Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Chadema wanaonyesha wako makini sana maana Mbowe alipoanza tu na helikopta hiyo wananchi hao. CCM kuona hivyo nao pruuuuuuuuuuuuuu na mbili. Angalieni wanaweza hata kutumia ya polisi.
 
Chadema iko juu alafu ccm ndo inafata.
Kilichowavutia watu sio helkopter ni mbowena na sera za chama chao juzi mbowe alipofika tarime watu wengi mji mzima walimiminika barabarani kumpokea mbowe maelfu ata rais alipokwenda tarime watu walio mpokea hawakuwa wengi kama mbowe alivyokuja tarime.Kwenye
mkutano ndo uliluwa umati mkubwa wa watu.
kajamaa ka ITV kamaratu akasemi ukweli wa mambo.
 
Wote wapuuzi. Yaani kweli Tarime wanahitaji helikopta? Wenzao wanatamba kwa kutumia mabasi kufanyia kampeni wakati sisi tunatambiana kwa helikopta! Mawazo yale yale ya wingi wa mashabiki ndio wingi wa kura. Mimi ningewasifu kama wote wangetumia baiskeli kuonyesha wanaelewa hali duni ya wananchi wao, kupunguza madhara ya mazingira na kuonyesha umuhimu wa mazoezi maana baada ya kampeni vitambi vyote vitakuwa history! Huku ni kutia chumvi kwenye kidonda na kuwadharau hao wapiga kura.
 
Hivi kweli helikopta inahitajika kweli kwenye uchaguzi wa jimbo dogo kama la Tarime? Nani analipia gharama zake? Hivi haya si ndiyo marehemu Wangwe aliyokuwa anayapinga??

Gharama za CCM nani analipa? Wao wanatumia mbili kazi kuiga kila kitu au makamba nae anataka kupanda helikopta?
 

Findi Mchundo nadhani hujui sababu inayowafanya watumie Helikopta. Tatizo ni barabara na ugumu wa kufanya mikutano mingi kwa siku moja sasa ukisema watumie baiskeli si itakuwa balaa.
 
Matumizi ya helkopter ni ubunifu uliobumiwa na campain team ya mgombea urais wa CHADEMA 2005, na kupata baraka ya vikao vya juu vya chama yaani Kamati kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, CCM walitubeza sana kwamba eti tunafuja fedha, niliwashangaa sana walipoleta Chopper kule Kiteto na sasa wanapeleka Chopper 2 Tarime, hii inawaonesha dhahiri kwamba wao ni Muflis, CHADEMA hatutegemei ushindi wa Tarime utatokana na matumizi ya Chopper, ushindi wa Tarime utatokana na rekodi ya utendaji wa kazi tulizozifanya tokea wananchi wa Tarime walipotupa ridhaa zao za kuwawakilisha Bungeni na pia tulipoanza kuiongoza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, hapo ndio ushindi wetu ulipo tunayo mengi ya kujivunia tuliyoyafanya na ambayo tunatarajia kuyafanya, Matumizi ya Chopper ni ili itupe urahisi tu kuwafikia watu katika maeneyo mengi na kwa muda mfupi tu na hii ni kutokana na miundombinu mibovu iliyojaa katika inchi yetu, ni maeneyo machache sana ambayo yanafikika kwa urahisi tena ni barabbara zilizounganisha mikoa tu, sasa ukiingia katika ngazi za Wilaya na Kata huko hakusemeki, sasa kama hawa wendawazimu wa CCM wanategemea Chopper 2 zitawapa ushindi Tarime dhana hiyo ni dalili ya kufilisika kisiasa
 
Hawana njia ila ni serikali ya mseto tu ndio njia pekee ya kutokea, kwa sababu wazungu wameshamuonya Muungwana kuwa this time hawataruhusu watu wa CCM ku-cross kutoka bara na kwenda kupiga kura huko kama zamani.
Kamanda mkuu FMES heshima kwako,
Hivi hawa jamaa kumbe walikuwa wao ndio wanaruhusu CCM ku-cross kisha wanatuzuga kwamba uchaguzi ulikuwa huru na haki eeh!
 
