Uchaguzi 2020 Ubunge yawa kama mishemishe za ajira, mkoa wa Mara watia nia 462

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001


Fursa za ajira zinapotoka waombaji wanakuwa lundo sana, inaweza kutoka nafasi moja wakaomba watu 400. Ndicho kinachotokea kwenye kura za maoni kwa sasa.

Tazama Mkoa wa Mara watia nia 462. Ni kweli hawa wote wana wito na uwezo wa kutunga sheria na kusimamia serikali? Au wanasaka nini hasa.

Bado najiuliza, ila majibu ya awali yanaonyesha kwamba Bunge na nafasi ya mbunge imerahisishwa sana,imekosa hadhi iliyotukuka. Hii ni aibu kubwa kuona kila mtu anajiona anafaa kuwa mbunge. Wengine huwezi kuwafikiria hata ujumbe wa mtaa ila wamechukua fomu.

Nampongeza Rais kwa kupiga chini wale wote wenye tamaa ya madaraka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…