KERO Ubungo, Makoka kuna nyumba shimo la majitaka linahatarisha afya za majirani, Serikali ya Mtaa haimchukulii hatua

KERO Ubungo, Makoka kuna nyumba shimo la majitaka linahatarisha afya za majirani, Serikali ya Mtaa haimchukulii hatua

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mtaani kwetu Ubungo, Makoka, DSM

Maeneo ya Kilimahewa kuna jirani amejenga nyumba ya kupangisha ambayo wanaishi wapangaji tu yeye anaishi mbali na hapo.

Sasa tatizo linaanza, choo cha hiyo nyumba kinavuja shimo la majitaka limeharibika hivyo majitaka yenye athari kwa mazingira na wakazi wa eneo hilo.

Cha ajabu akipelekwa Serikali za Mitaa hachukuliwi hatua wala nini na akirudi mtaani anaanza kusema mbovu kwa majirani kiasi cha kuleta uadui.

Tunaomba msaada kwa hili, kuna hatari ya kipindupindu na pia hata usalama kwa watoto maana shimo lipo wazi sana na bado linatumika.

----
JamiiForums imefanya juhudi za kuwasiliana na Mamlaka husika Manispaa ya Ubungo ambapo wamekiri kuna changamoto hiyo.

Joina Nzali Afisa habari Manispaa ya Ubungo ameiambia JamiiForums kuwa

Ni kweli kuna mwananchi alichimba shimo kwa ajili ya choo lakini hakumalizia kufunika na hivyo kujaa maji kipindi cha mvua. Baada ya wananchi kutoa taarifa, Afisa Afya wa kata ya Makuburi amemwandikia Notisi ya siku 14 inayomtaka amalizie ujenzi wa shimo hilo au kulifukia ili kuondoa kero hiyo. Asipotekeleza agizo hilo hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa

Notisi alipewa tarehe 17.06.2024 na itaisha tarehe 30.06.2024. Baada ya hapo manispaa itatembelea kuona utekelezaji wake kama hajatekeleza hatua nyingine za kisheria zitafuata
 
Huwa inakera sana aisee mtaani kama chemba la majitaka linavuja, usiombe sasa kuwe uswazi nyumba zilikobanana halafu hiyo nyumba iwe na wapangaji shazi.

Kama Serikali za Mitaa wanazingua ninyi ibukeni Kata, huenda mkapata msaada.
 
Fika ofisi ya kata onana na mabwana afya watakusaidia kero yako iishe.
 
Mtaani kwetu Ubungo, Makoka, DSM

Maeneo ya Kilimahewa kuna jirani amejenga nyumba ya kupangisha ambayo wanaishi wapangaji tu yeye anaishi mbali na hapo.

Sasa tatizo linaanza, choo cha hiyo nyumba kinavuja shimo la majitaka limeharibika hivyo majitaka yenye athari kwa mazingira na wakazi wa eneo hilo.

Cha ajabu akipelekwa Serikali za Mitaa hachukuliwi hatua wala nini na akirudi mtaani anaanza kusema mbovu kwa majirani kiasi cha kuleta uadui.

Tunaomba msaada kwa hili, kuna hatari ya kipindupindu na pia hata usalama kwa watoto maana shimo lipo wazi sana na bado linatumika.
Mkuu wa mkoa na wa wilaya hawana muda wa kushughulika na kero kama hizi, wako bize kukimbizana na malaya.
 
JamiiForums imefanya juhudi za kuwasiliana na Mamlaka husika Manispaa ya Ubungo ambapo wamekiri kuna changamoto hiyo.

Joina Nzali Afisa habari Manispaa ya Ubungo ameiambia JamiiForums kuwa

Ni kweli kuna mwananchi alichimba shimo kwa ajili ya choo lakini hakulilimalizia kufunika na hivyo kujaa maji kipindi cha mvua. Baada ya wananchi kutoa taarifa Afisa afya wa kata ya makuburi amemwandikia Totisi ya siku 14 inayomtaka amalizie ujenzi wa shimo hilo au kulifukia ili kuondoa kero hiyo. Asipotekeleza agizo hilo hatua zingine za kisheria zitachukuliwa

Notisi alipewa tarehe 17.06.2024 na itaisha tarehe 30.06.2024. Baada ya hapo manispaa itatembelea kuona utekelezaji wake kama hajatekeleza hatua zingine za kisheria zitafuata
Tarehe 30 Juni si mbali.
 
Back
Top Bottom