Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Watu wa Tarime wamezoea kuchinjana na wala siyo sababu ya kuchonganishwa na wana siasa mimi nafikiri mpaka wetu ulitakiwa uwe mto Mara huko Tarime wana tabia ya Kenya ambako wamezoea kuchinjana
Heey, watch what you are saying now.
We are all Tanzanians.
 
Mkuu naona unafanya kazi ya Sheikh Yahya, utabiri...waachie wenye fani yao...nani kakwambia ni amepotea? nadhani ametumia haki yake ya kikatiba..

Lakini wewe ndugu yangu Ushi Wa Rombo, baabu kubwa yaani popote pale penye maneno ya Chadema hukosi, unajua unanimaliza sana mkuu sasa lete habari za huko Tarime bro maana wewe umeshindikana kabisa.

Ushi Wa Rombooo!
 
Uchaguzi huu si huru hata kidogo


08.10.2008 0140 EAT
Mgombea ubunge CHADEMA afunguliwa mashitaka


*Wamo pia mgombea udiwani, Mnyika
*CCM yapongeza mkong'oto wa Polisi

Na George John, Tarime
Majira

JESHI la Polisi mkoani Mara limewafunguliwa mashitaka matatu watu 29 wakiwamo akiwamo mgombea ubunge wa CHADEMA jimbo la Tarime, Bw. Charles Mwera.

na wagombea ubunge na udiwani wa chama cha demkrasia na maendeleo CHADEMA ambao juzi jioni walitiwa mbaroni kuwekwa mahabusu kwa saa zaidi ya nne katika kituo kikuu cha polisi mjini Tarime.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Bw. Liberatus Barlow, aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa jana, kuwa polisi walikata watu 29 juzi saa 1.15 usiku wakati wakitoka kwenye mkutano wa kampeni katika kitongoji cha Buhemba nje kidogo ya mji wa Tarime.

Alisema watuhumiwa hao wamefunguliwa kesi tatu za kufanya mkutano kinyume cha sheria, kufanya maandamano haramu na kuharibu mali, mashitaka ambayo polisi wanadai hivi sasa yanachunguzwa.

Kwa mujibu wa Kamanda Barlow maandamano hayo yalilenga kuharibu mali mbalimbali za wananchi wa Tarime vikiwamo vituo vya mafuta vya mjini hapa.

Miongoni mwa viongozi walioonja nguvu hiyo ya Kamanda Venance Tossi ni Mwenyekiti wa Taifa wa Vijana, Bw. John Mnyika, mgombea ubunge ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri Tarime, Bw. Mwera, mgombea udiwani kata ya Tarime Mjini, Bw. John Heche na mjumbe wa Halmashauri Kuu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama hicho mkoa wa Iringa, Dkt. Kigwitu Kapwani.

Wengine waliotiwa mbaroni katika kamatakamata hiyo ya Polisi ni Bw. Werema Mwita, Katibu Mwenezi wa Wilaya, Bw. Babu Range, Mkurugenzi Msaidizi wa Vijana na Bw. Alex Chacha, Meneja wa Kampeni za ubunge na udiwani na wanawake na watoto wenye umri wa chini ya miaka 16.

Alisema katika vurugu hizo, viongozi na wafuasi wao walivunja kwa mawe magari matatu yakiwamo mawili ya Polisi aina ya Land Rover namba TP0901 na TP1509 na basi la kiraia aina ya Scania namba T548AGN ambalo lilivunjwa kioo cha nyuma.

Kamanda Barlow alisema kutokana na watuhumiwa kukaidi amri ya Polisi, askari walilazimika kutumia nguvu kubwa ikiwa ni pamoja na kurusha mabomu ya machozi na risasi za moto na kufanikisha kuwatia mbaroni wahusika.

Hata hivyo, kutokana na wengine kujeruhiwa, walipewa fomu namba tatu (PF3) na kwenda kupata matibabu hospitali ya wilaya ya Tarime na kwamba wahusika wote wako nje kwa dhamana.

Hata hivyo, kutokana na polisi kurusha ovyo mabomu hayo hata sehemu zisizohusika, ilisababisha wananchi wengi kuchukizwa na kitendo hicho, ambacho kilisababisha baadhi ya wafanyabiashara kupoteza mali zao.

