanga kuanzia Februari 13, 2025
- Picha: Washiriki wa mafunzo ya waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki Tanga wakila kiapo kabla ya kuanza mafunzo
- Mwenyekiti Tume Huru ya Uchaguzi: Hudumieni vizuri wateja wenu, kwa upole na waelekezeni kwe unyenyekevu
- Tanga: Afisa Mwandikishaji Handeni ataka waandikishaji wasaidizi kutunza siri za wananchi watakaojitokeza kujiandikisha
- Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuanza kuandikisha wananchi wa Morogoro kuanzia Machi 1. Wapigakura 302,752 watarajiwa kuandikishwa!
- Picha: Tume Huru ya Uchaguzi yatinga mtaa kwa mtaa mkoani Morogoro kuhamasisha wananchi kujiandikisha