Uchaguzi serikali za mitaa uunganishwe na Uchaguzi Mkuu - Policy Forum's advice

Uchaguzi serikali za mitaa uunganishwe na Uchaguzi Mkuu - Policy Forum's advice

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925
attachment.php

Mwenyekiti Kikundi kazi serikali za Mitaa kilicho chini ya Taasisi Policy Forum Bwana Hebron Mwakagenda (kushoto)
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu pendekezo uchaguzi serikali za mitaa kuunganishwa na uchaguzi Mkuu

Wajumbe wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum, wamependekeza uchaguzi wa serikali za mitaa ufanyike mwakani pamoja na uchaguzi mkuu kama ilivyofanya Kenya na Zimbabwe. Mwenyekiti wa Kikundi hicho ambacho kinawakilisha zaidi ya asasi za kiraia 70, Hebron Mwakagenda, alitoa kauli hiyo katika mkutano uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo, Mwakagenda alisema wanamuunga mkono Rais Jakaya Kikwete kuwa, taifa lipo kwenye mtikisiko kuhusiana wa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya. Alisema wanatambua Tamisemi siyo chombo mahususi cha kuendesha chaguzi nchini hivyo wamependekeza uchaguzi wa serikali za mitaa usimamiwe na kuendeshwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kwa sasa wapate nafasi ya kubadilisha sheria za uchaguzi na kufanya maandalizi mengine ili uchaguzi uwe huru.

Alisema kutokana na umuhimu wa uchaguzi huo wameamua kutoa mchango wao katika mchakato huo. Alisema serikali za mitaa zinalenga kupeleka au kuyasogeza madaraka kwa jamii ili kufanya maamuzi, kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma kulingana na matakwa ya wananchi.

“Mchakato wa uchaguzi huu unategemea mchakato wa katiba mpya ambao umepoteza ratiba yake ya awali kwa kuwa ingetakiwa kuzinduliwa Aprili 26, mwaka huu lakini upo njia panda,”alisema na kuongeza: Mwakagenda alisema wanapenda kufahamu uchaguzi huo utafanyika lini kwa kuwa kwa kawaida kipindi kama hiki kanuni za uchaguzi huwa zimeshaandaliwa na kutolewa.

Alisema kanuni hizo kazi yake kubwa ni kutoa mwongozo na taratibu wa jinsi serikali za mitaa zitakavyoendeshwa.

Pia alisema kikundi chao kinapenda kujua kama kanuni hizo kama zimeandaliwa, ziliandaliwa na chombo gani na ushiriki wa wadau ulikuwaje. “Tumeona kwenye vyombo vya habari mkutano wa vyama vya siasa na Tamisemi uliofanyika Morogoro hivi karibuni ambao uliandaa kanuni za uchaguzi wa serikali ambapo kama wadau toka mashirika yasiyo ya kiserikali hatujashirikishwa,” alisema.
 

Attachments

  • MMGM8382.jpg
    MMGM8382.jpg
    46.6 KB · Views: 611
Hizi sababu hazina mvuto. hata uchaguzi wa 2015 hautatumia katiba hii mpya kwa ukamili. Tusipende kujidanganya kwa kuweka malengo yasiyotekelezeka kirahisi.
 
Hizi sababu hazina mvuto. hata uchaguzi wa 2015 hautatumia katiba hii mpya kwa ukamili. Tusipende kujidanganya kwa kuweka malengo yasiyotekelezeka kirahisi.

Kuhusu gharama za kuendesha uchaguzi huoni kama zitapungua kama uchaguzi utafanywa kwa wakati mmoja?
 
Hizi sababu hazina mvuto. hata uchaguzi wa 2015 hautatumia katiba hii mpya kwa ukamili. Tusipende kujidanganya kwa kuweka malengo yasiyotekelezeka kirahisi.
Tatizo la maoni na mapendekezo mengi ya katiba yanatoka kwa wahusika wenyewe yaani kama vile daktari au mgonjwa wajipangie utaratibu wao. Mtumishi wa serikali za mitaa anatoa maoni yake ktk kuunda katiba inanitia shaka ni kwa muanufaa yake au ya taifa badala ya mtumishi wa serikali kutoa maoni juu ya sheria za utumishi ili kudai uhuru na haki za watumishi wa serikali.
 
Kuhusu gharama za kuendesha uchaguzi huoni kama zitapungua kama uchaguzi utafanywa kwa wakati mmoja?
Upungufu wa gharama hashabihiani na upotevu wa haki. Kama umepangiwa kuongoza miaka mitano, si haki ukiongoza miaka sita. Unless kuna sababu kama za majanga makubwa n.k.
hata hivyo, sababu iliyotolewa ni katiba mpya, which is bogus.
 
Upungufu wa gharama hashabihiani na upotevu wa haki. Kama umepangiwa kuongoza miaka mitano, si haki ukiongoza miaka sita. Unless kuna sababu kama za majanga makubwa n.k.
hata hivyo, sababu iliyotolewa ni katiba mpya, which is bogus.

Kunapotokea mabadiliko kuna wanaoumia na wapo wa kufufarijika tokana na mabadiliko ya dharura ili mambo baadaye yaende vema. Nchi nyingi zilifikia hatu ambayo sisi tunayo sasa kufikiria manufaa ya mbele zaidi badala yakuangalia effect ya sasa. Binafsi naona ni mpango mzuri ukikubalika tuwe na kipindi kimoja cha uchaguzi ambacho huunganisha chaguzi zote kuanzia serikali za mitaa, wabunge hadi Rais. Kinachotakiwa ni kuwaelimisha wapiga kura manufaa yake.
 
Back
Top Bottom