Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.

Ben Saanane

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2007
Posts
14,580
Reaction score
18,193
2008-08-09 09:37:58
Na Simon Mhina

Kuna taarifa kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza kumshawishi Profesa Samwel Wangwe Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, awanie ubunge Jimbo la Tarime, kumrithi mdogo wake marehemu Chacha Wangwe.


SOURCE: Nipashe


BTW.Kuna siku nilisema CCM watataka kumsimamisha kaka wa Marehemu ili kupata Sympathy votes maanke katika hali ya kawaida walijua itakua ngumu sana.Nina mashaka sana na hili jambo,interest za CCM kwenye hiki kifo ,imenishangaza sana
 
Last edited by a moderator:
Ben,

wewe unashangazwa na interest za CCM tu?bila hata kuongelea na interest za NCCR na TLP?

huu ni mwanzo,ila tusubiri tuone
 
Ben,

wewe unashangazwa na interest za CCM tu?bila hata kuongelea na interest za NCCR na TLP?

huu ni mwanzo,ila tusubiri tuone

Mkuu,hata mwili bado hujapoa? They are faster like nothing!

Sasa hapa nimeachwa hoi kabisa.
 
Mkuu,hata mwili bado hujapoa? They are faster like nothing!

Sasa hapa nimeachwa hoi kabisa.

Hao wengine nasikia walianza kampeni siku ile ile mazishi yalipoahirishwa!
 
Mnachekesha kweli, CCM haina nafasi hapa nyumbani, hata tuchukue gogo na huyo wa CCM gogo litashinda, CHADEMA NI CHAMA MBADALA ,
 
Mnachekesha kweli, CCM haina nafasi hapa nyumbani, hata tuchukue gogo na huyo wa CCM gogo litashinda, CHADEMA NI CHAMA MBADALA ,

Isayamwita,

Kiteto mungeliweka gogo pia labda lingeshinda. Ndio maana CCM wanashinda kirahisi, kuna watu wanashindwa hata kukubali the reality na matokeo yake badala ya kutafuta mbinu za kupambana na CCM wanabaki kushinda kwenye vijiwe wakiamini CCM wataanguka.

Sitashangaa CCM wakishinda Tarime safari hii hasa kama Prof. Wangwe ndiye atakuwa mgombea wao.
 

Mtanzania

Hata tukikuchukua jinsi ulivyo mzee ukasimama upande wa chadema kule Tarime, basi mjengoni ni lazima ulindime.Kwa habari za kiteto sisemi kitu. tumekubali kwa yote yaliyojili.
 
Mtanzania

Hata tukikuchukua jinsi ulivyo mzee ukasimama upande wa chadema kule Tarime, basi mjengoni ni lazima ulindime.Kwa habari za kiteto sisemi kitu. tumekubali kwa yote yaliyojili.

Mhh,No comment!
 
Ili prof ashinde ni lazima akisaliti chama chake cha CCM na aingie CHADEMA hapo ushindi ni mnono, hana mpinzani kwa hilo

Mkuu,

Sasa unajua CCM ni ma-opportunists ndio maana wanaanza kumshawishi Prof.Wangwe.Unakumbuka hata kwenye Mazishi ya mdogo wake bado kuna watu walimtukana kwamba au na yeye anataka lile Jimbo? So in order to compromise with political situation hana budi kuingia kupitia Chadema au chama kingine.

Nakuambia CCM hapa wameonyesha uroho wa madaraka wa hali ya juu kuliko kuthamini ubinadamu.

Makamba na ule waraka pia hawawezi kutenganishwa ingawa aliona moto unamuwakia akakwepa.Makongoro nae anajaribu kuwa smart ktk siasa zetu hizi lakini kwa sasa ni bora akakaa kimya zaidi
 
Mtanzania

Hata tukikuchukua jinsi ulivyo mzee ukasimama upande wa chadema kule Tarime, basi mjengoni ni lazima ulindime.Kwa habari za kiteto sisemi kitu. tumekubali kwa yote yaliyojili.

