Uchafuzi wa Lugha ya Kiswahili na ladha yake

Uchafuzi wa Lugha ya Kiswahili na ladha yake

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
Siku za karibuni kumekuwepo mlipuko (outbreak) ya matumizi mabaya ya maneno ya lugha ya Kiswahili katika majukwaa ya JF. Inaonekana ima watu wanaigana katika kuandika vibaya au hawajui wanaiga nini. Inawezekana anayeandika ni mtu mmoja akiwa na ID tofauti

Ladha ya lugha ni kutamkwa na kuandikwa kama ilivyo. Wapo waliozaliwa maeneo ambayo Kiswahili si lugha ya asili. Mmoja wa watu hao ni Mh Shibuda anayezungumza lugha nzuri sana ya Kiswahili licha ya kutoka mikoa ya kati, hajaathiriwa na herufi 'r'
Ni kama Mwalimu Nyerere aliyeongea Kiswahili kizuri sana licha ya kutoka mkoa kanda ya Ziwa.

Naomba niweke baadhi ya maneno yanayotia kinyaa na kutumika hovyo

JIRI na JILI Sahihi ni MSAJILI siyo MSAJIRI
RAU na LAU Sahihi ni DHARAU siyo DHALAU
URI na ULI Sahihi ni USHAURI siyo USHAULI, JEURI siyo JEULI
SIRI na THILI Sahihi ni KITHIRI siyo KISIRI, MITHILI siyo MITHIRI
BURI na BULI Sahihi ni KIBURI Siyo KIBULI
RI na LI Sahihi ni LIPUA Siyo RIPUA
PERE, PELE Sahihi ni PELEKEA Siyo PEREKEA

Hebu fikiria habari kama hii itakavyokutia maudhi ;

'' Msajiri na mkuu wa taaruma wamekubariana kushugurikia suara la mishala na masirahi ya wanachuo na watumishi.
Makamu mkuu amesema maandamano yamekisiri na kuasiri sana shuguli za taaruma.

Hivyo, ni muhimu jamii ya chuo ikae na kutoa ushauli nini kifanyike.
Majadiliano yasiwe na dhalau mithiri ya watu waliochanganyikiwa.
Vulugu zitaperekea kuhalibu usarama na amani ya chuo na hatua kari zitachukuriwa kwa wausika
Chuo hakitavumuria kibuli cha watu na watakaokaidi watakuwa wamejiripua wenyewe na kuperekea kupoteza usajiri wao katika chuo.
Shukulani sana''

Hayo ni baadhi ya maneno machache sana, niseme kuna matumizi ya ''RI' mabaya , yanatia kinyaa na kuharibu utamu wa lugha. Hakuna anayeweza kusema anamuda lugha kwa asilimia zote, hata hivyo yapo makosa ya wazi yasiyofaa kutendwa. Yanaudhi , yanatia karaha na kukihirisha. Hata kama lafudhi yako inakuelekeza vile ni lazima ukidhi haja ya lugha hivi.
 
Hivi yale mzee kifimbo cheza katokomeaga wapi? Au kafa
 
Halafu mkuu umeandika vibaya, Kiswahili unakiharibu, ubajifanya unakerwa wakati wewe mwenyewe unatukera
 
Siku za karibuni kumekuwepo mlipuko (outbreak) ya matumizi mabaya ya maneno ya lugha ya Kiswahili katika majukwaa ya JF. Inaonekana ima watu wanaigana katika kuandika vibaya au hawajui wanaiga nini. Inawezekana anayeandika ni mtu mmoja akiwa na ID tofauti

Ladha ya lugha ni kutamkwa na kuandikwa kama ilivyo. Wapo waliozaliwa maeneo ambayo Kiswahili si lugha ya asili. Mmoja wa watu hao ni Mh Shibuda anayezungumza lugha nzuri sana ya Kiswahili licha ya kutoka mikoa ya kati, hajaathiriwa na herufi 'r'
Ni kama Mwalimu Nyerere aliyeongea Kiswahili kizuri sana licha ya kutoka mkoa kanda ya Ziwa.