"Polisi hawakuwa na sababu ya kuturushia mabomu wakati hapakuwa na fujo, sasa angalia nimepoteza zaidi ya sh. 150,000 baada ya wateja kukimbia bila kulipa bili zao za vyakula na vinywaji," alidai mtu anayemiliki mgahawa wa Girango mjini hapa.

Naye Richard Mwaikenda, anaripoti kuwa wakati CCM imelipongeza Jeshi la Polisi kwa kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya viongozi na wafuasi wa CHADEMA, uongozi wa CHADEMA kwa upande wake, umelaani kitendo hicho na kukiita cha kinyama.

Kwa upande wa CCM, pongezi hizo zilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Propaganda wa Chama hicho, Bw. Richard Tambwe, katika mkutano na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Tarime.

Alisema Jeshi hilo limetimiza wajibu wake kwa kuwaadabisha wafuasi wa CHADEMA, akidai kwamba walikuwa wachokozi kwa kuwapiga mawe askari waliokuwa wanawaamuru kuacha maandamano.

Alisema mara nyingi CHADEMA ndio waanzilishi wa vurugu kwenye mikutano ya CCM na vyama vingine, likiwamo tukio la kumpiga mawe Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila alipohutubia kwenye viwanja vya Sabasaba.

Alizidi kuilaumu CHADEMA kuwa wafuasi wake wanaendeleza vurugu dhidi ya CCM kwa kuchoma na kumvisha mbwa sare za CCM.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, mjini Tarime jana, Mkurugenzi wa Vijana wa CHADEMA, Bw. John Mnyika, alilaani kitendo cha Jeshi hilo kutumia nguvu kwa kuwapiga mabomu ya machozi bila makosa wananchi na wafuasi wao.

Alisema kutokana na kitendo hicho alichokiita cha kinyama dhidi ya raia, jeshi hilo linatakiwa liombe radhi, kwani ni aibu kwao na kwa wananchi.

Pia Bw. Mnyika alikemea tabia ya askari, kuwakamata na kuwapiga viongozi na wagombea wa chama hicho na kuwapekua mifukoni na hatimaye kuwaibia fedha zao zikiwamo sh. 240, 000 za Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Iringa, Dkt. Kapwani.

Alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, Inspekta Jenerali Said Mwema kumkamata Kamanda aliyemtaja kwa
jina la Lyamba aliyedai aliendesha operesheni hiyo.

Katika sakata hilo, wafuasi wapatao 25 na viongozi kadhaa wakiwamo mgombea ubunge, Bw. Charles Mwera na mgombea udiwani, Bw. John Heche, kukamatwa, kupigwa na kuswekwa mahabusu kuanzia saa moja hadi saa 7 usiku walipoachiwa baada ya kuandikisha maelezo.

"Nashangaa polisi wanasema tulikamatwa kwa kosa la kuandamana bila kibali, hivi walitaka tutumie utaratibu gani wa kuondoka kwenye mkutano huo, kwani sisi tulijipanga viongozi na wagombea tukiwa kwenye magari manne, huku tukisindikizwa na baadhi ya wananchi waliokuwa wanatembea kwa miguu kwenda majumbani mwao," alihoji Bw. Mnyika.

Bw. Mnyika aliziomba Taasisi za kutetea haki za binadamu za kitaifa na kimataifa, kulaani na kukemea kitendo hicho alichokiita cha kinyama.
 
Sasa kama mambo ndiyo hivi katika jimbo moja tu la Tarime hiyo 2010 si watu watachinjana kama kuku? Halafu Rais wa nchi amekaa kimya wakati anaona nchi inatumbukia katika janga kubwa ambalo mwisho wake hakuna anayeujua. Maana kuna uadui mkubwa kati ya CHADEMA na CCM kama vile uadui kati ya wapalestina na wayahudi. Nchi yetu ikitumbukia kwenye janga la kuuana wenyewe kwa wenyewe basi viongozi wa sasa wa CCM akina Kikwete, Msekwa, Makamba na wale wote ambao ni viongozi wa zamani ambao wanaona hatari kubwa inayoinyemelea nchi yetu lakini kwa mshangao wa wengi wameamua kukaa kimya bila kukemea hali hiyo. Tumeona yaliyotokea Rwanda, Burundi, Kenya na Watanzania wengi tusingependa yatokee Tanzania.

