Elections 2010 UCHAGUZI 2010: CCM Vs CCM

- Pamoja na CCM kushinda, bado historia inatakiwa kuwaandika Wapinzani na hasa Chadema kuwa ndio hasa washindi wa uchaguzi wa mwaka 2010.......


William.....una maana gani kusema ''pamoja na CCM kushinda''?

Mwenzetu labda una matokeo YOOOOOOTE ya uRAIS na uBUNGE. Tuwekee hapa mkuu. Sharing is caring!
 
Jamaa anasema Mwanza hakuna upinzani mkali ... mpaka sasa Mkoa wa Mwanza majimbo 3 yameenda upinzani. Wengine wa Sumve na Buchosa bado wamekaliwa kooni mpaka kieleweke

Adhabu nyingine huwa zinatolewa hapa hapa duniani. Masha aliuchuna wakati wanamtosa Bashe ati sio Raia wa Tanzania. Then akataka kutumia trick ile ile kwa mpinzani wake wa ubunge.

Heko wana wa Mwanza. Heko wana wa Nyamagana. Hizi kura za ubunge zinareflect pia matokeo ya kura za uRais ila tu kwa sasa wapo busy kumuokoa JK (kwa kuchakachua kura kwa speed ya rocket) na hawana muda wa kutosha kuchakachua za wabunge na ndio maana wanbunge wa CCM wapo wanakula mieleka tu
 
CCM ni kama dhambi ya asili, wengi walizaliwa wakajikuta nayo. Jipe moyo tuu. Tunajua jinsi ambavyo watu wengi watumishi wa serikali wanavyolazimisha kufuata itikadi zenu za kifisadi, sasa wamewapa somo. Mtambue kuwa cheo ni dhamana. Mlidhani hizo Tshirts na mabango ndiyo campaigne. Wengine mkapita nyumba kwa nyumba. Poleni, mlale mahali pema ...... Kwisha habari yenu:bowl:
 
Hili hitimisho ni mapema sana kulifikia kwa sababu mwaka 1995 Agustine Mrema alipata kura za Uraisi asilimia 38 rekodi ambayo JK kwa mtandao wake wa kuyachakachua matokeo ya Uraisi atahakikisha Dr. Slaa hataweza kuifikia hata chembe..................Mafanikio ya Chadema yatakuwa kwa wabunge kwani hadi hivi sasa tayari wamekwisha kuweka kibindoni wabunge 25 lakini siyo rahisi kumpa pongezi Dr. Slaa peke yake hapo kwa sababu wagombea pia walikuwa na mvuto kwa wapigakura................
 
Huko iringa mjini nasikia siku ya kufunga kampeni walikodi daladala karibu zote za pale mjini pamoja na magari mengine kwa ajili ya kusomba watu toka vijijini kuwapeleka mwembetogwa uwanjani lakini haikuwasaidia mwisho wa yote ni mgombea fulani kulazwa hosipitali.
 
-William tumekumiss sana hapa JF na tulikutegemea kuja kugombea angalau kiti kimoja kama ulivyokuwa umetuahidi kuwa wajitayarisha kuja kugombea, nini kilikusibu?

-William mbona hujatushukuru kwa kumuondoa Masha?????????

-William karibu Chadema tuunganishe nguvu kuiondoa sisi m mtandao ambao wanawamaliza sisi m asili.
Asante.
 
futa kwanza kauli yako mzee ..ukidai ccm againts ccm unakuwa hueleweki,ila nakubaliana na point yako kuwa dr Slaa wa ukweli ameshaingia kwenye historia ya Tanzania kwa kuwa mpinzani wa kwanza kuingia madarakani .right?


mbona william anasema mambo ambayo yamekuwa na yako wazi. mfano jimbo la mbeya mjini. sugu asingeshinda kama sio kampeni za chini kwa chini za baadhi ya very senior ccm officials mjini mbeya dhidi ya bwana "askofu" pamoja na slaa kumbeba sugu dakika za mwisho kwenye hitimisho la kampeni mbeya mjini. kwa nini mbeya vijijini chadema haikufanikiwa pamoja na kuwa na a very strong candidate??
 

Heshima kwako W.J Malecela.

Mkuu nakubaliana na wewe uchaguzi wa mwaka huu CCM wameparurana wenye kwa wenyewe lakini zipo sababu nyingi zilizochangia anguko la CCM.

CCM imeacha misingi yake muhimu badala ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi imekuwa kimbilio la wafanyabiashara na wezi wa mali ya umma.Wananchi wengi baada ya kuanza mfumo wa vyama vingi hawakujua CCM ya Nyerere ilishakufa na mwasisi wake siku nyingi.Kitendo cha CCM kuwateua wananchama wake wenye tuhuma nzito kugombea nafasi za ubunge na udiwani kiliwastua wanchi wengi ambao kwa kiasi fulani bado walikuwa wamelala kuamka na kutoa maoni yao kupitia masanduku ya kura.


Mkuu vyombo vya habari vimesaidia sana wananchi/wapiga kura kujua nchi inakwenda wapi.Magazeti hasa Raia Mwema,Mwanahalisi,Mwananchi na Nipashe yametoa mchango mkubwa sana ilifika mahali serekali ikatishia kulifungia mwananchi.Mitandao mbali mbali hasa Jamiiforums havikubaki nyuma.

Misuguano baina ya wanaCCM kwa kiasi kikubwa ilitoa nafasi na uwanja mzuri wapinzani kufanya vizuri.Mfano jimbo la Arusha mjini kulikuwa na kambi mbili moja ya mbunge aliyeshindwa kwenye kura za maoni Bwana Felex Mrema na nyingine ya CCM Lowasa.
 
bwa ha ha ha ha kigeu geu huyo...sasa utamsikia anasema mnyika ni mshikaji wake wa siku nyiiiingi....pheew
bbbwwaahahaaaaaaa.... hahahaaaa... UMEPATIA SANA

atasema alikua anmwendesha alipokua anakuja bongo na wanapata soda pamoja

bbhwaaaaa hahaha ahahaaaaa:hurt:
 

Nimeipenda hii ..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…