DOKEZO Uchafuzi Wa Mazingira: Mgodi wa almasi Shinyanga

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mfikirishi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
8,939
Reaction score
10,403
Huku taarifa za kina zikiendelea kutafutwa, Nimesoma kwenye mtandao wa Shinyanga Press Club kuwa Maji machafu na tope lenye kemikali limesambaa kuvamia makazi, mashamba na visima vya maji.

Madhara ya kiafya hayajaripotiwa lakini wananchi wenye taharuki washaanza kuyakimbia makazi yao.

Taarifa hiyo inaonesha picha mbali mbali za tukio hilo ambalo limethibitishwa na wananchi wa kijiji cha Ng’wang’olo Kata ya Mwadui Luhumbo.

Baadhi ya wananchi wameonekana wakikatiza ndani ya maji na matope hayo.



Tukio ni la jana asubuhi, tarifa zaidi zitakuja...

=====

UPDATES: 12 Nov 2022

======

Thread 'Shinyanga: Maji na tope la bwawa la Mgodi wa Almasi wa Williamson Diamond Ltd (WDL) havina madhara kwa binadamu' Shinyanga: Maji na tope la bwawa la Mgodi wa Almasi wa Williamson Diamond Ltd (WDL) havina madhara kwa binadamu
 
Ila waafrika tu na roho ngumuu, apo pichani watu wanakanyaga maji, huchelewi baadae kusikia wamepatwa changamoto za kiafya.

Wale samaki tuliambiwa walikufa kwa sababu ya mlundikano wa vinyesi vya wanyama, halikuwa fundisho kwa wahusika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…