Isayamwita,

Kwi kwi kwi!! ujumbe umefika mkuu. Waswahili walisema akutukanaye hakuchagulii tusi.
 
Isayamwita,

Kwi kwi kwi!! ujumbe umefika mkuu. Waswahili walisema akutukanaye hakuchagulii tusi.

Mtanzania,

Usinielewe vibaya kabisa, nasema hivyo kwa sababu za msingi kabisa, je wajua kuwa sisi wana Tarime Serikali ya CCM ilitutelekeza siku nyingi? wajua kuwa uchaguzi wa 1995,2000 walikwiba ? ugomvi wetu uko hivi , mji wa tarime umejengwa na dhahabu ya nyamongo, kitendo cha serikali ya ccm kuwanyang'anya wachimbaji wadogowadogo hakika iko siku kitaeleweka.

Na ndiyo maana nasema wewe jiite mkurya nenda pale tarime gombea kupitia CHADEMA Mjengoni ni lazima ulindime Mkuu.
 
SISIEMU wanahangaika bure, na wala hawana haja ya kuharibu pesa yao kwa ajili ya kampeni katika jimbo la Tarime. SISIEMU haikubaliki hata kidogo, nakubaliana na IsayaMwita kuwa unaweza kuweka gogo against mgombea wa SISIEMU na gogo likashinda. Watu wa Tarime ni watu wa principle na msimamo thabiti. Hawataangalia kama Prof. Wangwe ni mdogo wa Marehemu, hakuna cha sympathy kwenye maslahi ya jimbo lao. Kama Prof. Wangwe atakuwa na mpango huo wa kurithi jimbo ni vema akaamia chama kingine tofauti na SISIEMU.
Ukweli utabaki palepale, SISIEMU haikubaliki Tarime.
 

Indume
Naona umenisoma, hakika CCM haina chake hapa nyumbani na si vinginevyo,
 
Jimbo apewe Mzalendo wa kweli...Ajiunge na chadema ama wafanye makubaliano...All in all...Vyama vyote ni muhimu kusimamisha mgombea mmoja wa upinzani hapo....Ama hata mgombea HURU kama ikiruhusiwa..Maana wote tunajuwa watu wa Tarime ni wajanja sana tu na wanajuwa utajiri wao..Kutokuwasikiliza ni sawa na kukaribisha vita ya wenyewe kwa wenyewe.
 
Naomba niwawekee habari hii iliyotoka kwenye Tanzania Daima mara baada ya matokeo ya uchaguzi mdogo wa Kiteto kutangazwa


Naomba habari hii ijadiliwe kuhakiki nguvu ya ushindi wa CCM pale Kiteto kwamba ilikuwa wingi wa kura ilizopata ama ununuzi wa shahada za wapiga kura, ama matumizi makubwa ya nguvu za dola (nitawawekea picha za vipgo walivyofanyiwa CHADEMA baadaye),
Kwa taarifa ya discussants hapa jukwaani CHADEMA Kiteto waliandikiana barua 24 kwa muda usiozidi mwezi mmoja na Msimamizi wa Uchaguzi kulalamikia faulu mbali mbali bila hatua yoyote kuchukuliwa (Nakala za barua hizo zikihitajika zitawekwa hapa wazi wazi)

Tuendelee kuadili ili tufikie ukweli kule Kiteto CCM walishindaje? Na je watashindaje huko Tarime?
 
...Maana wote tunajuwa watu wa Tarime ni wajanja sana tu na wanajuwa utajiri wao..Kutokuwasikiliza ni sawa na kukaribisha vita ya wenyewe kwa wenyewe.