Mungu tunusuru na janga linaloinyemelea nchi yetu.
 
Lakini wewe ndugu yangu Ushi Wa Rombo, baabu kubwa yaani popote pale penye maneno ya Chadema hukosi, unajua unanimaliza sana mkuu sasa lete habari za huko Tarime bro maana wewe umeshindikana kabisa.

Ushi Wa Rombooo!

Hahahaha mkuu wangu naona unaniunganisha na Chadema, well kwa kweli tarime ni changamoto kubwa kabisa kwa chama tawala....bila ajizi wala mazingaombwe nadhani jimbo haliwezi kurudi CCM. Sipo huko ila kwa taarifa nizipatazo upinzani upo juu hata kama wewe mkuu wangu hupendi, kama zengwe litapita basi litatokea lile ulipendalo ...

ushi
 
Sipo huko ila kwa taarifa nizipatazo upinzani upo juu hata kama wewe mkuu wangu hupendi, kama zengwe litapita basi litatokea lile ulipendalo ...

Mkuu Ushi,

Msimamo wangu uko wazi kabisa mkuu, kwamba CCM tayari ina wabunge 90%, sasa akiongezeka huku wa Tarime kutabdilika nini? Mkuu mimi ni mwanachama wa CCM damu, lakini siichukii Chadema wala chama chochote cha upinzani, ninachukia viongozi wasanii popote walipo bila kujali vyama vyao vya siasa.

Lakini heshima mbele sana Mkuu Ushi, salimia huko bro!
 

Mkuu Field Marshall ES, hili la wewe kuwa CCM nalijua sana sana ndo maana huko nyuma tulipishana kidogo ingawa ukiliangalia kwa makini tupo pamoja kwa masuala mengine. Unajua sana kujenga hoja hapo sifa nakupa, ila unazidiwa na uCCM labda sababu ya kuzaliwa humo hapo ndipo ninapokuwa na differ na wewe.....tuache hayo...wakati mwingine Field Marshall ES huwa unasimamia utaifa hili pia nakupongeza....mimi bwana nina speciality ya forensic medicine vipi tukiungana kama kweli wewe una jua mambo ya police investigation na criminology? usiweke UCCM tufanye kazi ya Utaifa!! unaweza ni PM pia....

Kata nondo mzee, vipi darasa lako? mimi niliopt kudropt hilo somo...
 
 
MKuu waachieni basi CHADEMA jimbo hili! 90 % is significant to bring changes mkiacha ufisadi na usanii...lakini hebu jivue magwanda ya kijani angalia faulo mnaoyoicheza CCM kule Tarime, hivi police ni jumuiya moja wapo ya CCM?

Huko Tarime kuna mikono mingi sana nasikia mpaka kina Odinga wapo huko, nafikri it is about time sasa vyama vtetu vya siasa vikagundua mbinu mpya za kampeni kwa sababu haiwezekani kuwa kila uchaguzi tukawa tunasikia yale yale tu,

Mkuu umesikia habari za CUF huko visiwani, subiri usikie uchaguzi ujao, wakati umefika wa ku-change strategy ikibidi basi ni kususia uchaguzi kama zimbabwe, hivi unajua kwua huwa kuna ruzuku maalum kwa ajili ya uchaguzi tukwa wgombea wote na vyama vyao?
 

Kazi ipo mkuu wangu....pamoja kuwa tuna itikadi tofauti hebu tuweke masilahi ya taifa mbele...FM ES, tufanye nini ili wananchi wape muwakilishi wanayemtaka? changamoto hiyo
 

Mkuu FM,

Sasa chama chako watacheza faulo ingine tena zanzibar au watakubali yaishe tu, nafikiri katika swala zima la kuweka nchi mbele inabidi lianzie Tarime hasa kwa sasa na huko zanzibar siku hiyo ya 2010 ikifika.
 
