Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wanabodi,
Siku ya jana Steven Mutambi, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya TAMISEMI alikuwa akizungumza kwenye mahojiano pale Crown FM na moja ya kauli ambayo alitoa ni kuwa kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu, ule utaratibu wa mwaka 2020 kwamba wagombea watapita bila kupingwa umeondolewa.
Soma pia: Licha ya Mapungufu, Sheria Mpya ya Uchaguzi Pia ina Mazuri Yake!, Imerejesha Mamlaka ya Uchaguzi kwa Wananchi, Hakuna Kupita Bila Kupingwa!.
Akizungumzia kuhusu utaratibu, Steve alidokeza kuwa tofauti na mwaka 2020 kwenye Uchaguzi huu, hata kama kutakuwa hakuna wagombea kutoka vyama vingine waliojitokeza kuwania nafasi, huyo mgombea mmoja aliyebaki atatakiwa kupigiwa kura ya ndio au hapana.
"Na niombe sana wananchi wajitokeze kwa sababu katika kanuni zinazoongoza uchaguzi wetu safari hii hakuna kupita bila kupingwa. Itafika hatua vyama vya siasa vitaleta wagombea na atakapopatikana mgombea mmoja bado tutatoa fursa kwa wananchi wetu kumpigia kura ya ndio au hapana."
Wakuu mnaonaje utaratibu huu kutoka kwa TAMISEMI ni mzuri au ndo blah blah za kawaida za CCM?
Siku ya jana Steven Mutambi, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya TAMISEMI alikuwa akizungumza kwenye mahojiano pale Crown FM na moja ya kauli ambayo alitoa ni kuwa kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu, ule utaratibu wa mwaka 2020 kwamba wagombea watapita bila kupingwa umeondolewa.
Soma pia: Licha ya Mapungufu, Sheria Mpya ya Uchaguzi Pia ina Mazuri Yake!, Imerejesha Mamlaka ya Uchaguzi kwa Wananchi, Hakuna Kupita Bila Kupingwa!.
Akizungumzia kuhusu utaratibu, Steve alidokeza kuwa tofauti na mwaka 2020 kwenye Uchaguzi huu, hata kama kutakuwa hakuna wagombea kutoka vyama vingine waliojitokeza kuwania nafasi, huyo mgombea mmoja aliyebaki atatakiwa kupigiwa kura ya ndio au hapana.
"Na niombe sana wananchi wajitokeze kwa sababu katika kanuni zinazoongoza uchaguzi wetu safari hii hakuna kupita bila kupingwa. Itafika hatua vyama vya siasa vitaleta wagombea na atakapopatikana mgombea mmoja bado tutatoa fursa kwa wananchi wetu kumpigia kura ya ndio au hapana."
Wakuu mnaonaje utaratibu huu kutoka kwa TAMISEMI ni mzuri au ndo blah blah za kawaida za CCM?