Naomba niweke baadhi ya maneno yanayotia kinyaa na kutumika hovyo

JIRI na JILI Sahihi ni MSAJILI siyo MSAJIRI
RAU na LAU Sahihi ni DHARAU siyo DHALAU
URI na ULI Sahihi ni USHAURI siyo USHAULI, JEURI siyo JEULI
SIRI na THILI Sahihi ni KITHIRI siyo KISIRI, MITHILI siyo MITHIRI
BURI na BULI Sahihi ni KIBURI Siyo KIBULI
RI na LI Sahihi ni LIPUA Siyo RIPUA
PERE, PELE Sahihi ni PELEKEA Siyo PEREKEA

Hebu fikiria habari kama hii;

'' Msajiri na mkuu wa taaruma wamekubariana kushugurikia suara la mishala na masirahi ya wanachuo na watumishi.
Makamu mkuu amesema maandamano yamekisiri na kuasiri sana shuguli za taaruma.

Hivyo, ni muhimu jamii ya chuo ikae na kutoa ushauli nini kifanyike.
Majadiliano yasiwe na dhalau mithiri ya watu waliochanganyikiwa.
Vulugu zitaperekea kuhalibu usarama na amani ya chuo na hatua kari zitachukuriwa kwa wausika
Chuo hakitavumuria kibuli cha watu na watakaokaidi watakuwa wamejiripua wenyewe na kuperekea kupoteza usajiri wao katika chuo.
Shukulani sana''

Hayo ni baadhi ya maneno machache sana, niseme kuna matumizi ya ''RI' mabaya , yanatia kinyaa na kuharibu utamu wa lugha. Hakuna anayeweza kusema anamuda lugha kwa asilimia zote, hata hivyo yapo makosa ya wazi yasiyofaa kutendwa. Yanaudhi , yanatia karaha na kukihirisha. Hata kama lafudhi yako inakuelekeza vile ni lazima ukidhi haja ya lugha hivi.
Sio hapa tu. Hii hatari imeingilia hadi vyombo vingine vya habari. Utakuta watangazaji wanachanganya Kiswahili na Kiingereza sijui ili waonekane wa "leo" au vipi. Huyu Barbra Hassan wa Clouds Power Breakfast ndio kinara wa huu mchezo wa kilimbukeni. Hii inachangia kutokumudu kujieleza kwa ufasaha aidha kwa Kiingereza au Kiswahili. Baraza la Kiswahili sijui liko wapi kwa kweli. Kuna hatari vijana wetu kuishia kutokujua aidha Kiswahili au Kiingereza. Huwezi kwenda "majuu" ukanza kuchanganya lugha hizi mbili na ukategemea utaeleweka. Ni vyema Baraza likakemea kwa nguvu zote huu ulimbukeni unaokuzwa na vyombo vya habari. Kama mtu anajifanya ni mwingereza basi atumie Kiingereza mwanzo mwisho na sio kudonoa donoa hapa na pale sijui ili aonekane "msomi". Inaudhi kweli kweli.
 
Sio hapa tu. Hii hatari imeingilia hadi vyombo vingine vya habari. Utakuta watangazaji wanachanganya Kiswahili na Kiingereza sijui ili waonekane wa "leo" au vipi. Huyu Babra Hassan wa Power Breakfast ndio kinara wa huu mchezo wa kilimbukeni. Hii inachangia kutokumudu kujieleza kwa ufasaha aidha kwa Kiingereza au Kiswahili. Baraza la Kiswahili sijui liko wapi kwa kweli. Kuna hatari vijana wetu kuishia kutokujua aidha Kiswahili au Kiingereza. Huwezi kwenda "majuu" ukanza kuchanganya lugha hizi mbili na ukategemea utaeleweka. Ni vyema Baraza likakemea huu ulimbukeni unaokuzwa na vyombo vya habari. Kama mtu anajifanya ni mwingereza basi atumie Kiingereza mwanzo mwisho na sio kudonoa donoa hapa na pale. Inaudhi kweli kweli.
Nimesoma magazeti tatizo la lugha ni kubwa.
Habari inaandikwa hadi kujiuliza kuna mhariri kweli
Maneno ya kiswahili rahisi sana yanaharibiwa, hakuna anayejali.
Kuna gazeti moja la kila siku na maarufu linaongoza kwa uozo wa lugha