Watu wa Tarime wamezoea kuchinjana na wala siyo sababu ya kuchonganishwa na wana siasa mimi nafikiri mpaka wetu ulitakiwa uwe mto Mara huko Tarime wana tabia ya Kenya ambako wamezoea kuchinjana

Ulisikia wachuna ngozi? walikuwa Tarime? Ulisikia wanaoua albino? walikuwa Tarime? Umesikia wapiga nondo watu usiku na mchana kwenye Vichochoro? wapo Tarime? Uliwahi kusikia mapanga ya Ubapa? Uliwahi kusikia Jiwe la Fatuma? Nayo ni Tarime..... should I say More.....
 

Afadhali umeliona hilo kwa sababu ndugu yetu alitaka kupotosha ukweli hapa na kuwasingizia wapenda amani kwa kesi ambayo siyo yao, if anything kwa yote yanayowakumba watu wa Tarime wanapaswa kuhurumiwa hasa na hii ubabe ubabe wa wanaotafuta kura.
 
Sasa chama chako watacheza faulo ingine tena zanzibar au watakubali yaishe tu, nafikiri katika swala zima la kuweka nchi mbele inabidi lianzie Tarime hasa kwa sasa na huko zanzibar siku hiyo ya 2010 ikifika.

Hawana njia ila ni serikali ya mseto tu ndio njia pekee ya kutokea, kwa sababu wazungu wameshamuonya Muungwana kuwa this time hawataruhusu watu wa CCM ku-cross kutoka bara na kwenda kupiga kura huko kama zamani.
 
Kampeni Tarime mwee! kunatetesi kwamba Mhe. Mbowa yupo na chopa yake na CCM wameingiza chopa mbili! duh. Mambo ya kampeni hayo, nguvu kubwaaaa!!

Lo salaale !! Makamba na Msekwa kwenye chopa, ni vitimbwi kama vya star wars lakini hivi vizee vitaweza kupambana na kizazi kipya. Hapa sheria lazima iwekwe kapuni na faulo iwe mtindo moja. Cry, the beloved Tarime, na peacekeepers tuwatoe wapi. If a**holes could fly, Tarime would be an airport!!
 

Mr. Mwanakijiji;
Ili kujifunza taaluma yoyote ile kwanza lazima tuwe na lugha. Taaluma au ujuzi tuliozonazo, kama zinapimwa kwa diploma ua degree au any measure, lazima zitegemee kutokana na lugha ambayo umetumia kuzipata. Kwa hiyo lugha ni muhumu sana (zaidi ya vyote) kufaulu katika taaluma au professional yako. Kama hujui lugha then huwezi kuelewa unachojifunza. Kwa hiyo Kama taaluma umeisomea katika kiingereza then lazima uwe unakijua kiingereza vizuri. Kama umechukua taaluma kwa kiswahili then lazima ujue kiswahili vema. Kiingereza, Kiswahili au lugha yoyote ile ambayo umejifunzia taaluma yako au professional yako ni muhimu sana. Huwezi kuniambia ati wewe ni engineer uliyejifunza kwa kiingereza halafu hujui kiingereza; au wewe ni engineer uliyefuzu kwa kichina halafu hujui kichina; otherwise we will be lying!
 
wanaosema wanamfahamu mwita tangu akiwa daruso mnakosea sana, huwezi kumhukukkumu mtu kwa kuangalia maisha yake ya uanafunzi watu wanabadilika sana baada ya kutoka shuleni,akina mbatia na wengine wanayofanya sasa ni tofauti sana na yale waliyoamini wakiwa pale mlimani, hata akina lowasa nk.

halafu, kuna hili linalojitokeza kuwa upinzani ukiwa na nguvu mahali fulani, tunaanza kuzungumza na kuhofu kuchinjana, haitawezekana upinzani uwe hafifu kwa ajili ya hadithi za rwanda na burundi
 
tumehama kwenye mjadala na kuhamia kwenye lugha, jibu ni kuwa makamba ni mwizi wa kura, na amedhamiria kuiba kura kule tarime jumapili, anaogopa hilo litamsuta mbele ya mabalozi
 
mapambano makali ya kampeni kuwania ubunge huko tarime sasa yamehamia kwenye kampeni za anga, wakati helikopta ya chadema ikiwa imeanza kazi rasmi, ccm wao wanapeleka helikopta mbili kabisa, visit mwanachi, breaking news
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…