Hivi kweli helikopta inahitajika kweli kwenye uchaguzi wa jimbo dogo kama la Tarime? Nani analipia gharama zake? Hivi haya si ndiyo marehemu Wangwe aliyokuwa anayapinga??


Ni sahihi muda wa kampeni ndo umekwisha hivi.
Sasa unashangaa hao wana helikopta moja na hao mafisadi wanao leta helikopta 2 je utasemaje hapo?
 
CCm siku zote hawana ajenda za maendeleo.Hicho ni chama cha slogan wakati wa uchaguzi,muulize muungwana kuhusu ile slogani yake saa hizi kama anaikumbuka.

Wamekua ni watu wa kukopi kila kitu.It is nonesense,na hivi si walikua wanapinga matumizi ya helkopta? Iweje leo waibuke nazo mbili? Kweli CHADEMA wamewashika CCM pabaya na hawana pa kutokea
 
Kwanza,Mkamap nakuomba uje hapa utetee ule upuuzi wako uliokua unasema against CHADEMA kutumia helkopta
 
Findi Mchundo nadhani hujui sababu inayowafanya watumie Helikopta. Tatizo ni barabara na ugumu wa kufanya mikutano mingi kwa siku moja sasa ukisema watumie baiskeli si itakuwa balaa.

Kisingizio, Mkuu. Hizo barabara zimeanza kuwa mbovu leo? Kwani ni lazima hiyo mikutano mingi kwa siku moja lazima ihutubiwe na walewale? Mbona kwa wenzetu, wanagawana sehemu za kwenda na kuhutubia. Watasemaje wanajua machungu ya wananchi kama wanakwepa hizo barabara mbovu ambazo wanazitumia? Hapana, hizi ni zile zile siasa za Simba na Yanga. Zimejaa kutambiana zaidi kuliko substance. Heri wangepanda baiskeli angalau hivyo vitambi vingepunguka.
 
Yale mabezo ya Helicopter yako wapi sasa? Hawa CCM kwa kula matapishi yao hawawezekani? Sasa kama Chama kikongwe kinafikia mahali kinadhani kunapoteza wapenzi na wapigakura kwa ajili ya helicopter na sio uongozi mbovu basi KWISHA KAZI.KIONDOKE TUU.
 
Teh Teh teh teh! Duh,makamba ndani ya Chopa? Ha ha ha ha haaaa!
 
aibu taiweka wapi? Hatta hivyo katibu mkuu kama makamba ingetakiwa awe anajua hata lugha ya kiingereza,lakini kwa vile chama chenyewe ni CCM,then there is no need!
 



Nadhani hapo unawasema CCM zaidi maanke CHADEMA hakuna wenye vitambi,wote ni makomandooo.Sema na akina kepteni komba huko CCM na tapiamlo Makamba
 
Yale mabezo ya Helicopter yako wapi sasa? Hawa CCM kwa kula matapishi yao hawawezekani? Sasa kama Chama kikongwe kinafikia mahali kinadhani kunapoteza wapenzi na wapigakura kwa ajili ya helicopter na sio uongozi mbovu basi KWISHA KAZI.KIONDOKE TUU.

Kama kuna kitu kinatia kinyaa,ni mtu kula matapishi yake mwenyewe but kwa CCM imeonekana ni kawaida.Shame on them,they cannot invent something constructive!
 
kuna mtu anaitwa Mtanzania,najua hana uajsiri wa kuja kuliongelea hili suala
 
aibu taiweka wapi? Hatta hivyo katibu mkuu kama makamba ingetakiwa awe anajua hata lugha ya kiingereza,lakini kwa vile chama chenyewe ni CCM,then there is no need!
Nasikia anajua kuzungumza kwa ufasaha kabisa lugha tatu nazo ni KISWAHILI,KISAMBAA NA KIBONDEI. Huyo ndio Katibu Mkuu wa Chama Tawala Tanzania. Hongera sana Mheshimiwa Makamba kwa kumudu lugha tatu.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…