Kuchanganya kiswahili na kiingereza ni kuonyesha mtu anamudu lugha zote wakati hamudu hata moja.Mitaani inaonekana kawaida, katika vyombo vya habari ni tatizo

Hivi hawa TUKI na Baraza la Kiswahili wanafanya nini kusaidia umma
Hizi ni taasisi zinazotia shaka kwa utendaji. Leo hii hatujui neno lipi ni sahihi kati ya haya mawili ' TANZIA au TAAZIA'

Hakuna utimilifu wa lugha kwetu sote, ni vema makosa ya dhahri yakaepukika
Neno Msajili linatumika sana, vipi mtu aandike Msajiri kana kwamba hajawahi kuliona popote?
Tena ukimuuliza atasema ni mwanafunzi au ni mfanyakazi
 
Mbona na wewe umeharibu kiswahili kwa kuchanga na kingereza et outbreak Mara ID umeshindwa kutumia lugha vzr
 
...Kuchanganya kiswahili na kiingereza ni kuonyesha mtu anamudu lugha zote wakati hamudu hata moja.Mitaani inaonekana kawaida, katika vyombo vya habari ni tatizo

Hivi hawa TUKI na Baraza la Kiswahili wanafanya nini kusaidia umma
Hizi ni taasisi zinazotia shaka kwa utendaji. Leo hii hatujui neno lipi ni sahihi kati ya haya mawili ' TANZIA au TAAZIA'...
Ndio hapo sasa. Hii tabia ninaanza kuiona hadi Bungeni. Yaani sasa wabunge ili waonekane "wamesoma" nao wameanza huu ulimbukeni. Hata TBC redio ya taifa haya mambo ya kiholela holea yanaachiwa tu. Katika nchi nyingine (hususan nchi za Ulaya) huu upuuzi haukubaliki hata kidogo. Mabaraza ya lugha yamepewa meno ya kukemea pale mtu anapojaribu kunajisi lugha kwenye vyombo vya habari, iwe Ujerumani, Ufaransa au hata nchi ndogo ndogo (kwa idadi ya watu) kama Sweden na Norway, kwa mfano. Utaona huyo Barbra Hassan ukimwambia jieleze sasa kwa Kiingereza mwanzo mwisho hawezi kabisaa. Sijui kuna faida gani kwa kweli. Ni kunajisi lugha tu. Sisi wenyewe hatujithamini tunataka nani atuthamini sasa? Baraza la Kiswahili halijui majukumu yake. Vijana wa leo wanaishia kutokujua aidha Kiingereza au Kiswahili. Baya zaidi na wasanii nao wameanza kuiga pidgin English ya wanaijeria wakidhani huo ndio "ukisasa" wenyewe kumbe wanajipoteza tu. Hao wanaijeria wanatumia pidgin kwa sababu hawana lugha ya kitaifa kama ilivyo kwetu kwa Kiswahili. Huu ulimbukeni unakera sana lakini basi tu.
 
Mbona na wewe umeharibu kiswahili kwa kuchanga na kingereza et outbreak Mara ID umeshindwa kutumia lugha vzr
ha ha ha, nimetumia neno mlipuko halafu nikaweka mabano(outbreak) ili kutofautisha kati ya (explosion na outbreak). Kwa lugha ya kiswahili mlipuko unaweza kuwa na maana zote
 
Kuna nyakati uvumilivu unakosekana, soma HAPA uniambie kosa la kiswahili

Soma vichwa vya habari tu, usisome habari nzima

FaizaFoxy
 
Back
Top Bottom