When was the last time you had psychiatric evaluation, jmush1? And who told you that kutowasikiliza watu wa Tarime ni sawa na kukaribisha vita ya wenyewe kwa wenyewe? C'mon man! The fact of matter is, citizens of Tarime are too smart than you think! Kwahiyo usitake ku-generalize mambo hapa kwa kuwa-paint watu wa Tarime kama watu wasioweza ku-resolve issues kwa njia nyingine isipokuwa kwa fujo tu. And by the way, ni watu gani Tanzania kama sio watu wa Tarime ambao walikuwa wa kwanza kifunidisha nchi kuhusu nini maana ya mageuzi ya kweli?
 

MAGEUZI YA KWELI HAPA TANZANIA YATATOKA MARA, SIKU ZAJA WAKATI WASOGEA, SIKU UTAONA AKINA NIMROD MKONO, BUTIKU, MAKONGORO NA WENGINE WENGI, WAMEHAMIA CHADEMA MJUE UKOMBOZI UMEKARIBIA, HAPA TARIME BADO CHADEMA ITASHINDA TU, SIKU YAJA CCM WATABAKI SITOFAHAMU, MUNGU IBARIKI MARA, MKOA WA WALE WANAOJITOA KAFARA(SADAKA) ILI TAIFA HILI LIPONE, ALIANZA MWALIMU, NA SISI TUTAFUATA.................................., HAIJALISHI.

Wana Mara hatuna ukabila, watu tunaolipenda taifa letu, jamani..............!!!!!

Tunajulikana kama matahira (MACHIZI)tusiyo na akili, laiti mwalimu angefufuka akayaona haya,basi yale aliyoyasema yangetimia.

Mwalimu alikwisha kiona chama chenye mwelekeo ni CHADEMA na ndiyo maana tutaendeleza fikra zake.

Vita dhidi ya mafisadi itaendelea tu, ninyi ni mashahidi ni wapi raia wameweza kupigania haki zao bila kuhofu serikali iliyomadarakani? tutaendelea kujitetea hadi tone letu la mwisho.

Tuungeni mkono basi watanzania wenzetu, vita hii isiwe yetu tu,Leo CHACHA KATANGULIA SISI TUKO NYUMA YAKE TU.

Ilikuwaje Makongoro akakisariti CCM siku zile? Hivyo hivyo ndinyo watakavyokisariti mara tena.
 
Safi sana wanatarime.Hawa mafisadi mpaka wakome.AFADHALI NINYI MNATAMBUA UHURU WENU
 
Mimi nashangazwa sana na tabia hii ya kurithiana vyeo hasa vya kisiasa.
Watanzania itabidi tujiulize kuwa huko Tarime kuna watanzania wangapi? Au kuna ukoo tu wa kina Wangwe ambao ndio wao tu amabao wanawajibu wa kugombea cheo cha Ubunge wa Tarime.
Raul Castro huko Cuba aliporithi cheo ya ndugu yake Fidel Castro sisi wengi tulivurupuka na kusema kitendo hicho si cha kidemkrasai. Sasa kwa nini CCM inamtongoza Prof.Wangwe ili angombee ubunge wa Tarime kwa maana cheo kile hapo awali kilikuwa ni cha ndugu yake?
Kama ni hivyo kwa nini CCM ile ile ilitowa jina la J.Kikwete kugombea urais wa Tanzania badala ya mtoto wa mzee Nyerere hususan Makongoro Nyerere kama wao wanaamini vyeo vya kisiasa vinarithiwa?
Tanganyika toka 1961 {Baada ya Uhuru) na Tanzania toka1964 (baada ya muungano) tuliuondoa Uchifu,Umangi na Usultani kwa vile vyeo hivi vyote vilihitaji urithi.Sasa ninyi CCM mnataka kurudisha Uchifu huko Tarime ili kina Wangwe warithiwe cheo cha Ubunge?

Ndio maana hata wabunge wengi wanalalamika kuwa serikali ya CCM sio ya kidemokrasia. Wacheni uppuzi huu.
Tanzania ina mambo mengi muhimu ya kuyafualiza, umasikini,umeme,uchumi na kadhalika.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…